Friday, May 24, 2019

UNAPOSHIKWA NA HASIRA , JIPE MUDA WA KUTAFAKARI.

 Ukishagundua kwamba upo kwenye hasira, basi kaa kimya, jipe muda wakutafakari na kutulia na utajiepusha na makosa makubwa unayoweza kufanya ukiwa na hasira.
 
Hasira ni moja ya hisia zenye nguvu sana, na hisia zinapokuwa juu uwezo wetu wa kufikiri unakuwa chini. Hivyo unapokuwa na hasira, unakuwa umetawaliwa na hisia na siyo fikra. Na ni wakati mbaya sana wa kufanya chochote, kwa sababu unaposukumwa na hisia, hujui kipi sahihi kufanya, kwa kuwa hufikiri sawasawa.
 
Hivyo rafiki, unapogundua kwamba una hasira, usifanye chochote.
 
Kama kuna mtu amekukosea na umepatwa na hasira usimjibu wakati una hasira hizo.
 
Kama kuna mtoto wake amekosea usimwadhibu ukiwa na hasira.
 
Ukiwa na hasira usifanye chochote, jipe muda wa kukaa mbali na kile kinachokupa hasira na akili zako zitarudi.

No comments:

Post a Comment