Saturday, April 18, 2020

UJASIRIAMAARIFA , BIDHAA 10 ZA KIDIJITALI UNAZOWEZA KUUZA MTANDAONI NA KUINGIZA KIPATO.

Kuna bidhaa nyingi za kidijitali unazoweza kuuza mtandaoni na ukaingiza kupato kwa muda mrefu. 

1. Vitabu

2. Makala

3. Picha

4. Michoro

5. Muziki

6. Ushauri

7. Kozi

8. Ukocha

9. Blog

10. Matangazo.

Tumia mtandao wa intaneti kwa manufaa, jua jinsi ya kuingiza kipato mtandaoni kwa kutumia blog.

Thursday, April 16, 2020

UJASIRIAMAARIFA , LIPWA KWA MAARIFA NA TAARIFA ULIZONAZO.

Tunaishi kwenye zama za  TAARIFA  na  / MAARIFA ,Hivyo mwenye maarifa na taarifa zenye manufaa makubwa kwa wengine, ndiyo wanaonufaika sana.Na hapo kuna aina mpya ya ujasiriamali ambao unahusisha maarifa, ambao tunauita UJASIRIAMAARIFA.Kupitia ujasiriamali huu, unaweka maarifa na taarifa ulizonazo kwenye kifurushi ambacho wengine wanaweza kununua kama nakala ngumu (HARDCOPY ) au tete.( SOFTCOPY )

Unaweza kujifunza kwa kina kuhusu ujasiriamaarifa katika   Mada  ya  JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA MTANDAONI KWA KUTUMIA BLOG.  Una maarifa na taarifa nyingi, anza kuziuza sasa .

 WASILIANA  NA  KOCHA  MWL  JAPHET MASATU AKUTENGEHEZEE  BLOG  YAKO LEO NA  UJUE  JINSI YA  KUFANYA  HIVYO. ----- Call / SMS / WhatsApp / +255 716924136 /  + 255 755 400128  / + 255 688361539

UZALISHAJI NI SANAA--JINASUE KUTOKA KWENYE MAARIFA YA KAWAIDA----NS DR. KZUO INAMORI---- ( PDF )

WANAWAKE NA NDOA ZA MATESO----NA MUNGA TEHENAN----- ( PDF )

Wednesday, April 15, 2020

JINSI YA KULIPWA UKIWA NYUMBANI----ONGEA NA KOCHA / COACH MWL JAPHET MASATU

Watu wengi wamezoea biashara ni mpaka utoke nyumbani na kwenda kwenye ofisi au eneo jingine la biashara na ukutane na wateja.

Lakini mapinduzi ya kiteknolojia yameshabadili hilo.
Sasa unaweza kufanya biashara na kulipwa ukiwa nyumbani kwako, bila hata ya kukutana na wateja.
Hii ni kupitia mtandao wa intaneti.
Hatua ya kwanza ya kulipwa mtandaoni, ni kuwa na blog.
Blog ndiyo inakuwa duka lako la mtandaoni, ambapo wale wenye uhitaji wa unachotoa watakuja na kukutana na wewe.
Baada ya hapo, kuna namna ya kuwapa thamani zaidi na wao wakakulipa.

 HUHITAJI   MTAJI  ILI  KUANZA .
Uzuri ni kwamba, kuigiza kipato mtandaoni kwa kutumia blog huhitaji kuwa na mtaji wowote wa kuanzia, kama unaweza kusoma hapa, basi kifaa hicho hicho unachotumia kusoma ndiyo unaweza kukitumia kuendesha blog yao.
Kama unatumia kompyuta hiyo hiyo inakutosha kufanya biashara hii. Na hata kama unatumia simu pekee, inakutosha sana kuweza kufanya biashara hii.
Unachohitaji kuwa nacho ni kitu kinachoongeza thamani kwenye maisha ya wengine na utayari wa kutoa thamani hiyo halafu kuwa na njia bora ya kulipwa na baada ya hapo kuweka kazi hasa.

