Monday, May 27, 2019

UONGO TUNAOJIAMBIA KUHUSU MAFANIKIO NA KWA NINI HATUPENDI KUBADILIKA.

 Mwandishi anasema yapo mambo ambayo tumekuwa tunajidanganya sana kwenye mafanikio, na haya ndiyo yamekuwa yanachochea matatizo mengi tunayokutana nayo kwenye maisha. Baadhi ya mambo tunayojidanganya kwenye mafanikio ni haya; Tunajikadiria zaidi kwenye mchango wetu kwa mafanikio ya kile tunachofanya. Tunafikiri bila sisi mafanikio yasingepatikana, huku ni kujidanganya. Tunachukua sifa ambazo hatustahili kuchukua, kazi wamefanya wengine lakini wewe kama kiongozi ndiye unayetaka upewe sifa. Huwa tunajiona tuna ujuzi wa juu kuliko wale wanaotuzunguka. Huwa tunapuuza muda na gharama ambazo tumeshapoteza kwenye miradi ambayo haizalishi. Kukuza matarajio ya mafanikio ya mradi, kuwa na mategemeo makubwa kuliko uhalisia. Uongo huu ambao tumekuwa tunajiambia, hasa tunapokuwa viongozi kwenye kazi au biashara, unaathiri mahusiano yetu na wale walio chini yetu. Uongo huu unakuwa umetokana na mafanikio ambayo tunakuwa tumeyapata huko nyuma. Tunapopata mafanikio kidogo, huwa tunajiamini zaidi ya uhalisia. Kujiamini huku kulikopitiliza ndiyo kunawaingiza wengi kwenye matatizo na kuwazuia kufanikiwa zaidi.

Friday, May 24, 2019

FURSA 10 ZA KUTENGENEZA PESA FACEBOOK ------ " Fursa Afrika Mashariki Blog "

SHAUKU NI NGUVU ITAKAYOKUWEZESHA KUPATA CHOCHOTE KATIKA MAISHA YAKO.


Shauku ndiyo nguvu ya kwanza ya kukuwezesha kupata kile ambacho unataka kwenye maisha yako. Shauku ni ule msukumo wa ndani wa kukutaka upate kile unachotaka. Msukumo ambao hauondoki wala kupungua. Shauku ina nguvu kubwa ya kukusukuma kufanya mambo ambayo wengine wanaogopa, lakini kwako yanaonekana kawaida.

Watu wengi wamekuwa wanategemea hamasa iwafikishe kwenye mafanikio makubwa, lakini tatizo la hamasa ni huwa haidumu, mara kwa mara inabidi uchochee upya hamasa yako. Lakini shauku huwa haipungui wala kuhitaji kuchochewa, shauku unakuwa nayo muda wote na hii ndiyo inakusukuma wewe kupiga hatua zaidi.
 
Shauku inatokana na ile sababu kubwa inayokusukuma kupata unachotaka, ile KWA NINI inayokufanya wewe upambane kupata unachotaka. Kwa nini zinatofautiana kwa watu, wapo ambao wanafanya kwa sababu wamejitoa kuyafanya maisha ya wengine kuwa bora zaidi, wapo ambao wanafanya ili kuwaonesha wengine wanaweza na kadhalika.
 
Hakikisha una msukumo mkubwa ndani yako wa kukupeleka kwenye kile unachotaka, kwa sababu bila ya msukumo huu, hakuna nguvu nyingine itakayoweza kukusaidia kupata unachotaka.

UNAHITAJI KUWA NA KOCHA , MENTA AU MSHAURI ILI UWEZE KUPATA CHOCHOTE UNACHOHITAJI KATIKA MAISHA YAKO

Ili kupata unachotaka, unahitaji kupata mwongozo kutoka kwa mtu mwingine. Mtu huyo anaweza kuwa kocha, menta au mshauri ambaye anakusimamia ufike kule unakotaka kufika.
 
Iko hivi rafiki, sisi binadamu ni wavivu na hatupendi kujitesa. Tunaweza kuweka mipango mikubwa na mizuri sana, lakini tunapokutana na ugumu ni rahisi kuacha na kujiambia haiwezekani au hatuwezi.
 
Lakini unapokuwa na mtu wa pembeni ambaye anakuangalia na kukusimamia, kwanza hutataka kumwangusha, hivyo utajisukuma zaidi na pili yeye mwenyewe hatakubaliana na wewe kirahisi, hivyo itakubidi ujaribu tena na tena na tena kabla hujasema haiwezekani.
 
Watu wengi wamekuwa wanajiwekea malengo peke yao, na asilimia 99 wamekuwa hawayafikii. Ila wale wanaoweka malengo na kuwa na mtu wa kuwasimamia kwenye malengo yao, zaidi ya asilimia 90 wanayafikia.
 
Hii ndiyo nguvu kubwa iliyopo kwa kuwa na mwongozo. Kwa sababu pia mtu anayekuongoza anaweza kukushauri vizuri pale ambapo unakuwa umekwama. Ni rahisi kuona makosa ya mchezaji aliyepo uwanjani ukiwa nje ya uwanja, lakini yule aliyepo uwanjani anaweza asione kwa urahisi. Kuna makosa unaweza kuwa unafanya kwenye maisha yako lakini huyaoni, ila unapokuwa na mtu anayekusimamia, atakuonesha makosa hayo kwa urahisi na utaweza kupiga hatua sana.
 
