Wednesday, November 14, 2018

KATIKA MAISHA USIBWETEKE NA YALE ULIYOKAMILISHA TUU !!!

Katika MAISHA watu hufurahia zaidi yale waliyokamilisha pekee huku wakiyasahau kabisa yale ambayo hawajayafanya au kuyakamilisha.
 
Pia kitendo cha kuyafurahia yale ambayo umeyafanya na kujiona wewe ni bora zaidi hukufanya uzidi kubweteka na kuachana na yale unayoyakosea katika maisha.

 Hivyo NDUGU yangu MDAU  wangu  katika maisha haya unatakiwa kukumbuka ya kwamba yale uliyoyapanga na kuyakamilisha ni jambo jema sana, ila kama unataka kuwa bora zaidi ya hapo ulipo sasa unatakiwa kushughulika na yale machache yalikuwa ni vikwazo ambayo yamekufanya ushindwe kufanya vizuri zaidi.

Asante sana   kwa   kusoma , Ndimi  MWL   JAPHET  MASATU , DAR  ES  SALAAM, TANZANIA,  AFRIKA  YA  MASHARIKI.

No comments:

Post a Comment