Friday, November 30, 2018

SAFARI YA MAFANIKIO INAANZA NA WATU WENGI SANA. WENGI HUISHIA NJIANI, KWANINI ??


Watu wengi wanakata tamaa kwenye safari ya mafanikio kwa sababu ya kutokujua kwamba mafanikioo yanataka muda mrefu. Katika kipindi cha kutafuta mafanikio yako unatakiwa ujitoe hasa, kuvumilia na kutoa kila ulichonacho hadi ufanikiwe.
Kwa mfano, ilichukua muda wa miaka 11 hadi program ya ‘Microsoft’ ya bilionea mkubwa duniani kuanza kufanya kazi na kuleta mafanikio makubwa. Mafanikio yake hayakutokea tu ghafla kuna miaka ilikataika hapa katikati.
Pia ilimchukua miaka 29 kwa Abraham Lincoln hadi kuweza kuwa Rais wa marekani. Ipo mifano mingi inayoonyesha kwamba mafanikio si kitu cha mara moja tu, unatakiwa kuwekeza muda ili uweze kufanikiwa kwenye mafanikio hayo uyatakayo.
Kwenye akili yako sasa weka wazi, mafanikio ni safari ya muda mrefu. Unatakiwa kabisa utenge miaka angalau kuanzia 5 hadi 15 ya kutafafuta mafanikio yako ya kweli na ya kudumu. Ukikurupuka na kutaka mafanikio ya chapu chapu utakwama.
Kama utakuwa ni mtu wa kutaka mafanikio na halafu ukategemea mafanikio hayo yakatokea ghafla ghafla kwa muda mchache ni rahisi sana kwako kuweza kukata tamaa na kuona ni kitu ambacho hakiwezekani au mafanikio ni ya watu wa aina fulani tu lakini si wewe.

JIWEKEE MUDA WA UKOMO KWA CHOCHOTE UNACHOPANGA KUFANYA.

Mtu mmoja amewahi kusema kwamba jukumu huwa linachukua muda uliopangwa lifanyike. Akimaanisha kama kuna jukumu ambalo linapaswa kufanywa kwa masaa mawili, litakamilika ndani ya masaa mawili. Jukumu hilo hilo likipangwa kufanyika ndani ya masaa matano, litachukua masaa matano.
Huwa tunasukumwa kufanya zaidi pale ambapo muda unakuwa mdogo, na tunaahirisha mambo pale muda unapokuwa mwingi. Ndivyo maana wanafunzi ni vigumu sana kusoma siku za kawaida, lakini mtihani unapokaribia, hamasa ya kusoma inakuwa juu.
Jiwekee muda wa ukomo kwa chochote unachopanga kufanya, na muda huo uwe mfupi kuliko muda uliozoeleka. Kwa kuwa na muda huu na kuufuata, utaweza kujisukuma kufanya zaidi. Kadiri unavyokuwa na muda mfupi wa kutekeleza jambo, ndivyo mawazo ya kuahirisha yanavyopotea kwenye akili yako. Waahidi watu kwamba jukumu litakamilika mapema kuliko kawaida, na tekeleza hilo uliloahidi.

KUWA NA MAMBO YAKO MATANO KWA SIKU AMBAYO UTAYATEKELEZA.

Kila siku unayoianza, ainisha mambo matano muhimu ambayo ukiyafanya siku hiyo yatakusogeza karibu na mafanikio unayotaka kuyafikia. Mambo hayo matano unapaswa kuyafanyia kazi bila ya kujali mazingira yapoje. Inyeshe mvua au liwake jua, hayo matano ni muhimu kwa siku yako na unapaswa kuyafanyia kazi.
Kwa kuwa na tano za siku, unajiweka kwenye nafasi ya kutekeleza yale muhimu na kuepuka kupotezwa na kelele ambazo zimekuzunguka kila mahali.

TUMEZOEA KUSIMAMIWA : KUWA NA MTU WA KUKUSIMAMIA.

Sisi binadamu ni wabaya sana kwenye kujisimamia wenyewe, huwa tunajionea sana huruma na ni rahisi sana kujidanganya. Unaweza kuwa na orodha yako ya siku, umepanga mambo yako matano muhimu na hata kujiwekea ukomo. Lakini katikati ya siku yako ukawa hujisikii kuendelea na yale uliyopanga, ni rahisi kujihalalishia kwamba labda umechoka au ni kitu hakiwezekani.
Lakini unapokuwa na mtu wa pembeni, mtu ambaye jukumu lake ni kuhakikisha umekamilisha uliyopanga na hapokei sababu bali matokeo, utalazimika kufanya kile ulichopanga kufanya.
Tafuta mtu wa karibu kwako, ambaye hakuonei huruma kisha mtake akusimamie kwa karibu ili utimize unachotaka. Kama huwezi kupata mtu wa karibu basi kuwa na kocha au menta ambaye atakusimamia kwa karibu.

