Sunday, October 10, 2021

WATU WENGI HUVUTIKA ZAIDI NA MATOKEO KULIKO MCHAKATO WA MATOKEO YENYEWE----NA KOCHA MWL. JAPHET MASATU.

 

KITU HIKI NDICHO KINACHOKUZUIA USIPATE MAFANIKIO MAKUBWA-----NA KOCHA MWL. JAPHET MASATU.

Rafiki yangu mpendwa, Mdau  wangu
Unayataka mafanikio makubwa ndiyo maana unasoma hapa. Hongera sana kwa hilo.

Lakini kuna habari ambazo siyo nzuri sana kwenye hiyo safari uliyochagua. Takwimu za mafanikio zinatisha na kusikitisha.
Wanaoyataka mafanikio ni wengi, lakini wanaoyapata mafanikio hayo ni wachache mno.

Ni asilimia 1 tu ya watu kwenye eneo lolote lile wanakuwa wamefikia mafanikio makubwa. Huku asilimia nyingine 9 ya watu wakiwa na mafanikio ya wastani.
Kinachoumiza ni hiki, asilimia 90 ya watu kwenye eneo lolote lile hawapati mafanikio.

Siyo kwamba watu hao hawayataki mafanikio, wanayataka mno.
Siyo kwamba watu hao ni wazembe, wanajituma sana.
Lakini kwa namna fulani ambayo wengi hawaielewi, wachache ndiyo wanaofanikiwa huku wengi wakibaki bila mafanikio.

Kwa miaka mingi tafiti zimekuwa zinafanywa kuhusu kinachowatofautisha wanaofanikiwa na wanaoshindwa.
Kila ambacho watu walikuwa wanadhani ni sababu imegundulika siyo.




Watu walidhani elimu ni sababu, lakini siyo. Kuna watu wenye elimu kubwa waliofanikia na ambao hawajafanikiwa. Na kuna watu wenye elimu ndogo waliofanikiwa na ambao hawajafanikiwa.

Wakadhani labda ni mazingira na eneo ambalo mtu yupo, nayo ikawa siyo kweli. Kwenye kila eneo, kuna watu wamefanikiwa sana na kuna ambao hawajafanikiwa. Yaani utakuta watu wanakaa eneo moja, wanafanya kazi au biashara ya aina moja, ila mmoja amefanikiwa na mwingine hajafanikiwa.

Pia watu walidhani ni kurithi, lakini hilo pia siyo kweli. Kuna watu wanarithi mali nyingi na kupoteza zote na kuna watu wanaanzia sifuri kabisa ila wanafanikiwa sana.

Kukosekana kwa majibu ya wazi ya kinachowatofautisha wanaofanikiwa na wanaoshindwa kumefanya watu watengeneze sababu zao wenyewe.
Kwa kuwa binadamu hatupendi kukosa sababu au maelezo ya watu, pale mtu anapokuwa amepata mafanikio makubwa na hatuwezi kuelezea ameyapataje, basi tunajipa jibu.


Tunasema huyo ni FREEMASON, au ana majini, mshirikina na kauli nyingine za aina hiyo.
Kwa kuwa hatujui nini kinawatofautisha watu hao, tunaamini kutakuwa na nguvu fulani za kishirikina ambazo ndiyo zinawatofautisha.

Lakini hilo nalo siyo kweli, ni sababu tu ya kujiridhisha, ambayo inawaacha wengi wakiwa hawajafanikiwa na wachache sana kupata mafanikio makubwa.

Kwa utafiti mkubwa ambao nimeufanya kwenye eneo la mafanikio, nimegundua kuna kitu kimoja ambacho kinawatofautisha wale wanaofanikiwa sana na ambao hawafanikiwi.
Kitu hicho kipo kwa kila aliyefanikiwa na kinakosekana kwa wote ambao hawajafanikiwa.
Tatizo la kitu hicho ni kiko wazi kabisa, lakini wengi hawakioni wala hawakielewi.
Hata wale wanaofanikiwa sana, hawajijui kama wana kitu hicho. Na ndiyo maana hata wanapoitwa freemason au wana majini, wanakosa cha kujitetea kwa sababu hata wao wenyewe hawaelewi kwa nini mafanikio makubwa sana yanakuja kwao.

Kitu hicho kimoja ambacho kinawatofautisha wanaofanikiwa sana na wanaoshindwa nimekipa jina la UBATIZO WA MAFANIKIO.


Hii ni dhana ambayo imekuwa haifundishwi kwenye maarifa mengi ya mafanikio, kwa sababu siyo rahisi kueleweka na wala haiwafurahishi watu.

Kwenye mafunzo mengi ya mafanikio, watu wanapenda kusikia vitu vizuri na vya kuhamasisha. Lakini kwenye uhalisia wa mafanikio mambo ni tofauti kabisa. Hakuna aliyefanikia kwa kufanya vitu rahisi na kwa namna anavyojisikia yeye.

Ubatizo wa mafanikio ni dhana iliyobeba ugumu hasa wa mafanikio ni kiasi ambacho mtu anapaswa kujitoa ili kuyapata mafanikio makubwa.

Umewahi kusikia ubatizo kwenye dini mbalimbali, kwa sehemu kubwa ubatizo huo ukiwa wa maji.
Sasa ubatizo wa mafanikio ni tofauti kidogo, siyo ubatizo wa maji, bali ubatizo wa moto.
Ni ubatizo unaokuacha ukiwa imara na kuweza kupambana na chochote kinachokuja mbele yako, bila kukata tamaa wala kurudi nyuma.

Ukishapata ubatizo huo wa mafanikio kuna vitu viwili tu mbele yako, kupata unachotaka au kufa ukiwa unakipambania. Hakuna chaguo jingine.

Ubatizo wa mafanikio una vitu viwili vikubwa; KAFARA NA MASHARTI.
Huwezi kupata mafanikio makubwa kama hujatoa kafara.
Na hapa kafara haimaanishi kuua watu, bali kuondokana na baadhi ya vikwazo vinavyokuzunguka sasa.
Pia huwezi kufanikiwa kama hujajiwekea masharti makali kwenye maisha yako.

Je upo tayari kupata ubatizo wa mafanikio ili ujihakikishie kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yako?


Kama jibu ni ndiyo basi   JIUNGE     NA  DARASA  ONLINE      UJIFUNZE    ZAIDI  KWA  UNDANI . Ndani ya  " DARASA  ONLINE " utajifunza kwa kina kuhusu dhana hii ya ubatizo wa mafanikio na jinsi unavyoweza kujibatiza wewe mwenyewe ili ufanikiwe.

Kwa  KUJIUNGA   NA  DARASA    ONLINE "  na  kuchukua hatua, mafanikio kwako litakuwa swala la muda tu, hutakuwa na wasiwasi wowote kwamba huwezi kufanikiwa.

TUWASILIANE   KWA  WhatsApp + 255 716 924136  /  + 255 755 400 128

 

TEHAMA---DARASA LA SITA ( STD 6 )---SURA YA 5---PROGRAMU JEDWALI-----KWA SHULE ZA MSINGI----TANZANIA---( PDF )

TEHAMA--DARASA LA SITA ( STD 6 )----SURA YA 1----MAWASILIANO----KWA SHULE ZA MSINGI-----TANZANIA----( PDF )

WAJIBIKA KWA JAMII IPASAVYO KILA SIKU MPAKA KIFO-----NA KOCHA MWL. JAPHET MASATU.

