Saturday, April 4, 2020

MFANYA BIASHARA / MJASIRIAMALI : JUA THAMANI NA WAELEZE WATEJA WAKO

 BIASHARA  pekee zitakazovuka kipindi hiki cha Mlipuko wa ugonjwa wa   CORONA salama ni zile ambazo zinatoa thamani kubwa kwa wateja wake na jamii kwa ujumla. Zile biashara ambazo watu hawawezi kuishi bila ya kuwa na kile kinachouzwa.
Hivyo huu ni wakati wa wewe kukaa chini na kujiuliza ni thamani gani unayoitoa kwa wateja wako. Huenda umezoea kuuza na kupokea fedha na umesahau thamani ipi unatoa.
Jiulize ni tatizo au hitaji gani la wateja ambalo biashara yako inatoa. Kisha waeleze wateja thamani hiyo vizuri, waoneshe jinsi ambavyo wanaihitaji thamani hii wakati huu wa mlipuko.
Mfano; biashara za huduma za kifedha zinatumia nafasi hii kuonesha jinsi ilivyo salama kutuma na kupokea fedha kwa mtandao na siyo fedha taslimu. Hii ni thamani kubwa ambayo mteja au mfanyabiashara hakuwa anaiona, lakini kwa sasa iko wazi.

No comments:

Post a Comment