JE , WAHITAJI   KUWA   NA   BLOG    YAKO  ???  WASILIANA  NA   KOCHA   MWL  JAPHET  MASATU   ------ 0716 924136 /   0755 400128 / 0688  361 539

Monday, April 13, 2020

FURSA 35 ZA BIASHARA KATIKA SEKTA YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA ------FURSA AFRIKA MASHARIKI BLOG

VIPAUMBELE VYAKO NI VIPI ? KAMA UNATAKA KITU KIFANYIKE , MPE MTU ALIYE BIZE

Huwa tunajidanganya kwamba hatuna muda wa kufanya vitu kwa sababu tupo bize.

Ila ukweli ni kwamba, kama kuna kitu unataka kufanya, basi utakifanya vizuri ukiwa bize kuliko ukiwa hauko bize.
Angalia, kipindi kama hiki ambapo watu wengi hawana kazi nyingi za kufanya, ungetegemea uwe ndiyo watu wangeutumia muda huu vizuri kusoma na kujifunza.


Lakini waangalie watu wanafanya nini, kufuatilia habari na mitandao siku nzima.


Hali hii inasababishwa na kukosa vipaumbele.
Unapokuwa bize unajiwekea vipaumbele na kukazana kuvifikia.
Lakini unapokuwa haupo bize, unakosa vipaumbele, hivyo hata kitu kidogo kinakushinda kufanya.