Friday, September 3, 2021

MITIHANI YA MAISHA HAINA MWISHO , UKISHINDA MTIHANI HUU UNAKUJA ULE.

Bila maandalizi maishani ni kukubali kushindwa au kufeli. Maandalizi hutusaidia kupunguza mawezekano ya kushindwa, kushangazwa au hata kuumia. Wanasema wakati wa vita sio wakati sahihi wa kufanya maandalizi isipokuwa kabla ya vita ndo ulikuwa wakati sahihi wa kujiandaa. Si hilo tu hata maisha ya kila siku bila maandalizi ya mapema ni mtu kujiandaa kushindwa au kuumia zaidi.

Imekuwa ni kawaida yetu sisi binadamu kutoweka uzito katika maandalizi ya mambo mengi maishani na hili linajitokeza kutokea kwa mambo yakitukuta hatukuwa na maandalizi yoyote yale. Inawezekana ni suala la kiuchumi, mahusiano au hata masuala ya kiafya huwa hatujiandai mpaka pale mambo yamejitokeza na kutuzindua kuwa tulipaswa kujiandaa mapema kabisa.

Maisha yamejaa mitihani na majaribu katika kila kona ya kuishi kwetu ikiwa ni kutufungua na kutukumbusha ilivyo haja kubwa ya kuwa na maandalizi mapema ya mambo hayo. Mambo mengi yanayojitokeza na tukayaona ni kama yametokea ghafla kama ajali ni kuwa hatukuwa na maandalizi nayo. Kila mtego ambao mtu anaweza kukutwa amenaswa ni kuwa hakugundua mapema kuwa ilibidi kujua ishara za awali na kujiandaa ili asijekushindwa katika mtihani huo. Wengi tumejikuta tunaanguka katika mambo mengi maishani sababu ya kuondoa nafasi ya maandalizi ambayo ilipaswa kuwepo kila siku.

Maisha hayaachi kutufundisha uhalisia wake kuwa kuna nyakati ngumu na nyepesi, furaha na huzuni, giza na nuru, kushuka na kupanda, kufaulu na kufeli na kuishi na kufa. Safari zote hizi hujitokeza na zinakuja wakati wowote ule ambao mtu anaweza asitegemee ingekuwa hivyo. Bila maandalizi ya kujua hilo ndo kunakozalisha kuyaona maisha yana sura moja tu ya kuwa ni magumu na yasoruhusu watu kuwa na furaha. Yote hujitokeza sababu ya mtu kukosa kujiandaa na kujua ukweli huu wa maisha kuwa wakati wowote ni safari ya maandalizi kwa kuwa mitihani haikosi kuwepo maishani.

Tunapaswa kujiandaa kukutana na kila aina ya watu ambao wanaweza kutufundisha vitu au kutuachia maumivu, wanaweza kutusaidia kukua au kutudumaza kabisa, watu wanaoweza kutuunga mkono au kutukatisha kabisa tamaa, watu ambao watafurahia hatua zetu au kutozifurahia. Aina ya watu hawa tunaweza kukutana nao katika safari ya maisha yetu ya kila siku. Tunapokosa kuwa tayari kujiandaa kwa hilo tunakubali kuumia na kushangazwa na mambo yatakapojitokeza.

Jiandae kwa kila hatua yako hasa pale ambapo upo karibu na watu wanaokuzunguka. Watu wanaotuzunguka wana uwezo mkubwa wa kutufanya tujikute tunaumizwa nao kwa vitu ambavyo wanaweza kuvifanya na tukabaki kushangaa kwa sababu huwa hatujiandai kuwa hata wanaotuzunguka ni watu wenye madhaifu na wanaweza kutuumiza pia. Mitihani ya maisha inaweza kuja kutoka eneo lolote na mtu anapokosa kujua hili tu ni kujiandaa kuumia na kushangazwa na mambo hayo.

Jiandae kwa kuyaweka mambo katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni lile lile la kuangalia mambo yaliyo katika uwezo wako ushughulike nayo na kundi la pili ni yale mambo yaso katika uwezo wako uyaache kama yalivyo au kuwa tayari kuishi nayo. Ni falsafa ngumu kuifuatilia ila inampa nguvu mtu katika kujiandaa na kukabiliana na mitihani maishani na majaribu mengi ambayo hujitokeza kutupima na kufungua uhitaji wa kujiandaa zaidi kila siku. 

JIUNGE  DARASA--ONLINE  "  UJIFUNZE   MENGI USIYOYAJUA  TUWASILIANE  SASA  NIKUUNGE KWA   DARASA. "

NA KOCHA   MWL. JAPHET  MASATU , DAR  ES  SALAAM , TANZANIA

WhatsApp + 255 716924136  /    + 255  755 400128

 

Thursday, September 2, 2021

KUWA NA VIPAUMBELE KATIKA MAISHA NA VIFANYIE KAZI



Tunaingia katika taabu maishani sababu ya kukosa msingi wa kujipa msimamo dhidi ya mambo fulani fulani katika maisha. Mtu anaporuhusu kila kitu kiwe sehemu ya maisha yake ni kuruhusu kuyaweka maisha hatarini. Mtu anayekosa msimamo ni rahisi kuyumbishwa na hali zozote zile zitakazojitokeza katika safari ya maisha. Na watu wengi wapo katika hatari hii ya kutoyapa maisha msimamo au msingi fulani unaowaongoza kutoyumbishwa na mambo maishani.

Msimamo hauendi pekee katika maisha bali hata uendeshaji wa kazi unahitaji mtu ajiwekee msimamo fulani ili kutoyumba kwa kazi zake. Mfano kama kazi ya utabibu mtu akikosa msimamo fulani alojiwekea wa kazi ni rahisi kuyakubali mambo mengine ambayo ni nje na maadili ya kazi yake.

Msimamo huu wa maisha ni kuchagua mambo ambayo hutakuwa tayari kuyavunja iwe kwa namna yoyote ile mtu atashawishiwa. Msimamo huu ni katika kuweka ugumu wa kutovunja ahadi ambayo mtu amejiwekea mwenyewe dhidi ya misingi fulani maishani. Hili humsaidia mtu kuwa na maisha yasoyumbishwa.

Ni hatua ngumu ambayo si watu wote wanaweza kuiendea katika maisha. Kuwa maisha yao yataongozwa na misimamo fulani fulani ambayo itawafanya waonekane ni watu wenye misimamo mikali dhidi ya wengine, au watu wasojali hisia za watu wengine. Ila hakuna matokeo mazuri maishani yanaweza kujitokeza isipokuwa kwa mtu kuweka mambo yake katika msimamo asokubali kuvunja kwa namna iwayo yoyote ile.

Weka msimamo katika kazi unayofanya, weka msimamo katika namna unavyohusiana na watu na weka msimamo katika mambo yote unayojua bila kuwa na msimamo thabiti basi mambo mengi yanaweza kuharibika. Hili litakusaidia kuwa na maisha yenye uimara na utulivu wakati wote. Kuna faida kubwa katika kujenga msimamo maishani ili lolote linalokuja kwako linakukuta ukiwa imara na hutayumbishwa na kitu chochote kile. 