JIAMBIE HIVI " NAFANYA SASA , MUDA HUU ".

Kuna wakati unakuwa umeshapanga kabisa nini utafanya na kwa wakati gani. Lakini inapofika muda wa kufanya, mawazo ya kuahirisha yanaanza kukuingia. Unaanza kuona labda hujawa tayari au ni bora kusubiri.
Ni katika wakati kama  huu ndiyo unapaswa kujiambia kauli hii, NAFANYA SASA HIVI, rudia kauli hiyo mara nyingi uwezavyo na utajikuta umeanza kufanya. Kila unapofikiria kuahirisha kufanya kitu, jiambie kauli hiyo kwamba unafanya. Kila unapoanza kujiambia kwambe umechoka, anza kujiambia kauli hiyo.
Kwa kurudia rudia kujiambia kauli hiyo, unaanza kuiamini na kujiamini wewe mwenyewe na kuanza kufanya.

TUNA MIPANGO MINGI SANA NA MIZURI, TATIZO NI UTEKELEZAJI WAKE ???

Mipango ni rahisi sana, kila mtu anapanga na msimamishe mtu yeyote njiani na muulize mipango yake ni ipi, atakupa mipango mizuri sana.

Pamoja na kila mtu kuwa na mipango mizuri, ni wachache sana ambao wanaweza kufanyia kazi mipango hiyo na ikawa uhalisia kwenye maisha yao. Wengi wamekuwa wanabaki na mipango tu, lakini haiwi uhalisia.

Kinachowazuia wengi kutekeleza mipango waliyonayo ni tabia ya kuahirisha mambo. Hii ni tabia ambayo ni asili yetu sisi binadamu, huwa hatupendi kufanya chochote ambacho kinatuumiza au kinataka tuweke kazi.

Huwa tunapenda kutumia muda wetu kwa vitu visivyo na maana. Kwa muda ule ule na kwa nguvu zile zile, huwa tunaona ni bora kutumia kufanya vitu ambavyo vitatupa raha ya muda mfupi, kuliko kufanya vitu ambavyo havina raha ya muda mfupi lakini kwa muda mrefu vina maana.

Kinachowatofautisha wale wanaopata mafanikio makubwa kwenye maisha yao na wale wanaoshindwa siyo bahati wala akili wala fursa. Kinachowatofautisha ni namba wanavyoweza kuishinda tabia ya kuahirisha mambo. 

Wanaofanikiwa na wanaoshindwa wote wanakuwa kwenye mazingira sana, wanakutana na fursa sawa, lakini wale wanaoshindwa huwa wanasubiri wakati wanaofanikiwa wanachukua hatua.

FANYA BIASHARA HIZI UTAPIGA PESA SANA. UTAFANIKIWA SANA.

1. USAFIRI.
Moja ya biashara ambayo inaaminika hasa kwa bara la afrika ikiwa utaifanya kwa utulivu na ukafata misingi yake ni biashara ya usafiri. Hapa unaweza ukawa na kampuni yako ya kusafirishia abiria kutoka sehemu moja na kwenda nyingine.
Kwa sasa hitaji la usafiri bado ni kubwa, kama si mjini hata kijijini. Watu wanataka kusafiri kila siku na kwa bahati mbaya wengi hawana uwezo huo wa kumiliki vyombo vya usafiri. Hii ni mojawapo ya biashara ya kuifikiria kuifanya kama unaweza, kwani itakupa mafanikio sana.

2. AFYA.
Kama pia utajikita na kufanya biashara inayohususha mambo ya afya, basi upo uwezekano mkubwa zaidi wa wewe kufanikiwa sana. Huduma za afya katika maeneo mengi bado hazijafikiwa kisawasawa na zinahitajika kweli.
Hivyo kwa kufanya biashara hii, kama ukifungua hospitali au zahati au duka la dawa, utapata pesa na hapo pia utakuwa imeisaidia jamii. Kikubwa kubali kuzunguka kuangalia ni wapi ambapo ukifanya huduma au biashara hii wewe itakulipa.