Unahitaji kuwa na mtu wa kukusimamia kwenye malengo na mipango uliyonayo ambaye atakusukuma kuyafikia.

WATU WANAOKUZUNGUKA WANA MCHANGO MKUBWA SANA KATIKA KUPATA CHOCHOTE UNACHOTAKA


Watu wanaokuzunguka wana nguvu kubwa sana kwako, hata kama hujui. Watu hao, hasa wale wa karibu, wana ushawishi mkubwa kwako. Kama wanaokuzunguka wana mtazamo hasi wa kuona mambo hayawezekani, na wewe pia utajikuta umebeba mtazamo huo, hata kama utakuwa unapingana nao kiasi gani.
 
Na kama watu wanaokuzunguka wana mtazamo chanya wa inawezekana, na wewe pia utabeba mtazamo huo. Nguvu hii ya wanaokuzunguka ni nguvu kubwa sana unayopaswa kuwa nayo makini. Wengi wamekuwa wanapuuza nguvu hii, wakiamini wanaweza kuzungukwa na watu wa aina yoyote lakini wakafanikiwa. Hicho kitu hakipo kabisa, kama haujazungukwa na watu sahihi, huwezi kufanikiwa. Ni asili ya binadamu, hatuwezi kwenda juu zaidi ya wale ambao wanatuzunguka.
 
Hivyo ili kupata kile unachotaka kwenye maisha, tafuta watu wanapiga hatua kwenye maisha yao na uwe nao karibu. Watu ambao wanaamini kwenye ndoto kubwa na wasiokata tamaa. Watu hawa watakupa nguvu ya kuendelea hata pale unapokutana na magumu na changamoto.

UNAPOSHIKWA NA HASIRA , JIPE MUDA WA KUTAFAKARI.

 Ukishagundua kwamba upo kwenye hasira, basi kaa kimya, jipe muda wakutafakari na kutulia na utajiepusha na makosa makubwa unayoweza kufanya ukiwa na hasira.
 
Hasira ni moja ya hisia zenye nguvu sana, na hisia zinapokuwa juu uwezo wetu wa kufikiri unakuwa chini. Hivyo unapokuwa na hasira, unakuwa umetawaliwa na hisia na siyo fikra. Na ni wakati mbaya sana wa kufanya chochote, kwa sababu unaposukumwa na hisia, hujui kipi sahihi kufanya, kwa kuwa hufikiri sawasawa.
 
Hivyo rafiki, unapogundua kwamba una hasira, usifanye chochote.
 
Kama kuna mtu amekukosea na umepatwa na hasira usimjibu wakati una hasira hizo.
 
Kama kuna mtoto wake amekosea usimwadhibu ukiwa na hasira.
 
Ukiwa na hasira usifanye chochote, jipe muda wa kukaa mbali na kile kinachokupa hasira na akili zako zitarudi.

Saturday, May 18, 2019

KILA MTU ANA HAIBA HIZI TATU : UJASIRIAMALI, UMENEJA , UFUNDI , ZIIBUE NA ZIFANYIE KAZI UTAFANIKIWA KATIKA BIASHARA YAKO

( 1 ). MJASIRIAMALI.

Hii ni haiba ambayo inabeba nafsi ya mjasiriamali. Mjasiriamali ni mtu wa kuja na mawazo mapya ya kuzitumia fursa mbalimbali ambazo zinapatikana. Mjasiriamali ni mtu wa ndoto na maono makubwa, mtu wa kutengeneza picha za mambo yasiyoonekana. Mjasiriamali anaangalia mambo yalivyo na kujiuliza vipi kama yangekuwa tofauti.

Bila ya mjasiriamali hakuna mawazo mapya, hakuna ugunduzi na wala hakuna maono makubwa ya kibiashara.

Nafsi ya ujasiriamali ndiyo inawasukuma wengi kuingia kwenye biashara, lakini nafsi hii imekuwa haidumu kwa muda mrefu, inazidiwa nguvu na nafsi nyingine na ndiyo maana tunasema mtu anakuwa amepatwa na kifafa cha ujasiriamali. Wazo la ujasiriamali linamjia kwa muda mfupi na nafsi hii kuondoka kabisa.

( 2 ). MSIMAMIZI/MENEJA.

Hii ni haiba inayobeba nafsi ya usimamizi au umeneja kwenye biashara. Meneja ndiye mtu ambaye anaisimamia biashara kwa ukaribu, kuhakikisha kwamba kila kitu kinakwenda kama kilivyopangwa. Huyu ni mtu ambaye anahakikisha rasilimali za biashara zinatumika vizuri. Pia meneja anahakikisha kilichofanywa kwenye biashara jana ndiyo kinafanywa leo. Mameneja hawapendi kujaribu vitu vipya kwa sababu hawana uhakika navyo.

Tofauti kubwa ya mjasiriamali na meneja ni mabadiliko, mjasiriamali anatafuta mabadiliko na kuwa tayari kuyafanyia kazi. Lakini meneja hataki kabisa mabadiliko, anataka kuendelea kufanya mambo kama ambavyo amekuwa

Meneja ndiyo nafsi inayoiwezesha biashara kufanya kazi. Mjasiriamali anakuwa na mawazo mapya na makubwa, lakini hawezi kuyafanyia kazi mawazo hayo kwa muda. Hivyo anahitaji kuwa na meneja ambaye anafanyia kazi mawazo hayo mapya.