Monday, April 6, 2020

UMEZALIWA ILI UFANIKIWE / YOU ARE BORN TO SUCCEED . HUFANIKIWI KWA SABABU ZIFUATAZO :--

 Mambo kumi ( 10 ) unayopenda kufanya kila siku, ambayo yanakuzua isifikie ushindi wako :--
( 1 ). HUJACHAGUA  KUWA  MSHINDI.
Hatua ya kwanza kuchukua ili kufikia ushindi kwenye maisha yako, ni kuchagua ushindi unaotaka kwenye maisha yako. Upo usemi kwamba kama hujui unakokwenda, njia yoyote itakuwa sahihi kwako. Hivi ndivyo wengi wanaendesha maisha yao, hawajui wanataka nini, ila wako bize kweli kweli.
Chagua leo unataka ushindi wa aina gani kwenye maisha yako ili uweze kuchukua hatua sahihi za kukufikisha kwenye ushindi huo.
( 2 ). HUJACHUKUA  JUKUMU  LA  MAISHA  YAKO.
Kama umewahi kulalamika au kumlalamikia mtu mwingine juu ya jambo lolote linalohusu maisha yako, basi jua unajizuia kushinda. Washindi wanachukua jukumu la maisha yao kwa asilimia 100. Chochote kinachotokea kwenye maisha yao, wanajua wa kwanza kulaumiwa na kulalamikiwa ni wao wenyewe. Kulalamika na kulaumu ni rahisi, lakini inakufanya ujione usiye na hatia na uwezo wa kupambana kwenye maisha yako.
Amua leo kushika hatamu ya maisha yako, chukua jukumu la maisha yako kwa asilimia 100 kwa kutokulalamika au kumlaumu yeyote.
(3 ). HUAMINI  KWAMBA  UNAWEZA  KUSHINDA / KUFANIKIWA.
Unapokutana na changamoto kidogo, unakata tamaa na kuona safari ya mafanikio haiwezekani. Watu wanapokupinga na kukukosoa unawasikiliza na kuona wapo sahihi kuliko wewe. Na hilo limekuwa kikwazo kwako. Ushindi unataka ujiamini kupitiliza, uamini unaweza kufanya chochote unachopanga, licha ya ugumu au changamoto unazopitia. Na ukweli ni kwamba, ukiamini na kuamua, hakuna kinachoshindikana.
Jiamini kwamba unaweza kushinda, licha ya magumu na changamoto unazopitia, endelea kuweka juhudi na utafikia ushindi mkubwa. 
( 4 ). HUNA  MALENGO  YANAYOPIMIKA.
Dhana yako ya malengo ni potofu, kwa sababu unajiambia tu kwamba mwaka huu nitafanikiwa zaidi, nitaongeza kipato, nitaanzisha biashara na kadhalika. Kujiambia kauli kama hizo siyo malengo, bali ni matamanio. Malengo ni pale unapopanga nini unataka, kwa kiwango gani na kufikia lini. Kama umepanga kuanza biashara, unajiambia kabisa ni biashara ya aina gani na utakuwa umeianza kufikia tarehe gani. Kama huwezi kupima malengo, huwezi kuyafikia.
Weka malengo yanayopimika na kila siku jipime kwa malengo hayo, gawa malengo hayo kwenye hatua za kuchukua na kila siku chukua hatua hizo bila kuacha na utafika kwenye ushindi.
( 5 ) . UMEKOSA   UAMINIFU.
Umekuwa unasikiliza kauli za wale walioshindwa, ambao wanaamini wale waliofanikiwa kuna namna wamefanya. Utawasikia masikini wakisema matajiri ni wezi na walaghai. Utawasikia wasioweka juhudi wakisema waliofanikiwa wana bahati. Wengine wanakuja kwako na njia za mkato za kufanikiwa, ambazo hazihitaji kazi yoyote. Wewe kwa kutokuijua misingi ya mafanikio, unaingia kwenye mitego hiyo, kinachotokea ni unajikuta unapoteza muda wako na hakuna hatua unazopiga.
Chagua kuwa mwaminifu, kufanya kile kilicho sahihi kulingana na misingi ya mafanikio na siyo kudanganyika au kufuata mkumbo. Njia zisizo sahihi zinaweza kukupa ushindi, lakini hautadumu. 
(6). HUWEKI  KAZI.
Umesikiwa watu wanakuambia usifanye kazi kwa nguvu, bali fanya kwa akili, wana kiingereza chao wanakuambia Don’t work hard, work smart. Ni uongo, hakuna ushindi unaopatikana bila kuweka nguvu na akili, tena kwa viwango vya juu sana. Watu wengi ni mashabiki na wafuatiliaji wa michezo mbalimbali. Nitajie mchezaji mmoja unayemkubali sana, ambaye wakati wenzake wanaenda kwenye mazoezi ya nguvu, yeye anafanya mazoezi kwa akili? Hakuna. Halafu wewe unajidanganya kwamba unaweza kufikia ushindi kwa akili bila nguvu!
Amua kuweka kazi, kazi hasa na siyo ya kitoto. Fanya kazi kwa juhudi na maarifa, nenda hatua ya ziada, toa thamani kubwa na ushindi utakuwa wako.
(7 ). HUTHAMINI  MUDA  WAKO.
Unauchukulia muda wako poa sana, unautawanya kama vile una chemchem ya muda isiyo kauka. Unapoteza muda wako wa thamani kwenye mambo yasiyo na mchango wowote kwenye ushindi wako, kwa sababu hujui hata thamani ya muda huo. Unahangaika na habari mbalimbali, umbeya, udaku, maisha ya wengine na mengine mengi. Halafu unakuja kulalamika kwamba huna muda wa kufanya zaidi yale uliyopanga kufanya.
Upe muda wako thamani, jua ni kiasi gani cha kipato unataka kupata, kisha kigawe kwa masaa na jua saa yako moja ina thamani ya shilingi ngapi. Hivyo unapopoteza muda, unajua kabisa ni kiasi gani cha pesa umepoteza.
(8 ). UNASIKILIZA  SANA  HOFU  ZAKO.
Hakuna mtu asiyekuwa na hofu, ila wewe unazisikiliza sana hofu zako, hivyo huthubutu kufanya kitu chochote kipya na kikubwa, kwa sababu unahofia kushindwa. Wanaoshinda wanapata hofu kama zako, lakini wanajua dawa ya hofu ni kufanya. Kuwa na hofu ni kawaida, ila kuzisikiliza hofu zako na kuzifuata ni kuchagua kuukosa ushindi.
Amua leo kuchukua hatua kwenye yale unayohofia, kwa sababu ndiyo yamebeba mafanikio yako na dawa ya hofu ni kufanya unachohofia.
( 9 ). HUJIFUNZI  KILA  SIKU.
Unapata muda wakula mara tatu kwa siku, kufuatilia habari, kufuatilia maisha ya wengine na kulala, lakini unajiambia huna muda wa kusoma vitabu. Hapo ndipo unapoagana na ushindi wako. Kwa sababu hakuna mshindi ambaye hajifunzi kila siku. Moja ya mahitaji ya maisha ya ushindi ni kila siku kuwa bora kuliko siku iliyopita, na ubora pekee utaupata kupitia kujifunza kila siku na kufanyia kazi yale unayojifunza.
Chagua sasa kujifunza kila siku, haijalishi siku yako imebana kiasi gani, hakikisha unatenga muda wa kujifunza kupitia usomaji wa vitabu na mafunzo ya aina nyingine. Usikubali siku ipite hujajifunza kitu kipya.
( 10 ). BADALA  YA  KUZALISHA  MATOKEO , UNAZALISHA  SABABU.
Kabla hata hujaanza kufanya kitu, tayari umeshatengeneza sababu za kujitetea utakaposhindwa kwenye kitu hicho. Hivyo badala ya kuweka nguvu zako kubwa kuzalisha matokeo ya ushindi unayotaka, unapeleka nguvu hizo kuzalisha sababu za kujitetea. Huwezi kuzalisha sababu na matokeo kwa pamoja, chagua kuzalisha sababu na kuachana na matokeo au kuzalisha matokeo na kuachana na sababu.
Kataa kuwa mtu wa sababu, kuwa mtu wa kujisukuma kwa kila namna kupata matokeo unayotaka, usiwe mtu wa kukimbilia sababu.

