Friday, November 16, 2018

HUDHURIA SEMINA AU WARSHA MBALIMBALI ZA KIBIASHARA UJIFUNZE MBINU MPYA ZA KIMAUZO. DUNIA INABADILIKA KILA SIKU. ACHANA NA MBINU ZA KIZAMANI ZA KIMAUZO.

Inapotokea mbinu zako za kimauzo zimepitwa na wakati huwezi kuendelea kuwapata wateja wengi. Hapa ndipo maana kampuni kubwa zikaja na kitengo cha huduma kwa wateja ili kila siku kuweza kumudu kuboresha huduma ili kuleta mafanikio. Kama kila wakati utaendelea kuwa na mbinu zile zile za kimauzo pasipo kuzibadilisha na kutegemea muujiza utakaokupa wateja wengi, naomba nikwambie kwenye hilo jambo lisahau kabisa. Ni muhimu ukabadilika kwanza wewe na wasaidizi wako.

NINI UFANYE ???
Kila mara pata mafunzo ya jinsi ya kuboresha huduma kwa wateja na unaweza kuyapata kupitia semina au warsha mbalimbali za kibiashara. Pia jenga urafiki na wateja ili wakusaidie kupata wateja wengine zaidi na zaidi ili kufikia mafanikio.

Ndimi  Mwl  Japhet  Masatu, Dar  es  salaam , Tanzania, Afrika  Ya  Mashariki.

EMAIL: japhetmasatu@gmail.com 

Call: + 255 716 924136 ( WhatsApp ) , + 255 755 400128

No comments:

Post a Comment