3. CHAKULA.
Hakuna mtu asiyekula, hiyo ikiwa na maana ukianzisha biashara ya vyakula na ukaifanya kwa ufanisi mkubwa utafanikiwa. Hapa unaweza ukauza chakula, lakini si maanishi uje na picha ile ya mama ntilie ‘pasee.’
Ukiamua kuja na biashara ya kuuza chakula ifanye kwa ukisasa zaidi. Zipo sehemu bado nyingi zinazohitaji huduma hii ya chakula safi, mazingira safi, lakini hawaipati kwa uhakika kwahiyo unatakiwa ujue jinsi ya kuanza ili uanze kupiga pesa.

4. VIWANDA  VIDOGO  VIDOGO. 
Huwezi  kuendelelea sana kama utaendelea kuwa mlanguzi wa biashara za watu wengine. Changamsha akili na anza mchakato wa kuweka viwanda vidogo vidogo ambavyo vitasaidia wewe kuweza kukupa kipato kikubwa.
Uzuri wakuwa na kiwanda kidogo wewe ndio unakuwa mzalishaji wa kwanza kwa hiyo ni lazima utapata faida kubwa sana. Hapa unaweza ukatengeneza kiwanda chako cha kutengeneza juisi au unga wa sembe na lishe, uamuzi ni wako.

Thursday, November 22, 2018

KILA MTU NA HAMSINI ZAKE. HAKUNA ANAYEJALI SANA MAISHA YA WENGINE.

Maisha ya sasa hivi naweza kusema yamekuwa ni kama ya kuishi kisiwani, watu wamekuwa hawajali sana watu wengine kwa kiasi kikubwa, ukilinganisha na zamani. Kwa sasa ukipata changamoto kubwa wewe jua hiyo ni changamoto yako tu, inabidi ukomae nayo hadi utoke.
Kutokana na hili kuendelea kudumu kunafanya maisha yanazidi kuendelea kuwa magumu sana hadi watu wanakosa msaada ambao ungeweza kuwasaidia. Ubinafsi ambao wengi wanao imekuwa ni kichocheo kikubwa sana cha ugumu wa maisha.

KUTEGEMEA CHANZO KIMOJA CHA MAPATO , HUPELEKEA MAISHA KUWA MAGUMU SANA !

Kutokana na maisha kubadilika na gharama za maisha kupanda karibu kila siku, suala la kutegemea kipato kimoja, ni moja ya chanzo cha maisha kuwa magumu. Watu wengi wanategemea kipato kimoja, zaidi kwa wengi ikiwa ni ajira.
Kwa bahati mbaya kipato kimoja hakiwezi kukidhi mahitaji yote hata iweje. Sasa kwa sababu hiyo ya maisha kupanda mara kwa mara, ni lazima tu ugumu wa maisha uonekane. Hata siku moja usitegemee maisha yako yakawa rahisi kama bado una kipato kimoja.

Saturday, November 17, 2018

TABIA YA FEDHA. FEDHA NI ZAO LA HAMASA.

 FEDHA  ni kama mchumba mwenye wivu, mchumba ambaye anataka muda wote uwe naye, muda wote umfikirie yeye tu. Na mchumba huyu akigundua humfikirii na kumjali yeye anaondoka na kwenda kutafuta wengine wanaomjali na kumfikiria.
Hivi ndivyo fedha zilivyo, kama huna muda nazo hazitakuwa na muda na wewe. kama huzijali na kuzifikiria muda wote zitaenda kwa wale wanaojali na kuzifikiria.

Fedha ni zao la hamasa, chochote ambacho kinakuhamasisha, kile unachopenda kweli, kila ambacho unakifanya muda wote bila ya kuchoka, ndiyo kitu kitakachokuletea kipato kikubwa sana.
Hivyo rafiki, unapofikiria kuhusu fedha, anza kufikiria nini kinakupa hamasa sana, nini unapenda kufanya sasa kisha weka maisha yako yote kwenye kufanya hicho, na fedha hazitakuwa tatizo kubwa kwako.

Tatizo kubwa kwenye hili ni watu huwa wanakosa uvumilivu, wakiona kile wanachofanya kinachelewa kuwaletea matokeo wanayopata, na kuona wengine wakifurahia matunda ya vile wanavyofanya, wanajidanganya kule ndiyo kwenye fedha, wanaacha wanachofanya na kwenda kufanya vitu vingine. Wanahangaika sana, na hawapati fedha walizofikiria kupata. Na hata wakizipata, bado maisha yao yanakuwa na utupu fulani, kwa sababu kile wanachofanya siyo kinachowahamasisha zaidi.