( 3 ).FUNDI/MTAALAMU.

Hii haiba inayobeba nafsi ya ufundi au utaalamu unaohitajika kwenye biashara. Huu ni ule ujuzi au utaalamu ambao mtu anaingia nao kwenye biashara. Fundi kazi yake ni kutengeneza vitu na anapenda sana kutengeneza vitu. Haiba hii ya ufundi inapenda kufanya yale yanayopaswa kufanywa kwenye biashara.

Wakati mjasiriamali anakuja na mawazo mapya, meneja anaweka mfumo mzuri wa kufanyia kazi mawazo hayo, fundi ndiye anayefanya kazi kwenye biashara hiyo na kuzalisha matokeo yanayohitajika. Fundi ndiye anayezalisha matokeo kwenye biashara.

Wednesday, May 15, 2019

KWA NINI SUKARI NI MADAWA YA KULEVYA YALIYOHALALISHWA.

Pamoja na madhara makubwa ya kiafya ya utumiaji wa sukari tutakayojifunza hapo chini, sukari haina tofauti kubwa sana na madawa ya kulevya kama kokeini au heroine.
Hii ni kwa sababu matumizi ya sukari yamedhibitishwa kusisimua sehemu za ubongo ambazo zinasisimuliwa na madawa hayo. Pale mtu anapotumia sukari, ubongo unasisimka na kuzalisha homoni inayoitwa dopamine, hii ni homoni ambayo huwa inaleta raha na kumsukuma mtu kurudia tena kile alichofanya.
Hivyo unapotumia sukari, ubongo unazalisha dopamine, ambayo inakufanya ujisikie vizuri na upate utamu wa sukari. Lakini baada ya hapo unasukumwa kutumia tena sukari ili upate utamu zaidi na kujisikia vizuri zaidi.
Hii ndiyo sababu watu wamekuwa wanapata msukumo mkubwa sana wa kutumia kitu chenye sukari, na wakishatumia mara moja hawawezi kuacha, wanatumia tena na tena na tena.
Matumizi haya ya sukari yanaleta hali ya uteja au uraibu ambao ni mgumu sana kuuvunja. Kila mtu anapoona kitu cha sukari akili yake haifikirii kitu kingine chochote bali jinsi ya kupata sukari hiyo. Na anapoonja mara moja, hawezi kujizuia bali atataka tena na tena.
Tafiti zinaonesha pia ya kwamba matumizi ya sukari yamekuwa yanabadili tabia za watu. Muda mfupi baada ya kutumia sukari watu wengi huwa wakorofi, wenye hasira na wasio na subira. Sukari inawapa nguvu za ziada ambazo zinawasukuma kuzitumia kwa njia ambazo siyo sahihi. Mtu anapokuwa na sukari nyingi kwenye mwili huwa kwenye hali ya msongo kama mtu ambaye ametumia kilevi.
Hivyo kwa uwezo wa sukari kusisimua ubongo kama madawa mengine, kitendo cha watu kuwa tegemezi kwenye sukari na kuadilika kwa tabia baada ya mtu kutumia sukari, kunaifanya sukari kuwa kwenye kundi moja na madawa ya kulevya.

HATUA SAHIHI KWAKO KUCHUKUA KUHUSU SUKARI.

Rafiki, kama kuna hatua moja ambayo unapasa kuichukua, hata kama utashindwa kuchukua hatua nyingine zozote kwenye ulaji wako, basi ni kuachana kabisa na sukari. Yaani acha kabisa kutumia sukari, na utaupumzisha mwili wako na hali hii ya kutengeneza sumu ambazo zinakuchosha, kukuletea magonjwa na hata kukuzeesha haraka.
Vyakula vya sukari vya kuepuka ni kama ifuatavyo, sukari yoyote unayoongeza kwenye chai au chakula, asali, miwa na juisi yake, matunda yoyote yenye utamu wa sukari, soda, juisi za matunda hata kama ni asili, bia, mvinyo, bidhaa zozote za kiwandani ambazo zimetengenezwa kwa kuongezwa sukari, kama mikate, maandazi na chochote ambacho kimeongezwa sukari.
Pia punguza sana matumizi yako ya vyakula vya wanga, kwa kula kiasi kidogo sana na mara moja kwa siku, hasa mlo wa jioni au usiku. Sehemu kubwa ya chakula chako inapaswa kuwa mafuta sahihi, protini na mbogamboga.
Nyongeza; usidanganyike na vitu vitamu ambavyo unaambiwa havina sukari, mfano soda za dayati, hizi zina kemikali ambazo ni sumu kwenye mwili wako kama ilivyo sukari. Tofauti yake na soda nyingine ni kwamba hazipandishi sukari kwenye damu, lakini bado ni sumu.
Najua hili litakuwa limekustua sana, kwa sababu vyakula vingi hapo ndiyo unatumia kila siku. Lakini kutumia kila siku au kuzoea haifanyi kuwa sahihi. Tafiti za kisayansi na za lishe zinaonesha wazi kwamba mazoea yetu kwenye ulaji ndiyo kikwazo kwetu kuwa na afya bora. Hivyo tunapaswa kujifunza na kuchukua hatua sahihi ili tuwe na afya bora na maisha bora pia.