 

NA  KOCHA  MWL.  JAPHET  MASATU , DAR  ES  SALAAM , TANZANIA.

WhatsApp + 255 716 924 136 / + 255 755 400128 / + 255 68 361  539

 

MAGUMU , MATATIZO NI SEHEMU UKUAJI KATIKA SAFARI YA MAISHA , USIJILAUMU NA KULALAMIKA

Kujilaumu ni kitendo cha kujiona mwenye hatia dhidi ya jambo fulani unaloona kwa namna moja umelisababisha litokee na linakuumiza sana ukilitafakari. Hali hii ni mbaya tena iso na usaidizi wowote ule mbali na kuongeza ugumu na taabu ya jambo apitialo mtu. Mtu anaweza kuendelea kuumia juu ya jambo alofanya iwe ni siku za karibuni au miaka mingi imepita. Haisaidii kujilaumu au kulaumu mtu juu ya matukio mbalimbali yanayotokea maishani.

Jamii zetu nyingi tumejengewa hali za kulaumu watu pale mambo yanapoenda tofauti na vile ambavyo tumepanga. Hivyo watu wengi kulaumu wengine inakuwa inaonekana ni kisingizio cha kujiondoa dhidi ya jukumu hilo na kuona wengine walipaswa kuadabishwa kwa hilo. Wakati wote kulaumu au kujilaumu hakujawahi kusaidia kutatua majukumu ya maisha mtu anapoishi. Ni kujisahaulisha tu kuwa tatizo halipo ingali tatizo lipo.

Eneo mojawapo ambalo watu wengi huanza kujilaumu ni pale ambapo vipindi vya hali ngumu maishani vinapobisha hodi, watu hujilaumu huenda wao si watu wenye bahati maishani, wao ni watu wanaonewa, wao hawastahili kupitia hayo na wengine ni kuona ni mikosi tu wao kutokoma kupitia hayo magumu. Magumu ni tafsiri yetu tunayoiweka katika yale yanapotokea maishani. Inaweza kuwa ni matukio yenye kuumiza yamekuja kwa mkupuo kama misiba, hali zisizoleta dalili za afueni iwe ni mahusiano au uchumi, hali za kiugonjwa na kadhalika.

Magumu hutukuza misuli ya akili, hutukuza kuwaza kiutu uzima. Hili ndilo linalowasaidia watu wengi katika umri mdogo kuwa na uwezo mkubwa wa kukabiliana na maisha ambapo kumetokana na wao kupitia magumu na magumu hayo hayakuwadumaza bali yaliwasaidia kukua zaidi. Si rahisi mtu aliyepitia magumu na yakamsaidia kukomaa kushangazwa na hali ngumu za maisha zikitokea maana tayari anajua na uzoefu wa kupitia magumu ya awali. Watu imara hawatengenezeki kwa njia rahisi isipokuwa kwa darasa la kushinda changamoto na kukabiliana na kila gumu njiani.

Mtoto ambaye anaepushwa asipitie magumu au kujua uhalisia wa maisha mapema ni kumwandaa kutokuwa imara siku za baadaye. Atakapokuja kuishi na kukutana na magumu kwa mara ya kwanza lazima itampa wakati mgumu sana kukabiliana na hilo. Huenda wazazi wengi wanaogopa kuwaambia watoto wao juu ya ugumu katika kuyakabili maisha kwa kuona watakuwa wakiwaonea ila si kweli bali wanawapa wakati mgumu baadaye watakapopita katika magumu hayo. Magumu humfanya mtu akutane na ukweli wa maisha kuwa maisha ili ukue kiuzoefu lazima upite magumu mbalimbali yanayomjenga mtu kuwa imara na kuyaendesha maisha.

Uhalisia wa maisha ni kuwa mtu atapitia magumu katika siku za kuishi kwetu. Magumu yapo na yataendelea kuja kwa namna tofauti tofauti. Si kuyalaumu pale yanapokuwa zamu yake kujitokeza. Magumu hutuimarisha na kutukuza kuyaona mambo

NA  KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU , DAR  ES  SALAAAM , TANZANIA

WhatsApp + 255 716 924136 / + 255 755 400128  /   +  255 688  361 539


 

KUPOTEZA " TUMAINI " NI KITU KIBAYA SANA KATIKA MAISHA

Maisha yanaweza kukupitisha katika nyakati ngumu ambazo mbele yako huoni kama utatoka au kuna nafuu yoyote. Nyakati hizi ndizo zinazofanya wengine wasiamini kama lipo tumaini au njia ya kuvuka. Ni lugha ngumu mtu kukuelewa pale anapopitia magumu na unamwambia kuwa hayo magumu utashinda tu huku akiangalia hakuna dalili zozote za suluhisho. Kibinadamu si hali rahisi kushawishiwa kuwa mambo yatakaa sawa na yatapita. Hili ndilo ambalo watu wengine huamua kukatisha maisha yao kwa kuona hawaoni msaada unaoweza kuwatoa walipo.

Hali ya kukosa tumaini inaweza kumkuta mtu yeyote yule katika zama tuishizo. Mambo yanapobadilika ghafla na matarajio mbalimbali kupotea ni hali inayosababisha mtu ashuke hamasa ya kufanya vitu, changamoto zinapokuwa hazikomi, hali ngumu za kiuchumi, migogoro katika kazi au mahusiano, nyakati ngumu za masoko na biashara vinapokuja kwa pamoja kwa mtu mmoja si jambo jepesi la kuvumilika. Ni wengi utakuta wanapata hali ya kukosa hamasa, wanashuka ari ya kufanya kazi na mzigo unapowazidia basi tumaini la nafuu ya hali wapitiazo hufifia au hata kuzima kabisa. Inahitaji ustahimilivu, faraja na nguvu ya kutia moyo na watu wengine kipindi cha hali ngumu.

Mtu anapoanza kupoteza matumaini ni dalili za hatari ambapo asiposaidiwa ni rahisi kufanya maamuzi mabaya ya kimaisha. Hali ya kukosa tumaini huanza pale ambapo mtu huanza kukata tamaa kwa yale anayoyapitia. Huenda ni katika kila jaribio mtu anaona kushindwa na kuanguka. Kukata tamaa kunamsababisha mtu afadhaike na kupata hali ya kupata hatia, kuona hamasa haipo tena na kujawa na hali ya kukata tamaa kabisa ya kimaisha. Hali hizi huwatokea watu wengi wanaopitia hali za sonona katika maisha ambapo kutokana na hali mbalimbali walizoshindwa kuzikabili basi wakajikuta wanazidiwa na kupoteza tumaini.

Magumu katika maisha hayakosekani na si kuwa watu hawapitii magumu. Ikiwa kila mmoja atahadithia simulizi ya yale aloyapitia utakuja kuona unayoyapitia huenda ni madogo. Kinachotia moyo ni kuwa wapo ambao maisha yao ukiyatazama unaona la kwako unalopitia ni dogo na wakati mwingine maisha yao yanaweza kukutia moyo kuwa hupaswi kumbe kukata tamaa. Kila wasaa unapoona tumaini linafifia jipe wasaa wa kuona watu wengine wenye magumu zaidi wasivyokata tamaa wala mioyo yao kuinama.

