Saturday, May 4, 2019

WEKA KIPAUMBELE KIKUU CHA BIASHARA YAKO .

JIULIZE  Kipi kipaumbele kikuu cha biashara Yangu ?

Hakuna kitu kinachowapoteza wafanyabiashara wengi kama fursa mpya na nzuri zinazojitokeza kila wakati. Iwapo mfanyabiashara atakuwa mtu wa kukimbizana na kila fursa inayojitokeza, hawezi kufanikiwa kabisa kwenye biashara.

Hii ni kwa sababu fursa mpya huwa ni nyingi na haziishi, na ili upate mafanikio kwenye jambo lolote, unahitaji kuweka muda na kazi.

Jukumu lako kama mfanyabiashara ni kuweka kipaumbele kikuu cha biashara yako, yaani ni aina gani ya biashara utafanya na kisha kuachana na kelele nyingine zozote.

Ukishachagua biashara utakayofanya, funga masikio kuhusu biashara nyingine zisizoendana na biashara hiyo. Hata uambiwe kuna biashara mpya na yenye faida kubwa, usidanganyike kuondoka wenye vipaumbele vyako na kwenda kwenye biashara hiyo mpya, utajipoteza mwenyewe.

Ukichagua nini unataka na kuweka nguvu zako zote kwenye kitu hicho, lazima utakifikia. Lakini ukigawa nguvu zako kwenye kila kitu kipya kinachojitokeza, unajizuia mwenyewe kufanikiwa.

Kama biashara uliyoanzisha imekuwa na unaona fursa ya kuingia kwenye biashara nyingine, fanya hivyo kwa mipango na maono yako na siyo kwa kusukumwa na tamaa zako na za wengine.

No comments:

Post a Comment