FURSA 19 ZA BIASHARA KATIKA SEKTA YA BURUDANI.------" FURSA AFRIKA BLOG "

FURSA 33 ZA BIASHARA KATIKA SEKTA YA MICHEZO NA UTAMADUNI----- " FURSA AFRIKA MASHARIKI BLOG "

Saturday, April 4, 2020

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : JIANDAE KWA MABADILIKO MAKUBWA YANAYOKUJA.

Kuna watu wanasema kwamba ugonjwa huu wa Corona ni mwisho wa dunia. Hilo ni kweli, lakini siyo kwa wanavyomaanisha wao. Corona siyo mwisho wa dunia kwamba watu wote watakufa. Ila Corona ni mwisho wa dunia kwamba baada ya janga hili kupita, dunia mpya itazaliwa, kila kitu kitabadilika.

Hakuna chochote kitakachobaki kama kilivyokua kabla ya Corona. Kuanzia mfumo wa afya, mfumo wa uchumi, ushirikiano wa kimataifa, ufanyaji kazi wa watu na hata tabia za wateja.
Watu kufanyia kazi majumbani kutaongezeka, matumizi ya fedha za noti na sarafu yatapungua, tabia ya watu kunawa mikono itaendelea na mengine mengi ambayo yanasisitizwa sana kipindi hiki.
Hivyo angalia ni jinsi gani biashara yako inaathirika na yale yanayoendelea sasa, kisha usijipe moyo kwamba hali hii itapita na biashara zitarudi kawaida. Jua kwamba hii ndiyo kawaida mpya.
Iandae biashara yako kuendana na mabadiliko yaliyopo sasa na mengine makubwa zaidi yanayokuja. Kufanya biashara kwa ukawaida na mazoea kumefika ukomo. Huu ni wakati wa mabadiliko, hivyo badilika la sivyo utakufa.

Mfano; biashara ambazo zilikuwa zinasubiri wateja kwenda kununua, zinapaswa kubadilika na kuweka mfumo wa wateja kuagiza na kisha kupelekewa au kutumiwa.

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : WSAIDIE WATEJA WALIOKWAMA

Huu ndiyo wakati mzuri kwako mfanyabiashara kuwaonesha wateja waaminifu kwako kwamba biashara yako inawajali, haiangalii tu kuingiza faida, bali inataka mteja aendelee kuwepo.
Kuna baadhi ya wateja wako watakuwa wamekwama kutokana na hali inavyoendelea, iwapo watakueleza kukwama kwao na ukawa na njia ya kuwasaidia, wafanya hivyo. Kwa sababu usipowasaidia na wao wakashindwa, basi biashara yako itakuwa imepoteza mteja moja kwa moja.