Unaweza kupoteza kila kitu maishani na ukarejea tena katika kuyaishi maisha endapo hutapoteza “tumaini”. Watu wengi ambao wamepitia magumu, taabu na shida na wakainuka tena hawakupoteza tumaini. Waliweka tumaini kuwa licha magumu yote ambayo yamejitokeza bado wanaona ipo njia, hali zitabadilika na mbele kuna njia ya kutoka. Maisha huwa mapya pale ambapo kila unapopitia magumu hupotezi tumaini kwa kile unachokifanya, tumaini la kuishi na tumaini la kuona kila kitu kitakuwa sawa kadri muda unavyoenda.

Kuna nyakati ambazo nilipitia ngumu sana, niliona siwezi kuinuka tena, niliona ndo mwisho wa kile nilichokuwa nakitegemea ila ninashukuru kuwa nilibakiwa na hali ya kuwa na tumaini kuwa hali nayoipitia itapita. Hili limekuwa likinisaidia hata sasa kuwa kwa kila hali ambayo itatokea iwe ngumu, yenye misusuko mingi nachotakiwa kukitunza ni kuwa na tumaini kuwa mambo yataenda tu. Tumaini ni ukombozi mkubwa katika maisha tuishiyo duniani.

NA  KOCHA   MWL.  JAPHET  MASATU , DAR  ES    SALAAM

WhatsApp + 255 716924136 /   + 255 755 400128

 

Wednesday, July 21, 2021

BIASHARA YA GENGE : JINSI YA KUIENDESAHA NA KUFANIKIWA.

Rafiki yangu mpendwa,
Nimekuwa naamini na kusema hili mara kwa mara na nilirudie tena hapa, kukosa mtaji siyo sababu ya kushindwa kuingia kwenye biashara. Ni kisingizio tu.

Sasa visingizio vyote huwa ni vya uongo, kwa sababu vinaficha kile ambacho mtu hataki kukikabili.

Wengi wanaotumia kisingizio cha mtaji, hawapo tayari kuukabili ukweli kwamba ni wavivu, wazembe, wasio tayari kujitoa na wanaopenda mazoea. Ni vigumu sana mtu kukiri una tabia hizo, hivyo kisingizio cha mtaji au muda kinakuwa rahisi.

Kwa zama tunazoishi sasa, hakuna kinachoweza kumzuia mtu aliyejitoa kweli kuingia kwenye biashara. Siyo wazo, siyo mtaji na wala siyo muda.
Kinachomzuia mtu hakitoki nje, bali kipo ndani yake.
Na yule ambaye hana kizuizi cha ndani, anaweza kuyafanya makubwa mno.




Chukua mfano wa biashara ya genge la mahitaji muhimu ya kila siku kwenye familia.
Ni biashara yenye uhitaji, kwa sababu watu kila siku wanakula.
Ni biashara unayoweza kuanza kwa mtaji kidogo.
Ni biashara ambayo huhitaji kuwa na eneo la gharama kubwa kuifanyia.
Na ni biashara ambayo haina vitu vingi, hivyo unaweza kuisimamia vizuri.

Hii ni biashara ambayo mtu ambaye hana shughuli nyingine ya kufanya anaweza kuianzisha, akaiendesha vizuri na ikawa sehemu ya yeye kupiga hatua na kuelekea kwenye biashara kubwa zaidi.

Unapochagua kufanya biashara kama hii, unapaswa kuifanya kwa tofauti, ili ikue na kuweza kuzalisha biashara nyingine kubwa zaidi.

Huenda unawajua wauza genge ambao miaka yote unawaona wakiwa pale pale. Siyo kwamba biashara hailipi, ila wanaifanya kwa viwango vya chini.

Kwenye makala hii unakwenda kujifunza jinsi ya kuifanya biashara ya genge kwa viwango vya juu sana na ikawa na manufaa makubwa kwako.

Kabla hatujaingia kwenye ushauri, tusome aliyotuandikia msomaji mwenzetu aliyeomba ushauri kwenye hili.

“Nahitaji kufungua genge la matunda na mboga mboga napenda kuelimishwa namna ya kuboresha iliniweze kukuza biashara yangu na wateja wavutiwe na huduma yangu.” – Hussein B. M.

I. MAONO MAKUBWA.
Anza kidogo lakini fikiri kwa ukubwa. Japo unafanya biashara ya genge, kwenye fikra zako usione genge, bali ona biashara kubwa kabisa.
Ona ukiwa na maduka mengi ya kuuza mahitaji hayo ya msingi na ona ukifanya kwa kiwango kikubwa zaidi.
Ni maono makubwa unayokuwa nayo ndiyo yanakusukuma kupiga hatua kubwa pia.
Tunapata kile tunachoona, hivyo kuwa na maono makubwa na jisukume kuyafikia.

II. BIDHAA BORA.
Kwenye biashara ya genge wateja wanaangalia vitu vikuu viwili, bidhaa bora na kwa bei nafuu. Pambana kuwapatia wateja vitu hivyo viwili na watakuwa wako kwa muda mrefu.
Chagua bidhaa zilizo bora kabisa ndiyo uweke kwenye biashara yako.
Jua maeneo unayoweza kupata bidhaa hiyo bora kwa bei nafuu ili pia uweze kuwauzia wateja wako kwa bei nzuri.
Jiwekee viwango vya ubora wa bidhaa utakazouza ili wateja waweze kujenga imani kwako na kwa biashara yako.

III. ENEO ZURI.
Biashara yako inapaswa kuwa eneo ambalo ni rahisi kuwafikia wateja wako na hata wateja kuifikia pia.
Kwa kuwa unachouza ni mahitaji muhimu ya maisha ya kila siku, biashara itafanya vizuri pale inapokuwa eneo lenye watu wengi.
Lakini pia mazingira ya eneo lako la biashara yanapaswa kuwa safi na mazuri, yamfanye mteja aiamini na kuithamini biashara yako.
Wengi wanaofanya biashara ya genge hawaweki maeneo yao ya biashara kwenye mwonekano mzuri, ukifanyia kazi hilo unajitofautisha kabisa na wengine.

IV. HUDUMA BORA KWA WATEJA.
Wahudumie vizuri saba wateja wako ili waweze kurudi tena na tena. Wasikilize kwa umakini na wajali pia. Jua mahitaji yao na uwatimizie.
Usiuze tu na kuishia hapo, jenga mahusiano mazuri na wateja wako na hayo yataiwezesha biashara kukua zaidi.
Pale wateja wanapopata huduma nzuri, wanaendelea kuja na wanawaleta wengine pia.

V. KUWEKA MAFUNGU.
Unayajua mahitaji ya wateja wako, unaweza kutengeneza mafungu ya vitu vinavyonunuliwa kwa pamoja na kisha kumshawishi mteja anunue kama fungu badala ya kununua kimoja kimoja.
Kumsukuma kuchukua hatua, hakikisha bei ya fungu inakuwa na unafuu kuliko mteja akinunua kimoja kimoja.
Njia hii itakuwezesha kuuza zaidi kwa wateja ambao tayari unao, ambao ni wateja wazuri tayari.