KWA NINI SUKARI NI MADAWA YA KULEVYA YALIYOHALALISHWA.

Pamoja na madhara makubwa ya kiafya ya utumiaji wa sukari tutakayojifunza hapo chini, sukari haina tofauti kubwa sana na madawa ya kulevya kama kokeini au heroine.
Hii ni kwa sababu matumizi ya sukari yamedhibitishwa kusisimua sehemu za ubongo ambazo zinasisimuliwa na madawa hayo. Pale mtu anapotumia sukari, ubongo unasisimka na kuzalisha homoni inayoitwa dopamine, hii ni homoni ambayo huwa inaleta raha na kumsukuma mtu kurudia tena kile alichofanya.
Hivyo unapotumia sukari, ubongo unazalisha dopamine, ambayo inakufanya ujisikie vizuri na upate utamu wa sukari. Lakini baada ya hapo unasukumwa kutumia tena sukari ili upate utamu zaidi na kujisikia vizuri zaidi.
Hii ndiyo sababu watu wamekuwa wanapata msukumo mkubwa sana wa kutumia kitu chenye sukari, na wakishatumia mara moja hawawezi kuacha, wanatumia tena na tena na tena.
Matumizi haya ya sukari yanaleta hali ya uteja au uraibu ambao ni mgumu sana kuuvunja. Kila mtu anapoona kitu cha sukari akili yake haifikirii kitu kingine chochote bali jinsi ya kupata sukari hiyo. Na anapoonja mara moja, hawezi kujizuia bali atataka tena na tena.
Tafiti zinaonesha pia ya kwamba matumizi ya sukari yamekuwa yanabadili tabia za watu. Muda mfupi baada ya kutumia sukari watu wengi huwa wakorofi, wenye hasira na wasio na subira. Sukari inawapa nguvu za ziada ambazo zinawasukuma kuzitumia kwa njia ambazo siyo sahihi. Mtu anapokuwa na sukari nyingi kwenye mwili huwa kwenye hali ya msongo kama mtu ambaye ametumia kilevi.
Hivyo kwa uwezo wa sukari kusisimua ubongo kama madawa mengine, kitendo cha watu kuwa tegemezi kwenye sukari na kuadilika kwa tabia baada ya mtu kutumia sukari, kunaifanya sukari kuwa kwenye kundi moja na madawa ya kulevya.

Sunday, May 12, 2019

SUKARI NI SUMU KWENYE MWILI WAKO , EPUKA VYAKULA VYA SUKARI.

Kama kuna kitu kimoja ambacho kila mtu anapaswa kuambiwa na kukielewa ni kwamba matatizo yetu mengi ya kiafya yanatokana na ulaji wa sukari. Kwa kifupi sukari ni sumu kubwa sana kwenye miili yetu. Japo tunaiona tamu na tunaipenda sana, lakini hakuna kinachotuua kama sukari.
Sukari ya kawaida tunayotumia inaitwa sucrose, ndani yake ina sukari rahisi za aina mbili, glucose na fructose. Glucose ndiyo sikari inayotumika kwa urahisi na mwili na hata ubongo katika kuzalisha nguvu. Fructose huwa haitumiki sana kuzalisha nishati, badala yake inageuzwa kuwa mafuta na kuhifadhiwa kwenye mwili. Na aina hii ya sukari rahisi ndiyo inachangia sana kwenye magonjwa ya moyo na mishipa ya damu kama kukomaa na kujaa mafuta kwenye mishipa hiyo kitu kinacholeta shinikizo la juu la damu (presha).
Ubaya zaidi wa sukari uko hapa, unapokula chakula cha sukari au wanga, sukari ni rahisi kumeng’enywa, hivyo muda mfupi baada ya kutumia sukari, kiwango cha sukari kwenye damu yako kinakuwa juu sana. Hali hii inachochea mwili kuzalisha homoni inayoitwa Insulin, ambayo kazi yake ni kuondoa sukari kwenye damu na kuihifadhi kwenye seli za mwili na nyingine kugeuzwa kuwa mafuta kwenye ini. Sasa kwa kuwa sukari imepanda kwa wingi kwenye damu, insulini inayozalishwa inakuwa nyingi pia, kitu ambacho kinapelekea sukari kwenye damu kushuka haraka. Hii inaleta hali ya mtu kujisikia uchovu na kutamani kula kitu cha sukari muda mfupi baada ya kula sukari.
Kama umekuwa unakunywa chai yenye sukari asubuhi, utakuwa unaliona hili mara kwa mara, saa moja baada ya kutumia sukari unajisikia kuchoka choka na unatamani kitu chochote chenye sukari. Hapa ndipo wengi wanakunywa soda au hata kula pipi, ili mradi tu kutuliza lile hitaji la mwili la kutaka sukari ya haraka.
Ndugu  yangu, kama kuna hatua moja ambayo unapasa kuichukua, hata kama utashindwa kuchukua hatua nyingine zozote kwenye ulaji wako, basi ni kuachana kabisa na sukari. Yaani acha kabisa kutumia sukari, na utaupumzisha mwili wako na hali hii ya kutengeneza sumu ambazo zinakuchosha, kukuletea magonjwa na hata kukuzeesha haraka.
Vyakula vya sukari vya kuepuka ni kama ifuatavyo, sukari yoyote unayoongeza kwenye chai au chakula, asali, miwa na juisi yake, matunda yoyote yenye utamu wa sukari, soda, juisi za matunda hata kama ni asili, bia, mvinyo, bidhaa zozote za kiwandani ambazo zimetengenezwa kwa kuongezwa sukari, kama mikate, maandazi na chochote ambacho kimeongezwa sukari.
Nyongeza; usidanganyike na vitu vitamu ambavyo unaambiwa havina sukari, mfano soda za dayati, hizi zina kemikali ambazo ni sumu kwenye mwili wako kama ilivyo sukari. Tofauti yake na soda nyingine ni kwamba hazipandishi sukari kwenye damu, lakini bado ni sumu.
Najua hili litakuwa limekustua sana, kwa sababu vyakula vingi hapo ndiyo unatumia kila siku. Lakini kutumia kila siku au kuzoea haifanyi kuwa sahihi. Tafiti za kisayansi na za lishe zinaonesha wazi kwamba mazoea yetu kwenye ulaji ndiyo kikwazo kwetu kuwa na afya bora. Hivyo tunapaswa kujifunza na kuchukua hatua sahihi ili tuwe na afya bora na maisha bora pia.