Friday, November 16, 2018

HUDHURIA SEMINA AU WARSHA MBALIMBALI ZA KIBIASHARA UJIFUNZE MBINU MPYA ZA KIMAUZO. DUNIA INABADILIKA KILA SIKU. ACHANA NA MBINU ZA KIZAMANI ZA KIMAUZO.

Inapotokea mbinu zako za kimauzo zimepitwa na wakati huwezi kuendelea kuwapata wateja wengi. Hapa ndipo maana kampuni kubwa zikaja na kitengo cha huduma kwa wateja ili kila siku kuweza kumudu kuboresha huduma ili kuleta mafanikio. Kama kila wakati utaendelea kuwa na mbinu zile zile za kimauzo pasipo kuzibadilisha na kutegemea muujiza utakaokupa wateja wengi, naomba nikwambie kwenye hilo jambo lisahau kabisa. Ni muhimu ukabadilika kwanza wewe na wasaidizi wako.

NINI UFANYE ???
Kila mara pata mafunzo ya jinsi ya kuboresha huduma kwa wateja na unaweza kuyapata kupitia semina au warsha mbalimbali za kibiashara. Pia jenga urafiki na wateja ili wakusaidie kupata wateja wengine zaidi na zaidi ili kufikia mafanikio.

Ndimi  Mwl  Japhet  Masatu, Dar  es  salaam , Tanzania, Afrika  Ya  Mashariki.

EMAIL: japhetmasatu@gmail.com 

Call: + 255 716 924136 ( WhatsApp ) , + 255 755 400128

HUDUMA MBOVU, HUPOTEZA SANA WATEJA.

Huwezi kukwepa kukosa wateja kama una huduma mbovu kwa wateja wako. Unaweza usiwe wewe, hapa wanaweza wakawa ni wasaidizi au wafanyakazi wako  ndio wanaokuharibia pasipo wewe kujua kitu chochote na ukaona uko sawa.
Wengi kwa kushindwa kujua kwamba wanahuduma mbovu ndio wanajikuta ni chanzo cha kuanza kupoteza wateja wengi tena bila kujua. Huduma yako mbovu inaweza ikawa kwenye bidhaa au mazingira au  hata jinsi ya kuwahudumia wateja na wakaridhika.

NINI  UFANYE ?
Hapa kuwa makini sana na mazingira yote yanayoweza kupelekea huduma mbovu ikatolewa, kama wafanyakzi wako, mazingira na bidhaa unazozitoa. Vitu hivyo unatakiwa kuvihakiki mara kwa mara ili visiwe chanzo cha huduma ya hovyo kwako na kupelekea kukosa wateja. 

Na  Mwl  Japhet  Masatu , Dar  es  salaam , Tanzania, Afrika  Ya  Mashariki

+255 716 924136 ( WhatsApp ) , +255 755 400128 
EMAIL: japhetmasatu@gmail.com

Wednesday, November 14, 2018

KATIKA MAISHA USIBWETEKE NA YALE ULIYOKAMILISHA TUU !!!

Katika MAISHA watu hufurahia zaidi yale waliyokamilisha pekee huku wakiyasahau kabisa yale ambayo hawajayafanya au kuyakamilisha.
 
Pia kitendo cha kuyafurahia yale ambayo umeyafanya na kujiona wewe ni bora zaidi hukufanya uzidi kubweteka na kuachana na yale unayoyakosea katika maisha.

 Hivyo NDUGU yangu MDAU  wangu  katika maisha haya unatakiwa kukumbuka ya kwamba yale uliyoyapanga na kuyakamilisha ni jambo jema sana, ila kama unataka kuwa bora zaidi ya hapo ulipo sasa unatakiwa kushughulika na yale machache yalikuwa ni vikwazo ambayo yamekufanya ushindwe kufanya vizuri zaidi.

Asante sana   kwa   kusoma , Ndimi  MWL   JAPHET  MASATU , DAR  ES  SALAAM, TANZANIA,  AFRIKA  YA  MASHARIKI.