VI. KUWAFIKIA WATEJA.
Usisubiri tu wateja waje, badala yake watuate kule walipo. Watu sasa wametingwa na mambo mengi wanaweza kusahau kabisa hata uwepo wako.
Hivyo watembelee wateja wako maeneo walipo na kuwashawishi kuja kununua.
Hapa pia unaweza kutoa huduma ya mteja kuagiza na kupelekewa bidhaa zake.
Na kama umeziweka bidhaa kwa mafungu na bidhaa zako ni bora, mteja anaagiza na kupelekewa, akijua anapata anachotaka na ambacho ni bora pia.

VII. KUWASILIANA NA WATEJA.
Omba mawasiliano ya wateja wako na wasiliana nao mara kwa mara.
Unajua wateja wa genge wanapanga mahitaji yao ya siku asubuhi. Unaweza kuwatumia ujumbe asubuhi kuwasalimia na kuwaomba oda pia. Mteja anapopata ujumbe wako, anakufikiria kwa muda mrefu na hilo linamshawishi kuja kununua kwako.
Tumia kila sababu na ushawishi kupata mawasiliano ya wateja wako na wasiliana nao kwa njia ambayo siyo ya usumbufu kwako.

VIII. KUWEKA AKIBA.
Kwa lengo lako la kufika kwenye mafanikio makubwa kibiashara, unapaswa kuweka akiba kwenye kila faida unayoingiza kwenye biashara yako.
Wakati biashara inafanya vizuri, usibweteke na kuona mambo yataenda hivyo wakati wote.
Weka akiba ambayo itakusaidia wakati biashara haiendi vizuri.
Akiba hiyo ndiyo itakusaidia kwenye ukuaji wa biashara yako.

IX. KUKUZA BIASHARA.
Kwa kuwa una maono makubwa ya biashara yako, kila wakati angalia fursa za ukuaji zaidi.
Kila wakati piga hatua kuikuza biashara yako zaidi.

X. KUJIFUNZA KILA SIKU.
Kujifunza kila siku ni hitaji muhimu la ukuaji wa biashara yako.
Kila siku hakikisha unajifunza kitu kwenye kuikuza biashara yako.
Biashara inahitaji ubobezi maeneo mbalimbali kama masoko, mauzo, fedha, ushawishi na uongozi.
Soma vitabu mbalimbali vya biashara yako na  unayojifunza yafanyie kazi.

Saturday, July 10, 2021

MITANDAO YA KIJAMII INAELEKEA KUWAGAWA WATU KATIKA MAKUNDI HAYA.

Umakini wako ndiyo utajiri wako, kama utaweza kuweka umakini wako wote kwenye kile unachofanya, kwa hakika utaweza kuongeza kipato chako maradufu.

Mtaalam Mmoja Aliwahi Kusema Hivii.Siku zijazo, kutakuwa na makundi makuu mawili ya watu duniani.

Kundi la kwanza litakuwa la wale ambao wanaruhusu umakini wao kudhibitiwa na watu wengine, ambao wanaruhusu kila aina ya usumbufu kuwaingia. Kundi hili litakuwa na watu wengi sana, na mara zote watakuwa wamevurugwa na wasiweze kufanya makubwa kwenye maisha yao.

Kundi la pili litakuwa la wale ambao wanadhibiti umakini wao na kutoruhusu usumbufu wa aina yoyote ile kuwavuruga. Kundi hili litakuwa na watu wachache sana, na hawa ndiyo watakaoweza kufanya makubwa na kufanikiwa sana.”

Swali kwako, je kwa hali inavyokwenda sasa kwenye maisha yako, unajiona ukielekea kwenye kundi lipi kati ya hayo mawili?

Na je ungependa kuwa kwenye kundi lipi? Kama ungependa kuwa kwenye kundi la kwanza huna cha kufanya, endelea kufuata mkumbo na kila aina ya kelele.

Lakini kama ungependa kuwa kwenye kundi la pili, basi yale yote ambayo umejifunza kwenye kitabu cha juma hili yafanyie kazi.

Jua usumbufu wako wa ndani na wa nje na tenga muda wa kufanya yale muhimu na kuepukana na usumbufu.

Maarifa tayari unayo, kama hutachukua hatua huna wa kumlaumu, utakuwa umechagua wewe mwenyewe.

Tuko kwenye vita, adui mkuu anajua yuko vitani ila wanaolengwa hawajui.

Hivyo unapaswa kuwa na maandalizi mazuri ya kupambana na vita hii ili uweze kutoka salama na siyo kuwa mfungwa.


KAMA UNATAKA MAFANIKIO MAKUBWA , USIWE " FAIR " KWENYE MAENEO HAYA KUMI ( 10 ).

Rafiki yangu mpendwa,
Kuna vitu waliofanikiwa sana wanavijua, lakini huwa hawaviweki wazi.

Wanafanya hivyo kwa sababu jamii huwa haielewi vitu vingi kuhusu mafanikio, na hivyo huishia kuwashambulia waliofanikiwa pale wanapojaribu kuwa wakweli.

Mara ngapi umesikia masikini wakiwasema matajiri kwamba ni freemason au wamepata utajiri wao kwa njia za giza?
Umewahi kumwona tajiri akibishana na masikini juu ya hilo?

Jibu ni hapana, tajiri anajua masikini hawezi kuelewa na hata kuamini mengi yaliyomsaidia yeye, hivyo anamuacha aamini anachochagua kuamini.

Leo nakupa siri kubwa, nakupa ukweli mchungu ambao ukiweza kuupokea na kuuishi, utaweza kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yako.

Ukweli huo ni kama unataka mafanikio makubwa, basi usiwe ‘fair’.
Neno fair yaani usawa limekuwa linatumika sana.
Wengi wamekuwa wanalalamika kwamba maisha hayapo fair, pamoja na juhudi wanazoweka bado hawapati wanachotaka.

Leo nakwenda kukushirikisha maeneo 10 ambayo upaswi kuwa ‘fair’ kama unayataka mafanikio makubwa.
Kwenye maeneo hayo, unapaswa kuwa tofauti kabisa na wengine walivyo ili uweze kupata matokeo ya tofauti.




Kama unataka mafanikio makubwa, usiwe fair kwenye maeneo haya 10.

(1). USIWE  "FAIR"   KWENYE  KAZI.
Watu wengi wanafanya kazi kwa mazoea na kwa viwango vya chini sana. Wewe nenda kinyume nao, fanya kazi kwa juhudi kubwa na kwa viwango vya juu sana.
Anza kwa kufanya kazi muda mrefu kuliko wengine.
Kama wanaanza kazi saa mbili asubuhi na kumaliza saa 10 jioni, wewe anza saa moja asubuhi na kumaliza saa 12 jioni.
Kila siku weka masaa 2 mpaka 4 ya ziada kwenye kazi unayofanya.
Na unapofanya kazi  weka umakini wako wote kwenye kile unachofanya na usiruhusu usumbufu wowote ukuvuruge.