Sunday, May 5, 2019

CHANGAMOTO TANO ZINAZOKABILI KILA AINA YA BIASHARA.

Zipo changamoto kubwa tano ambazo zinakabili kila aina ya biashara, changamoto hizi tano ndiyo zinapelekea biashara nyingi kufa na hata zinazopona kushindwa kukua zaidi.
 
(1). KUKOSA  UDHIBITI .  Huna udhibiti wa kutosha kwenye muda wako, soko na hata biashara yako. Badala ya kuiendesha biashara, biashara inakuendesha wewe.
 
(2). WATU. Unavurugwa na wafanyakazi, wateja, wabia na hata wanaokusambazia huduma mbalimbali. Watu hao hawaonekani kukuelewa na wala hawazingatii yale unayowataka wazingatie.
 
(3). FAIDA. Faida unayopata haitoshi kuendesha biashara.
 
(4). UKOMO. Ukuaji wa biashara yako umefika ukomo, kila ukikazana kuweka juhudi zaidi hakuna ukuaji unaopatikana, unajikuta unachoka zaidi lakini hakuna cha tofauti unachopata.
 
( 5 ). HAKUNA  KINACHOFANYA  KAZI. Umeshajaribu mbinu mbalimbali za kuiwezesha biashara yako kukua na watu kukuelewa, lakini hakuna hata moja ambayo imeleta matokeo mazuri. Unaelekea kukata tamaa na kuona labda biashara siyo bahati yako.
 
Changamoto hizi tano zinaikabili kila aina ya biashara, lakini habari njema ni kwamba, changamoto hizi siyo mwisho wa biashara, unaweza kuzivuka na kuiwezesha biashara yako kukua zaidi kama utazingatia nguzo sita muhimu za ukuaji wa biashara yako.

FANYA KAZI NJE YA BIASHARA YAKO.

Kama unataka kufurahia biashara yako, basi unapaswa kufanya kazi nje ya biashara na siyo ndani ya biashara. Kufanya kazi ndani ya biashara ni pale ambapo unakuwa bize na shughuli za kila siku za biashara hiyo, kuuza, kuwahudumia wateja na kuzalisha au kuandaa bidhaa na huduma unazouza. Japokuwa unaweza kuona hilo ni muhimu na hata kupenda sana kulifanya, linakuzuia kuikuza zaidi biashara yako, maana unapofanya kazi ndani ya biashara, unachoka sana na hupati nafasi ya kuona mbali zaidi ya kile unachofanyia kazi kwenye biashara hiyo.
 
Kufanya kazi nje ya biashara yako ni pale ambapo unaiangalia biashara yako kama mtu baki, kuangalia kila kitu kinavyofanyika na kuona uimara na udhaifu wako. Ni sawa na kupanda juu angani kisha kuangalia biashara yako kwa chini, na kutathmini kila kinapofanyika. Unapofanya kazi nje ya biashara, hufikirii yale majukumu ya kila siku ya biashara, bali unaangalia kule ambako biashara inakwenda na uwezo wa kufika huko.
 
Kama unataka biashara yako ikue, lazima uweze kufanya kazi nje ya biashara yako, uweze kuiangalia biashara kama mtu wa pembeni na kupata picha ya pale ilipo sasa na inapoweza kufika.
 

WEWE NA BIASHARA YAKO NI VITU VIWILI TOFAUTI

Hiki ni kitu ambacho kila mfanyabiashara anapaswa kuambiwa, tena kupigiwa kelele kila mara mpaka aelewe. Kwa sababu kama wafanyabiashara wakielewa hili, nusu ya matatizo ya biashara yatatoweka yenyewe.
 
Sehemu kubwa ya matatizo ya biashara yanasababishwa na mfanyabiashara kufikiri yeye ni biashara yake, kitu ambacho siyo kabisa.
 
Biashara nyingi hazikui kwa sababu hakuna mpaka baina ya biashara na mmiliki wa biashara. Mtu anaweza kutoa fedha kiholela kwenye biashara kwa sababu anaona biashara ni yake. Kitu ambacho kinakuwa na athari kubwa sana kwenye ukuaji wa biashara hiyo.
 
Ndugu , naomba nikusisitizie hili, na liandike mahali ambapo utaweza kulisoma kila siku; WEWE SIYO BIASHARA YAKO, wewe na biashara yako ni vitu viwili tofauti kabisa.
 