Mfano; kama kuna wateja umekuwa nao kwa muda mrefu na wamekuwa walipaji wazuri bila kusumbua, ila kipindi hiki wameshindwa kulipa kwa wakati, wape nafasi ya kuchelewa kulipa au kulipa kwa viwango tofauti na awali kama ipo ndani ya uwezo wako.

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : MIKAKATI YA UKUZAJI BIASHARA IENDELEE.

Wakati wa majanga kama haya, wengi huacha kufanyia kazi mikakati yao ya ukuzaji wa biashara. Kwa kuwa hali ya uchumi inakuwa siyo nzuri, wateja siyo wengi na waliopo hawanunui sana, wafanyabiashara huona hakuna haja ya kujisumbua, badala yake wanasubiri mpaka mambo yawe vizuri.
Kama tulivyoona mpaka sasa, hakuna mwenye uhakika mambo yatarudi sawa lini, inaweza kuwa kesho, wiki ijayo, mwezi ujao au mwaka ujao, hakuna ajuaye.
Hivyo wewe endelea na mikakati yako ya ukuzaji wa biashara kama vile hakuna mlipuko unaoendelea.
Endelea na mkakati wako wa masoko kwenye matangazo na hata kuwatembelea wateja kule walipo, mtaa kwa mtaa, ofisi kwa ofisi na nyumba kwa nyumba. Ila hakikisha unajikinga na kuikinga timu yako.
Endelea na mkakati wa mauzo kwa kuwashawishi wateja kununua na kununua zaidi ya walivyopanga kununua.
Endelea na mkakati wa utoaji wa huduma bora sana kwa wateja wako ili wanunue tena kwako na wawaambie watu wao wa karibu kununua
Mikakati hii inapaswa kufanyiwa kazi kila siku, iwe kuna majanga au hakuna. Hata kama huoni matokeo yake kwa haraka, usiache kufanya.

Mfano; mikakati ya masoko, mauzo na huduma kwa wateja kwenye kila biashara inapaswa kuendelea kama vile hakuna kilichobadilika, ila iendane na hali halisi ilivyo sasa.

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : JIHAKIKISHIE UPATIKANAJI WA MALI NA / AU MALIGHAFI.

Kama unafanya biashara ya kununua kwa jumla na kuuza kwa reja reja, unapaswa kujihakikishia upatikanaji wa mali katika kipindi hiki cha mlipuko. Kutokana na mipaka ya nchi nyingi kufungwa na shughuli kusimamishwa, hili linaathiri sana uzalishaji. Hivyo jipange mapema kwa kuhakikisha una mzigo wa kutosha katika kipindi cha mlipuko.
Kama unafanya biashara ya kuzalisha bidhaa, basi jihakikishie upatikanaji wa malighafi katika wakati huu wa mlipuko. Mabadiliko yanayoendelea yataathiri sana upatikanaji wa malighafi, jipange kwa kuhakikisha hilo haliathiri uzalishaji wako.

Mfano; wafanyabiashara wa bidhaa zinazotoka nje, kama nguo kutoka china, wamejikuta katika wakati mgumu kupata mzigo mpya tangu mlipuko huu uanze. Hivyo ni muhimu kuangalia njia nyingine ya kupata mzigo na kuhakikisha unapata mzigo wa kutosha kwa sababu hujui mlipuko huu utaisha lini.

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : TOA ELIMU NA USHAURI SAHIHI KWA WATEJA WAKO,

Kwenye mlipuko unaoendelea sasa, kila mtu ni mwalimu, mshauri na mtaalamu wa magonjwa ya mlipuko. Hata mtu ambaye mwezi mmoja uliopita alikuwa hajui (na huenda mpaka sasa) hajui kwamba kirusi siyo kiumbe hai kamili, ni mshauri mzuri sana kwa wengine kuhusu mlipuko unaoendelea.