( 2 ). USIWE  "FAIR"  KWENYE  MUDA.
Watu wengi huwa wanachezea muda kama vile ni kitu ambacho hakina ukomo.
Lakini muda una ukomo, kuna masaa 24 tu kwenye siku, ukishayatumia huwezi kupata tena mengine.
Kuwa bahili sana wa muda wako, usikubali upotee hovyo kwa mambo yasiyo na tija.
Kila siku unayoianza pangilia muda wako, weka vipaumbele vyako vya siku na vifuate hivyo.
Kuwa na orodha ya mambo utakayoyafanya kwenye siku yako na ifuate hiyo.
Usiruhusu usumbufu au mahitaji ya wengine yaingilie ratiba yako muhimu ya siku.

( 3 ). USIWE  "FAIR"  KWENYE  FEDHA.
Watu wengi wakipata fedha huwa wanakimbilia kuzitumia mpaka ziishe na hata zikiisha hawaishii hapo, badala yake wanakopa ili waendelee kutumia zaidi.
Wewe usiwe hivyo, unapopata fedha yoyote ile, tenga kwanza akiba kabla hujatumia. Usitumue kisha inayobaki ndiyo uweke akiba, fedha huwa haibaki. Badala yake weka akiba kwanza kisha inayobaki ndiyo utumie.
Na akiba unayoweka, iwekeze mahali inapozalisha na kukua zaidi. Hiyo ndiyo njia ya uhakika ya kuondoka kwenye umasikini na kwenda kwenye utajiri.

(4). USIWE  " FAIR "  KWENYE  KUSUDI.
Watu wengi wanaishi maisha ya bendera kufuata upepo, hawalijui kusudi la maisha yao na hivyo ni rahisi kushawishiwa na chochote kinachopita mbele yao.
Wewe usiwe na maisha ya aina hii, pambana ulijua kusudi la maisha yako na kuliishi kila siku.
Jua kwa nini uko hapa duniani, maisha yako yanapaswa kuacha alama gani na jipe wajibu mkubwa unaokusukuma kuchukua hatua kila siku.
Ukiwa na kusudi unakuwa na msimamo.

( 5 ). USIWE " FAIR " KWENYE   NDOTO.
Watu wengi hawana ndoto kubwa, wanaishi maisha ya mazoea, wanafanya shughuli zao, wanapata pesa ya kula na wanaridhika na hayo.
Wewe usiwe mtu wa kuridhika na mambo madogo unayopata sasa.
Kuwa na ndoto kubwa sana, ndoto ambazo wengine wakizisikia wanaona kama umechanganyikiwa na wanakuambia haiwezekani.
Ni ndoto kubwa unazoziamini bila ya shaka zinazokusukuma kufanya makubwa zaidi kwenye maisha yako.

( 6 ). USIWE " FAIR "  KWENYE  KUJIFUNZA.
Watu wengi wakishahitimu shule, hawajifunzi tena vitu vipya wala kusoma vitabu. Watu hawasomi kabisa vitabu, wakiamini hakuna kipya wanachoweza kujifunza, tayari wanajua kila kitu.
Wewr usiwe hivyo, kuwa mtu wa kujifunza vitu vipya kila siku. Kuwa mtu wa kusoma vitabu kila siku.
Hakikisha kila mwezi unasoma angalau kitabu kimoja na kwa kila kitabu unachosoma chukua hatua za kuyabadili maisha yako.
Hilo pekee linatosha kukupa fursa nyingi na kukuwezesha kupiga hatua kuliko wengine.

(7).USIWE  " FAIR "  KWENYE  MAHUSIANO.
Walio wengi wanazungukwa na watu hasi, watu waliokata tamaa na wanaowakatisha tamaa pia. Mahusiano yao mengi yanakuwa kikwazo kwao kupiga hatua.
Wewe kuwa makini sana na mahusiano yote uliyonayo, hakikisha yanakuwa mahusiano bora na yanayokusukuma uwe bora zaidi.
Waepuke watu hasi na waliokata tamaa kama ukomo, usijenge ukaribu na watu wa aina hiyo, kwani watakuambukiza waliyonayo.
Ulivyo ni wastani wa watu watano wanaokuzunguka, chagua watano bora ambao watakusukuma upige hatua zaidi.

( 8). USIWE " FAIR "  KWENYE  KUJIAMINI.
Watu wengi hawajiamini, wanaweza kuwa na ndoto kubwa ila wanapowaambia wengine na wakawakatisha tamaa, wanawasikiliza na kukubaliana nao.
Ndiyo maana kundi kubwa la watu kwenye jamii hawawi na maisha wanayoyataka, maana hawajiamini kiasi cha kuwashinda wale wanaowakatisha tamaa.
Wewe jiamini kupitiliza, amini ndoto kubwa ulizonazo utaweza kuzifikia bila ya kujali unaanzia wapi sasa.
Hata kama wengine wanakuambia haiwezekani, hata kama wanakuonesha na mifano kabisa, usiwaamini zaidi ya unavyojiamini wewe. Jifunze yote muhimu na endelea kusimama kwenye ndoto zako kubwa.

( 9 ). USIWE  " FAIR " KWENYE  UNG"ANG"ANIZI.
Ili ufanikiwe lazima uwe king’ang’anizi sana, ujitoe kweli kweli na ukomae mpaka upate kile unachotaka.
Utakutana na magumu, vikwazo na kushindwa, lakini usiruhush hayo kuwa mwisho wa safari yako.
Jipe kiapo kwamba utapata kile unachotaka au utakufa ukiwa unakipambania, hakuna mbadala wa hilo.

( 10 ). USIWE " FAIR " KWENYE  KUTOA  KAFARA.
Ili upate kile ambacho hujawahi kupata, lazima uwe tayari kupoteza kile ambacho tayari unacho sasa. Kuna vitu vizuri unavyo sasa lakini ni kikwazo kwako kupata mafanikio makubwa unayotaka.
Wengi wanataka mafanikio lakini hawapo tayari kutoa kafara, kuachana na vile vizuri walivyonavyo sasa ili kupata vilivyo bora zaidi.
Ukiweza kuvuka hilo, utaweza kupata makubwa.

Ukiondoa usawa kwenye maeneo haya 10 muhimu, utakuwa na maisha ya tofauti kabisa na utaweza kufanya makubwa sana.
Lakini utakapokua na maisha ya tofauti wengi watakushambulia, hivyo utakuwa kama mpweke katikati ya kundi kubwa la watu.

Nakukaribisha ujiunge kwenye " DARASA  ONLINE " UJIFUNZE  MENGI  USIYOYAJUA.

Usikubali tena kuendelea kuwa fair kwenye mambo yanayokurudisha nyuma.
Chagua kushika hatamu ya maisha yako ili uweze kufanya makubwa.

Ndimi  rafiki yako  mpendwa,
KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU , DAR  ES SALAAM, TANZANIAW

 

WASILIANA  NAMI   SASA  KWA

 

 ( WhatsApp + 255 716 924136    )  + 255 755 400 128 

 

KILA MTU ANA KIU YA KUTENDEWA UKARIMU / MEMA---" UKARIMU NI MGUSO WA PEKEE KWA KILA BINADAMU.