Wewe una maisha yako, ndoto zako na mahusiano yako, biashara ina maisha yake, ndoto zake na mahusiano yake. Kinachowaunganisha wewe na biashara yako ni mtaji ambao umeuweka kwenye biashara hiyo, mtaji huo umeikopesha biashara, na njia pekee ya kunufaika kupitia biashara hiyo ni pale inaopata faida baada ya kufanyika kwa biashara.
 
Ukiweza kuelewa hili, kwamba wewe siyo biashara yako, ukaiheshimu biashara yako na kuiacha ikue bila ya kuiingilia, ukaiendesha kwa misingi ya ukuaji wa biashara, utaiwezesha biashara hiyo kukua zaidi.

FURSA 20 ZA KUFANYA KIPINDI CHA MVUA----Maisha Na Mafanikio Blog ( Life & You )

Saturday, May 4, 2019

FURSA ZA KUFANYA UKIWA NYUMBANI KWAKO ( A ) / BIASHARA ZA KUFANYA NYUMBANI-------Maisha Na Mafanikio Blog ( Life & You )

KILA BIASHARA INA CHANGAMOTO ZAKE . USIPUUZE AU KUKWEPA IKABILI KILA CHANGAMOTO INAPOJITOKEZA.

Ni changamoto zipi unazokutana nazo na unazoweza kukutana nazo mbeleni?
Kila biashara ina changamoto zake, hakuna biashara isiyokuwa na changamoto kabisa. Lakini watu wengi huwa hawapendi kukutana na changamoto, na hivyo huwa hawapo tayari kuzikabili.
Wanachofanya wafanyabiashara wengi pale wanapokutana na changamoto ni kuzipuuza au kuziacha wakiamini zitaondoka zenyewe. Changamoto hizo huwa haziondoki, badala yake zinakua na kuota mizizi, na hizo ndiyo huja kuua biashara.
Unapaswa kujua zipi changamoto kubwa zinazoikabili biashara yako sasa na hata siku za mbeleni. Kisha kuwa na mkakati sahihi wa kukabiliana na kila changamoto pale inapojitokeza. Usijaribu kupuuza au kukwepa changamoto, badala yake ikabili kila changamoto inapojitokeza, na siyo tu utaitatua, bali pia utapiga hatua zaidi kwenye biashara yako.

KUWA NA MKAKATI WA MASOKO YA BIASHARA YAKO.

Upi mkakati wa masoko unaofanyia kazi wa  biashara     yako ?
Biashara ni wateja, bila ya wateja, haijalishi una bidhaa au huduma bora kiasi gani, huna biashara. Na njia pekee ya kuwaleta wateja kwenye biashara hiyo ni mkakati wa masoko.
Wafanyabiashara wengi wadogo huwa hawajisumbui kabisa na masoko. Huwa wanaendesha biashara zao kwa mtazamo wa kizamani kwamba ukijenga biashara wateja watakuja wenyewe. Lakini zama hizi ambazo wafanyabiashara ni wengi, hakuna mteja atakayekuja kwako, bali unapaswa kuwatafuta wateja.
Unawatafuta wateja kupitia mpango mkakati wa masoko unaokuwa nao kwenye biashara yako.
Hii ni kusema kwamba ili biashara yako ifanikiwe, lazima iwe na mkakati wa masoko, ambao unawatambua wateja wa biashara hiyo, kuwafikia kule waliko na kuwashawishi kununua.
Mkakati wako wa masoko unapaswa kuzingatia vitu vinne muhimu sana;
  1. Kuwatabua wateja sahihi wa biashara yako, wale ambao wanaweza kunufaika na bidhaa au huduma unazotoa.
  2. Kutambua vitu vitatu vinavyokutofautisha wewe na wafanyabiashara wengine wanaofanya biashara kama yako. Kama huna utofauti wowote na wafanyabiashara wengine, hakuna sababu ya mteja kuja kwako.
  3. Mchakato sahihi wa ufanyaji wako wa biashara, jinsi mteja anavyohudumiwa na hatua zote zinazochukuliwa kwenye biashara yako.
  4. Uhakika unaowapa wateja wako. Wateja wamepata fedha zao kwa shida, hawataki kuzipoteza, hivyo wanahofia sana kufanya manunuzi mapya. Unapaswa kuwapa uhakika kwamba wakinunua kwako hawapotezi fedha bali wanapata thamani.
Tengeneza mkakati wako wa masoko ambao unajumuisha vitu hivyo vinne na utaweza kuwafikia wateja wengi na kuwashawishi kununua kwako.

WEKA MALENGO YA MUDA MREFU ( MIAKA MITANO , KUMI ........... !! ) YA BIASHARA YAKO.

Ni lengo lipi kubwa unataka kufikia ndani ya miaka MITANO ,  KUMI ?  YA  BIASHARA   YAKO ?

Kabla sijaendelea hapa, hebu tafakari hilo swali na jipe majibu sahihi. Ni lengo lipi kubwa unalofanyia kazi ambalo unataka kulifikia miaka MITANO , KUMI  ijayo? Watu wengi wanaweza kushangaa unapangaje miaka kumi ijayo, wengi kupanga mwaka mmoja tu ni shida.