Friday, November 2, 2018

TENGENEZA UHURU KAMILI KWENYE MAISHA YAKO UTAPATA FURAHA YA KWELI

Wapo watu ambao wameajiriwa na wanalipwa mshahara mkubwa sana, kipato chao kinawawezesha kupata chochote wanachotaka, kwa upande wa kipato, lakini bado wanakosa furaha kwenye maisha yao. Na sababu kubwa ni kukosa uhuru wa maisha yao. Kwa sababu kadiri mtu anavyolipwa, ndivyo anavyotumika zaidi. Kadiri kipato cha ajira kinavyokuwa kikubwa, ndivyo majukumu yanakuwa mengi na kutegemewa kuwa tayari na kazi wakati wowote. Mtu hawezi kuchagua afanye nini na maisha yake, ni mpaka aombe ruhusa kwanza.

Uhuru ni kiungo muhimu sana cha furaha, huwezi kuwa na furaha kama huna uhuru.
Na uhuru siyo kwenye eneo la fedha na kazi pekee, bali hata kwenye fikra za wengine. Kama una chuki na wengine haupo huru, hivyo huwezi kuwa na furaha. Kama unashindana na wengine huwezi kuwa huru, kwa sababu muda wote utakuwa unawaangalia wanafanya nini.
Ili kuwa na furaha ya kudumu kwenye maisha yako, lazima uwe na uhuru na maisha yako. Kadiri unavyokuwa huru, ndivyo unavyokuwa na furaha.

UFUNGUO  WA  FURAHA:Tengeneza uhuru kamili kwenye maisha yako, ondoa utegemezi wako kwa wengine au vitu fulani ndiyo maisha yako yakamilike. Hata kama huna kila unachotaka, kitendo cha kuwa huru na muda wako na maisha yako, kinakuwezesha kuwa na furaha ya kudumu kwenye maisha yako.

JENGA MAHUSIANO CHANYA UTAPATA FURAHA YA KWELI KATIKA MAISHA YAKO

Mahusiano yetu na wengine yana mchango mkubwa sana wa namna maisha yetu yanavyokuwa. Kama utakuwa na mahusiano chanya, mahusiano ya kuelewana na wale watu unaojihusisha nao, mahusiano ya kujaliana, mahusiano ya kuwa tayari kutoa zaidi, kwa kuhusiana na wanaotoa zaidi, basi maisha yako yatakuwa ya furaha.

Kitendo cha kujua kuna watu wapo kwa ajili yako, na wewe upo kwa ajili ya wengine kinakufanya uridhike na maisha na kuwa na furaha.
Kwa upande mwingine mahusiano hasi, yasiyo na maelewano, yenye msuguano mara zote, ni chanzo cha kukosa furaha kwa wengi.

UFUNGUO WA FURAHA:Tengeneza mahusiano chanya kwenye maisha yako, chagua wale watu ambao ni wa muhimu kwako na unapenda kuwa na mahusiano bora na wao, kisha wape muda na wajali zaidi. Kuwa tayari kujitoa zaidi kwa ajili yao, na wao watakuwa tayari kujitoa kwa ajili yako.

KUWA STADI UTAPATA FURAHA YA KWELI KATIKA MAISHA YAKO.

Umahiri katika jambo fulani unalofanya kwenye maisha yako. Mtu unakuwa na furaha pale unapojua kwamba kuna kitu unaweza kukifanya vizuri na kikawa na msaada kwenye maisha ya wengine.

Mtu unakuwa na furaha pale unapofanya kitu chenye maana kwako na kuweza kukifanya kwa ustadi na umahiri wa hali ya juu. Hata kama kitu ni kigumu kiasi gani, unapoweza kukifanya vizuri, unajijengea kuridhika ndani yako na hiyo ndiyo inakufanya uwe na furaha ya kudumu.

Ukitaka kudhibitisha hili angalia watu ambao wanapata fedha nyingi bila ya kufanya kazi. Labda wameshinda bahati nasibu au wamepata urithi, maisha yao huwa mabovu sana licha ya kuwa na fedha nyingi. Ni kwa sababu wanakuwa hawajafanya kitu kikubwa kupata fedha hizo, na wengi huishia kuzipoteza.

UFUNGUO  WA   FURAHA: Chagua kitu au eneo utakalokuwa na ustadi nalo kwenye maisha yako, eneo ambalo utafanya vizuri na utaongeza thamani kwenye maisha ya wengine. Kama ni mwalimu fundisha vizuri sana, kama daktari tibu vizuri, kama mwandishi andika vizuri vitu vinavyowasaidia watu. Kadhalika kwenye kilimo, ufundi, uwakili na ujuzi mwingine wowote.