Maisha yetu sisi binadamu yanahitaji mguso. Mguso wa kutendewa mambo mazuri hata kama sisi tunawatendea wengine mabaya au tu wabinafsi. Ile kiu ya kutendewa mambo kwa ukarimu huwa kunatugusa sana. Kiu hii au njaa hii imo kwa kila mtu katika moyo wake kutamani kuona anapata kutendewa mema na mazuri. Licha tunaweza kuishi katika nyakati ambazo zimejaa watu wenye chuki, wasio na upendo bado mioyo yetu inatafuta wapi itapata ukarimu, wapi upendo ulipo, wapi furaha ilipo na wapi pa kupata matumaini.

Jamii zetu zina upungufu mkubwa wa watu ambao wana mioyo ya majitoleo. Kila mtu anapambana kuona ni kwa vipi atafaidika kuliko namna atakavyosaidia wengine wafaidike kwanza. Hili linajenga watu wakose ukarimu, wakose kusaidia wengine na wengine hata kuzuia wengine kupata vitu vizuri. Ukarimu imekuwa bidhaa adimu katika maisha tunayoishi maana kila mtu anajifikiria yeye mwenyewe tu na kusahau kuangalia wengine.

Usijekushangaa pale mtu mkarimu anapoonekana ni bidhaa adimu sokoni anapokuwa ni mtu anayewajali wengine, anayewatanguliza wengine, anayejitoa kwa faida ya watu wengine, anayejitosa kuingia gharama kwa ajili ya watu wengine. Si jambo rahisi kupatikana kwa kila mtu kuwa tayari kuingia gharama katika kujisahau yeye kwanza na kuwafikiria wengine kuwa kwa kuwafanyia wengine ukarimu ni yeye mwenyewe kujifanyia ukarimu. Ni vile mtu anavyojitoa kusaidia wengine ni yeye anajisaidia, ni kama vile mtu anavyoona kuwanyima nafasi wengine kufanikiwa ndivyo na yeye anavyojinyima kufanikiwa. Lolote lile tunalowafanyia wengine si kuwa wanaathirika wao tu bali hata sisi tunaathirika iwe moja kwa moja au njia nyingine.

Watu waliojeruhika ni wengi katika mioyo yao, watu walipitia mateso na taabu ni wengi, watu walopita manyanyaso ni wengi. Tendo la ukarimu kwa makundi haya ya watu ni jambo kubwa lisiloweza kupimika. Watu hawa wana kiu na njaa ya kuona hata kidogo wapate kuona matendo mema na ya ukarimu yakifurika katika maisha yao. Tendo jema lina mguso na huacha alama kubwa kwa maisha ya watu.

Tunaishi sasa na ipo siku ambayo tutayaacha maisha haya ya mwili na kufa. Kumbukumbu la maisha yetu itaanzia kwanza katika wema tulotenda kwa wengine au ubaya kwa wengine. Matendo mema huliliwa sana na watu ambao walitenda katika siku za uhai wao. Matendo ya ukarimu hugusa mioyo ya watu na huacha alama njema ya jina la mtu duniani. Tafuta nafasi hata ndogo ya kuonesha matendo ya ukarimu kwa watu wanaokuzunguka. Utaacha mguso usiofutika katika maisha yao na hii ni maana njema ya kuishi kikamilifu na kuishi kwa umoja kwa kuhesabu watu wanaokuzunguka ni sehemu ya viungo vya mwili wako.

UJUMBE : TAFUTA   NAFASI YA  KUTENDA  TENDO   LA  UKARIMU. MUNGU  AKUBARIKI  SANA.

Ndimi  KOCHA   MWL.  JAPHET   MASATU , DAR  ES  SALAAM , TANZANIA.

 ( WhatsApp + 255 716 924136 ) / + 255  755 400 128 

 

TUMIA MBINU HIZI SIKU ZOTE KUPAMBANA NA CHANGAMOTO YOYOTE MBELE YAKO.

HAKIKISHA! Siku Zote Unapopambana Na Changamoto Yoyote Ile Usisahau Kutumia Mbinu Hizi Muhimu Zenye Matokeo Ya Haraka…!

Rafiki yangu mpendwa,

Katika maisha lazima ujue kila wakati unaweza kukutana na changamoto.

Na watu wanasema kila ukitoka kwenye changamoto moja utaingia kwenye changamoto nyingine, duniani hapa kama hauko kwenye changamoto basi utakuwa umetoka kwenye changamoto au unaelekea kwenye changamoto nyingine.

Shida sio changamoto unazokutana nazo, tatizo kubwa ambalo watu linawakabili ni namna ya kushughulika na changamoto ambazo zile zinatokea katika maisha yao.

Na Leo lingependa nikwambie namna ambavyo unaweza kutoka kwenye changamoto yoyote inayokukabili, inawezekana leo upo kwenye changamoto kwenye taaluma yako inawezekana leo upo kwenye changamoto ya mahusiano yako au upo kwenye changamoto ya kiuchumi, au upo kwenye changamoto ya kazi, kazi unayofanya au eneo lako la kiofisi au kwenye biashara yako.

Bila kujali upo kwenye changamoto ipi kuna maeneo manne ukiweza kuyazingatia yatakusaidia sana kutoka kwenye changamoto yako tena kwa haraka.

Kumbuka tena washindi ni wale ambao wakipita kwenye changamoto wanaondoka kwenye changamoto zao kwa haraka sana bila kuchelewa.

Jambo La Kwanza; Ambalo unatakiwa kulifahamu katika maisha yako ni kwamba unapopitia changamoto USIKUBALI ile hali ya kujiambia changamoto yako ni SPESHO.

Changamoto SPESHO, maana yake ni kuna watu wanafikiri wanapopitia matatizo ni wao ndio wa kwanza kupitia katika matatizo hayo na hakuna mtu mwingine yeyote aliyepitia katika changamoto hiyo.

SI KWELI, ukiwa na fikra ya namna hiyo utashindwa kabisa kukabiliana na changamoto yako.

Changamoto yoyote leo unayokutana nayo, cha kwanza ambacho ningependa nikuambie. Kuna mtu ameshawahi kukutana na changamoto kama hiyo, na katika wale waliokutana na changamoto kama hizo hakika wako ambao wameshinda hizo changamoto.

Lakini kuna mtu leo anapitia changamoto kama ya kwako na hakika anaweza akashinda pia, wewe ukajua na kufikiri kwamba changamoto yako ni SPESHO na hakuna mtu ambaye anachangamoto kama ya kwako, hakika hautavuka, hautatoka katika hiyo changamoto.

Kuna watu ambao wakipitia matatizo wanaona changamoto yao hakuna mtu mwingine yeyote mwenye nayo. Wanaona kama lile tatizo ndio mara yao ya kwanza wanalipitia duniani yaani ni kama limevumbuliwa hakuna mtu mwingine ambaye amekutana nalo.

SI KWELI, usikubali hata siku moja kwamba changamoto yako ni SPESHO hakuna mtu mwenye changamoto kama hiyo, ukiwa na fikra kwamba changamoto yako ni spesho , hautapata uvumbuzi mapema na utaona hakuna msaada.

