Tuesday, July 23, 2019

TUMIA SIMU KUUZA.

Simu yako ni nguvu kubwa sana ya kukuwezesha kuwafikia wateja wengi na kuwauzia pia. Itumie simu yako kama kifaa cha masoko na mauzo kwa kuwasiliana na wateja wako kabla na baada ya kununua.
Kila mteja anayefika kwenye biashara yako au anayejibu kutokana na matangazo yanayotolewa na biashara, taarifa zake zinapaswa kuhifadhiwa. Hifadhi namba zao za simu na tengeneza mpango wa kuwa unawapigia simu wateja wako.
Kwa wale ambao hawajanunua wapigie kuwaeleza manufaa ya kile unachouza na kuwashawishi kuja kununua. Kwa ambao wameshanunua wapigie kujua wanaendeleaje na kile walichonunua kimewafaaje.
Kwa kutumia simu yako vizuri utaweza kuwafikia wateja wengi na kuuza zaidi.
Njia bora ya kuandaa mpango huu wa simu ni kurusha matangazo ambayo yanawataka wateja wako kupiga simu, kutuma ujumbe au kuja kwenye biashara yako. Na mteja akishakutafuta, basi tunza mawasiliano yake, hasa simu na hapo utaendelea kuyatumia kwa masoko na mauzo zaidi.

No comments:

Post a Comment