Huwezi kufanikiwa kwenye biashara kama huna malengo ya muda mrefu. Na hata kinachofanya wafanyabiashara wengi kukimbizana na fursa mpya zinazojitokeza ni kwa sababu hawana malengo yoyote ya muda mrefu, hivyo chochote kinachojitokeza wanaona ni sahihi kwao kukimbizana nacho.

Unapaswa kuwa na lengo kuu la miaka MITANO , KUMI  ijayo ya biashara yako, wapi unataka kufika na kwa kiwango gani. Lengo hili ndiyo litakusukuma kila siku, ndiyo litakuwa mwongozo wako na ndiyo litaathiri kila maamuzi unayofanya.

Kama huna lengo la miaka MITANO , KUMI  ijayo ya biashara yako, hujajitoa kufanikiwa kweli kwenye biashara hiyo. UNATANIA  NDUGU !  BADILIKA !  NA  AMKA !

WEKA KIPAUMBELE KIKUU CHA BIASHARA YAKO .

JIULIZE  Kipi kipaumbele kikuu cha biashara Yangu ?

Hakuna kitu kinachowapoteza wafanyabiashara wengi kama fursa mpya na nzuri zinazojitokeza kila wakati. Iwapo mfanyabiashara atakuwa mtu wa kukimbizana na kila fursa inayojitokeza, hawezi kufanikiwa kabisa kwenye biashara.

Hii ni kwa sababu fursa mpya huwa ni nyingi na haziishi, na ili upate mafanikio kwenye jambo lolote, unahitaji kuweka muda na kazi.

Jukumu lako kama mfanyabiashara ni kuweka kipaumbele kikuu cha biashara yako, yaani ni aina gani ya biashara utafanya na kisha kuachana na kelele nyingine zozote.

Ukishachagua biashara utakayofanya, funga masikio kuhusu biashara nyingine zisizoendana na biashara hiyo. Hata uambiwe kuna biashara mpya na yenye faida kubwa, usidanganyike kuondoka wenye vipaumbele vyako na kwenda kwenye biashara hiyo mpya, utajipoteza mwenyewe.

Ukichagua nini unataka na kuweka nguvu zako zote kwenye kitu hicho, lazima utakifikia. Lakini ukigawa nguvu zako kwenye kila kitu kipya kinachojitokeza, unajizuia mwenyewe kufanikiwa.

Kama biashara uliyoanzisha imekuwa na unaona fursa ya kuingia kwenye biashara nyingine, fanya hivyo kwa mipango na maono yako na siyo kwa kusukumwa na tamaa zako na za wengine.

JENGA MISINGI MIKUU YA BIASHARA YAKO.

JIULIZE   SWALI  HILI  WEWE  MFANYABIAHARA . Ipi ni misingi mikuu ambayo inaendesha biashara yako?
Kama unataka kujenga nyumba basi msingi ni sehemu ya kuweka umakini mkubwa. Kadhalika kwenye biashara, unapaswa kujenga msingi imara kama unataka biashara yako ifanikiwe.
Hatua ya kwanza kwenye maono ya biashara ni kuainisha misingi mikuu ambayo inaendesha biashara hiyo. Hizi ni kanuni na maadili ambayo kila anayekuwa kwenye biashara hiyo anapaswa kufuata, ukianza na wewe mmiliki wa biashara.
Misingi hii ni muhimu kwa sababu inaongoza jinsi maamuzi yanavyofanywa kwenye biashara. Pia inawavutia watu sahihi na kuwaondoa wale wasio sahihi.
Unapaswa kuwa na misingi imara ya maadili ya kuendesha biashara yako, ambapo maamuzi yote yataongozwa kwa misingi hiyo. Pia utaajiri, kutunza na hata kufukuza wafanyakazi kwa kutumia misingi hiyo.

Wednesday, May 1, 2019

FURSA 8 KWA WAAJIRIWA----Maisha Na Mafanikio Blog ( Life & You )

FURAHA HAIPATIKANI KWENYE MATOKEO , BALI IPO KWENYE MCHAKATO.

Kama unaitafuta furaha kwenye maisha, tayari umeshapotea, kwa sababu unatafuta kitu ambacho hakipatikani. Furaha haipo mwisho wa safari, bali ipo kwenye safari yenyewe. Furaha haipatikani mwishoni, bali katika ufanyaji wenyewe.
 
Ndiyo maana nakuambia furaha ndiyo njia yenyewe, hakuna njia ya kukupeleka kwenye furaha.
 
Mtu anajiambia nikipata kazi nitakuwa na furaha, anaipata na haioni furaha, anajiambia nikipanda cheo nitapata furaha, anapanda cheo hapati furaha, anajiambia tena nikiwa bosi nitakuwa na furaha, anakuwa bosi na haioni furaha. Mtu huyu haoni furaha kwa sababu anaangalia sehemu ambayo siyo sahihi. Furaha haipo kwenye matokeo bali ipo kwenye mchakato. Hivyo kama mtu huyo anataka furaha, basi inapaswa kutoka kwenye kazi zake za kila siku, na siyo matokeo ya mwisho ya kazi zake.

JINSI YA KUOKOA MUDA UNAOPOTEZA KILA SIKU NA OKOA MASAA MAWILI YA ZIADA KILA SIKU.