Wewe wape wateja wako elimu sahihi, ambayo umeitoa kwenye vyanzo sahihi. Usilete ujuaji wako au kukusanya taarifa za mtandaoni na kufikiri hiyo ni elimu. Nenda kwenye vyanzo vya uhakika, na kwa hili la Corona, sikiliza taarifa za serikali na tembelea tovuti ya Shirika la Afya Duniani (WHO), kwa anuani www.who.int kupata elimu sahihi kuhusu mlipuko huu wa Corona.
Mfano; kuna vitu vingi ambavyo watu wanashauriana kufanya, ambavyo siyo sahihi. Kwenye tovuti ya WHO, kuna kipengele wanakiita MYTH BUSTERS ambapo wanatoa ukweli kuhusu vitu visivyo sahihi wanavyoshauriana watu. Kama ulaji wa vitunguu hauzuii maambukizi ya Corona. Ingia kwenye tovuti hiyo, pata taarifa sahihi na kisha washauri wateja wako kwa usahihi.

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : USITUMIE NAFASI HII KUNUFAIKA ZAIDI.

Katika hali ya mlipuko kama huu, ambapo watu hawana uhakika wa lini hali itarudi kama kawaida, wanakimbilia kufanya manunuzi makubwa. Hapa mfanyabiashara unapata tamaa ya kuongeza bei kwa sababu uhitaji ni mkubwa. Watu wanaweza kununua kwa bei juu kwa sababu hawana namna.
Lakini tambua kwamba huu mlipuko utapita, na kama unataka biashara yako iendelee kuwepo na iwe na wateja waaminifu hata baada ya mlipuko huu, usiutumie kujinufaisha zaidi.
Usiongeze bei kwa sababu tu kila mtu anaongeza bei na uhitaji ni mkubwa. Kama ulikuwa na mzigo wa kutosha kabla ya janga hili kuanza, endelea kuuza kwa bei zile zile. Na kama uhitaji ni mkubwa, wape kipaumbele wale wateja ambao umekuwa nao kwa muda mrefu.
Kama mlipuko umepelekea gharama za wewe kupata unachouza kuwa juu, waeleze wazi wateja wako kuhusu mabadiliko hayo. Usikimbilie tu kupandisha bei, jua wateja hawatasahau hilo na watavunja uaminifu kwenye biashara yako baada ya janga hili kupita.

Mfano; wauzaji wa vitu muhimu kama dawa, vifaa vya kujikinga, vyakula na vitu vingine wamekuwa wanapandisha bei katika nyakati kama hizi, wewe usifanye hivyo.

MFANAYABIASHARA / MJASIRIAMALI : JIKINGE WEWE NA TIMU YAKO.

Wewe mfanyabiashara ukiumwa au wasaidizi wako wakiumwa, biashara itaathirika zaidi. Hivyo wewe na timu yako mnapaswa kuwa mstari wa mbele katika kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huu.
Hakikisha njia zote za kujikinga zinajulikana na kutumika na kila anayehusika kwenye biashara yako. Njia kuu zinafahamika, kunawa mikono kwa maji safi na sabuni, kuepuka kushikana, kuepuka kushika uso. Hivi vyote vinapaswa kufanyiwa kazi.
Pia eneo la biashara liboreshwe kwa namna ambayo linapunguza maambukizi. Ukaribu baina yako au watoa huduma na wateja unapaswa kupunguzwa. Maeneo ya kunawa mikono yanapaswa kuwepo au dawa za kusafisha mikono kupatikana kwa urahisi.
Usiache kujilinda wewe na timu yako kwa kuepuka gharama, ukiugua wewe au timu yako, ni tiketi ya kifo kwa biashara yako.

Mfano; kwenye kila eneo la biashara kunapaswa kuwa na sehemu ya watu kunawa mikono kwa maji na sabuni au kwa dawa maalumu. Pia kama biashara inahusisha watu wengi, kuwekwe utaratibu wa kupunguza msongamano wakati huu. Kwenye huduma za afya, watoa huduma wanapaswa kuwa na vifaa vya ziada vya kujilinda wao wenyewe.

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : BADILI MFUMO WA BIASHARA KUENDANA NA MABADILIKO YANAYOTOKEA.

Maisha ya watu yamebadilika katika wakati huu wa mlipuko wa ugonjwa wa Corona. Biashara yako pia inapaswa kubadilika ili kuweza kuwahudumia vizuri wateja wako.
Kama watu wanatumia muda mwingi nyumbani kuliko kutoka, usiendelee kusubiri wateja waje kwenye biashara yako, badala yake wafuate huko majumbani.
Badili mfumo wa biashara yako kutoka kusubiri wateja waje eneo la biashara na kufanya wateja waweze kuagiza wakiwa nyumbani na kupelekewa au kutumiwa kile walichoagiza.
Hatujui lini hali hii itaisha kwa hakika, hivyo usijiambie unasubiri mambo yatulie, badala yake chukua hatua sahihi ili uendelee kuwahudumia wateja wako.

Mfano; biashara ambazo zimekuwa zinategemea wateja waje kwenye biashara, ni wakati sahihi sasa kuweka mfumo wa wateja kuweza kuagiza wakiwa nyumbani na kisha kupelekewa au kutumiwa walichoagiza.

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : WAPE WATEJA WAKO MATUMAINI SAHIHI.

Wakati wa mlipuko kama huu, hakuna anayejua nini kitatokea kesho, na kadiri mambo yanavyozidi kuwa mabaya, ndivyo watu wanaendelea kutabiri kwamba mambo yatakuwa mabaya zaidi.
Watu wanatishana na kupeana wasiwasi mkubwa. Wapo wanaosema huu ndiyo mwisho wa dunia. Kila mtu ana maoni yake. Lakini tunajua kitu kimoja kuhusu maoni, siyo ukweli.
Hakuna aliyeweza kutabiri ujio au madhara ya mlipuko huu, na hakuna anayeweza kutabiri kwa uhakika mambo yataendaje. Tunachojua ni kwamba tutavuka hili, kama ambavyo jamii ya binadamu imevuka mengi siku za nyuma.
Hivyo wewe kuwa chanzo cha matumaini sahihi kwa wateja wako. Katika hali ya wasiwasi kama hii, watu wanapenda kuwasikiliza wale wanaoleta habari njema, lakini siyo habari njema hewa. Bali habari njema sahihi.
Usiwe mtu wa kutoa habari mbaya kwa wateja wako, utawatisha na kuwafanya waahirishe kununua. Badala yake kuwa mtu wa kutoa habari njema, mtu wa kuwapa wateja wako moyo na hapo watajisikia vizuri na kununua. Ukiweza kuwaonesha jinsi kile unachouza kinawasaidia kupunguza makali ya mlipuko, wateja wanakujali zaidi.

Mfano; biashara za ushauri na mafunzo zinapaswa kuwa chanzo cha matumaini kwa wateja wake. Kwa kuwaonesha kwamba hili linaloendelea siyo mwisho wa dunia na mambo yatakwenda vizuri baada ya hili.

MFANYA BIASHARA / MJASIRIAMALI : JUA THAMANI NA WAELEZE WATEJA WAKO

 BIASHARA  pekee zitakazovuka kipindi hiki cha Mlipuko wa ugonjwa wa   CORONA salama ni zile ambazo zinatoa thamani kubwa kwa wateja wake na jamii kwa ujumla. Zile biashara ambazo watu hawawezi kuishi bila ya kuwa na kile kinachouzwa.
Hivyo huu ni wakati wa wewe kukaa chini na kujiuliza ni thamani gani unayoitoa kwa wateja wako. Huenda umezoea kuuza na kupokea fedha na umesahau thamani ipi unatoa.
Jiulize ni tatizo au hitaji gani la wateja ambalo biashara yako inatoa. Kisha waeleze wateja thamani hiyo vizuri, waoneshe jinsi ambavyo wanaihitaji thamani hii wakati huu wa mlipuko.
Mfano; biashara za huduma za kifedha zinatumia nafasi hii kuonesha jinsi ilivyo salama kutuma na kupokea fedha kwa mtandao na siyo fedha taslimu. Hii ni thamani kubwa ambayo mteja au mfanyabiashara hakuwa anaiona, lakini kwa sasa iko wazi.