Kila mtu ana masaa 24 kwa siku ila kuna wanaofanikiwa sana na kuna ambao wanaishia kulalamika kwamba hawana muda. Kama una jambo ambalo ni muhimu kwako lazima utapata muda wa kulifanya. Tumia njia hizi hapa chini kuokoa muda unaopoteza kila siku na uanze kuwekeza kwenye maisha yako.

  Hebu fikiria unaambiwa ujisomee kila siku, ufanye mazoezi, ufanye  meditation, utenge muda wa kuweka mipango yako kwa siku, upate muda wa kupitia mipango yako, upate muda wa kupumzika na pia upate muda kwa ajili ya wale unaowapenda na wanaokupenda. Kwa mambo hayo tu tayari siku imeisha na bado hujaweka muda wa kufanya kazi na muda wa kulala.
 
  Kwa muda mfupi tulio nao ni vigumu sana kufanya mambo yote hayo kila siku. Unaweza kujiaminisha hivyo ila ni uongo mkubwa sana ambao umekuwa unajidanganya kila siku.
  Ili uache visingizio visivyo na maana leo ninakupa njia ya kupata masaa mawili ya ziada kila siku ambapo unaweza kufanya mambo hayo ambayo yatabadili maisha yako na kuwa bora zaidi.

  Kwanza hebu tuangalie muda wetu kwa siku. Kila binadamu ana masaa 24 kwenye siku moja. Wapo wengi ambao wameyagawa masaa yao kwa masaa nane ya kulala, nane ya kazi na nane ya kupumzika. Kwa vyovyote ulivyoyagawa wewe haijalishi, ila unaweza kuokoa masaa mawili ili kufanya mambo yako.

  Ili kupata masaa mawili ya ziada kila siku fanya mambo yafuatayo;
1. Amka nusu saa kabla ya muda uliozoea kuamka kila siku. Utumie muda huo kufanya jambo lenye manufaa kwenye maisha yako kama kujisomea au kuweka MALENGO   NA  MIPANGO. Na ili uweze kuamka nusu saa kabla ni vyema ulale mapema na ulale usingizi mzuri.

2. Punguza nusu ya muda unaotumia kusikiliza redio, kuangalia tv na kuangalia filamu. Asilimia 80 ya vipindi unavyofuatilia kwenye tv au redio havina msaada wowote kwenye malengo yako ya maisha. Asilimia kubwa ya taarifa zinazokushtua kila siku sio za kweli au zimeongezwa chumvi mno. Hivyo punguza muda huu unaotumia kwenye vyombo vya habari na uutumie kubadili maisha yako.

3. Punguza muda unaotumia kwenye mitandao ya kijamii hasa facebook na twitter. Mitandao hii ina ulevi fulani, unaweza kusema unaingia kuchungulia ujue ni nini kinaendelea ila ukajikuta saa nzima unashusha tu kuangalia zaidi. Na asilimia 90 ya unayofuatilia kwenye mitandao hii hayana msaada kwenye maisha yako. Tenga muda maalumu kwa siku wa kutembelea mitandao hii ili kujua nini kinaendelea.

4. Zima simu yako au iweke kwenye hali ya kimya kabisa(wala isitetemeshe). Hapa najua utanipinga sana na unaweza kudhani nimechanganyikiwa. Tumehamishia fikra zetu kwenye mawasiliano hasa ya simu. Mtu unakaa na simu ikiita kidogo tu unakimbilia kujibu bila ya kujali ni kitu gani cha muhimu unafanya. Inaingia meseji ambayo haina hata maana ila inakuhamisha kutoka kwenye jambo la muhimu unalofanya. Najua una madili mengi yanayokuhitaji kupatikana kwenye simu ila kuiweka simu yako mahali ambapo huwezi kuiona kwa masaa mawili kwa siku haiwezi kukupotezea dili lolote. Muda ambao unafanya kazi inayokuhitaji ufikiri sana na uwe na utulivu hakikisha simu yako haiwezi kukuondoa kwenye kazi hiyo. Hivyo izime au iwe kimya kabisa na iwe mbali.

USISUBIRI KUSTAAFU, NDIO UFANYE UJASIRIAMALI USIJE UKAFA MAPEMA.

Wengi wameingia kwenye mtego huo, kazi wanaifanya kweli, na wanafikia umri wa kustaafu, wanastaafu, mafao wanayapata, lakini maisha hayawi mazuri bali yanakuwa yamejaa msongo. Na wengi, hawavuki miaka mitano, wanafariki ndani ya miaka mitano baada ya kustaafu.
 
Hivyo kama hutaki kufa mapema, basi usikubali kustaafu. Kila siku ya maisha yako ifanye kuwa siku ya kazi, na kadiri mwili unavyokuwa kwenye kazi, unakuwa imara zaidi ya mwili uliopumzika.
 
Hivyo chagua kufanya kazi au biashara ambayo utaendelea kuifanya hata ukiwa na miaka 80, 90 na hata 100. Chagua kufanya kazi mpaka siku unayokufa, na utakuwa na maisha marefu, na yaliyo bora zaidi.
 
Kama umeajiriwa na ukifika miaka 60 au 65 ni lazima ustaafu, hakikisha unatengeneza mazingira ya kukuwezesha kuwa na kazi ya kuendelea kufanya hata baada ya kustaafu kwenye ajira. Na hapo siyo ukatafute tena ajira za muda, badala yake uwe umeshajenga kitu chako ambacho utakifanyia kazi kwa miaka yako yote.