Cha kwanza kabisa kataa fikra inayokuambia changamoto yangu ni spesho hakuna mtu kama mimi, mtu aliyopo kama mimi, hakuna mtu aliyepata matatizo kama mimi.

SI KWELI, wako wengi na wameshinda na wewe unaweza kuishinda.

Jambo La Pili; Unalotakiwa kulifahamu ni kwamba changamoto yoyote unayopitia ni SAIZI YAKO, watu wengi ambao changamoto zinawazidi sio kwa sababu wanashindwa kuzitatua kwa sababu walikata tamaa.

Ningependa nikuambie changamoto yoyote ile unayokabiliana nayo leo ya KIFEDHA, ya KIMAHUSIANO, ya KITAALUMA, KAZINI KWAKO au kwenye BIASHARA, inawezekana kabisa umekosa usingizi kabisa kwa sababu ya changamoto inayokukabili.

Ninachotaka nikuhakikishie ni kwamba changamoto hiyo unayokutana nayo leo ni SAIZI YAKO.

Ukiwa na fikra ya namna hiyo tafsiri yake ni kwamba utafanya kila unachoweza, kuweza kukabiliana nayo, unapokubali kwamba changamoto hii ni SAIZI YAKO. Unaulazimisha ubongo wako kutafuta suluhisho unaposema changamoto hii imenizidi umri unauambia ubongo wako ila tu kwa sababu hakuna kitu ninaweza kufanya.

Ninachotaka kukuambia ni kwamba changamoto ni saizi yako, ya mambo unayopitia leo.

Jambo La tatu; Ambalo ni la msingi sana, kulijua katika kutoka kwenye changamoto unayokutana nayo ni kujua katika kila changamoto KUNA MLANGO WA KUTOKEA, kuna njia za wewe kutoka kwenye changamoto ukweli ni kwamba hukuuona huo mlango wakutokea.

Ukweli ni kwamba haujaona njia za kutoka kwenye changamoto zinazokukabili haimaanishi kwamba changamoto yako imekosa suluhisho, kuna suluhisho kwenye changamoto yako inawezekana haujaiona ndio maana tunasema kama leo unapitia changamoto usikubali tu kukaa nyumbani, usikubali tu kukaa ndani, usikubali kujifungia, tafuta watu uzungumze nao, nenda mahali toka nje fuatilia kitu fulani utapata suluhisho.

Hakuna changamoto ambayo haina suluhisho katika maisha hata ya kwako, iwe inawezekana umefika sehemu unasema kwamba nimejaribu kila nilichofanya kupata suluhisho.

SI KWELI, changamoto uliyonayo ina suluhisho kama hutokata tamaa utapata suluhisho ya changamoto yako.

Jambo La Mwisho; Ambalo litakusaidia kutoka kwenye changamoto ambayo inakukabili sasa hivi kwa haraka sana nikijua kwamba changamoto zinapokuja saa zingine zinatuepusha na mabaya makubwa ambayo hatuyaoni.

Kuna watu wengi sana wanapitia changamoto za mahusiano na kusema yule nilimpenda sana, nikajitolea na leo hayupo tena kwenye maisha yangu, kuja kugundua kwamba hapana kumbe ni sababu ya wao kupata watu sahihi zaidi, kuna watu walifukuzwa kazi, kuna watu waliondolewa ofisini kwa kudhalilishwa lakini leo wanamiliki makampuni yao au wengine wamepata kazi kubwa zaidi.

Kwa hiyo kila wakati unapokutana na changamoto uwe na jicho la ziada la kuangalia usiangalie kile tu ulichokosa lakini pia kuna kitu ambacho kiko leo.

Kwa nini inakuwa hivyo mara nyingine tukiambiwa tuache vya sasa hivi tulivyonavyo ili tupate bora, tulivyoandaliwa mbele yetu hatutakuwa tayari kufanya maamuzi magumu ya namna hiyo kwa sababu yanatuumiza, lakini changamoto zinakuja pia kutuepusha na mabaya ambayo kwa macho ya kawaida hatuyaoni, ndio maana changamoto unayopitia leo ni mbaya na inakuumiza sana.

Lakini kesho utamshukuru mungu na kusema afadhali nimepitia hii changamoto. Kwa sababu imenisaidia kuwa hivi nilivyo sasa.

 KAZI   KWAKO   MDAU  WANGU .

TUWASILIANE   KWA 

 ( WhatsApp  + 255 716924136 )  kwa  USHAURI NA  MAONI  YAKO   WEWE  UNASEMAJE ??

JINSI MITANDAO YA KIJAMII INAVYOHARIBU AKILI YAKO NA JINSI YA KUEPUKA HILO.

Rafiki yangu mpendwa, mdau  wangu 
Ugunduzi wa mtandao wa intaneti yalikuwa ni mapinduzi makubwa mno kwenye maendeleo ya binadamu.
Kwani mtandao huo ulileta uhuru wa kila mtu kuweza kuwasiliana na yeyote akiwa popote.

Watu waliamini mtandao wa intaneti utaleta demokrasia na uhuru wa kweli, ambapo kila mtu anaweza kujifunza chochote anachotaka, anaweza kuwasiliana na yeyote na anaweza kushirikisha maoni yake bila kuzuiwa na yeyote.

Lakini ndoto hizo zimekuja kuyeyuka baada ya kugunduliwa kwa mitandao ya kijamii na simu janja.
Mitandao hii ambayo ilianza kama vitu tu vya watoto na vijana, sasa imepenyeza kwenye maisha ya walio wengi na imekuwa na madhara makubwa.




Mitandao ya kijamii imeharibu akili za wengi kwa njia mbalimbali, leo tunakwenda kuangalia njia moja ambayo ina madhara makubwa kwako na kikwazo kwa mafanikio yako.
Njia hiyo ni kutaka raha ya haraka (instant gratification).

Iko hivi rafiki, ili uweze kufikia mafanikio makubwa, lazima uwe tayari kuchelewesha raha (delayed gratification). Uweze kuweka juhudi kubwa mwanzoni na kuwa na subira kabla hujaanza kupata raha.

Hilo linajengwa na ukomavu wa kiakili, ambapo unaweza kuweka umakini wako kwenye jambo moja kwa muda mrefu bila ya kuhama hama.
Hicho ndicho ambacho mitandao ya kijamii inakwenda kuvunja na kukufanya uwe na uteja kwenye mitandao hiyo, kwa sababu unaitegemea ili kupata raha ya muda mfupi.

Muuzaji mkubwa wa madawa ya kulevya ambaye aliachana na biashara hiyo baada ya kufungwa kwa muda mrefu aliulizwa ni jinsi gani walikuwa wanapata wateja wengi wa kuwauzia madawa ya kulevya.
Muuzaji huyo alijibu walikuwa wakienda kwenye mji, wanawakusanya watumiaji wengi wa madawa kisha wanawapa ofa ya bure.
Haichukui muda watu hao wanakuwa wateja wao wa kudumu, kwa sababu madawa yanajenga uraibu kwao.

Hivyo pia ndivyo mitandao ya kijamii inaharibu akili yako, kwa kujenga uraibu wa kulata raha ya haraka.
Kabla ya ujio wa mitandao ya kijamii, watu waliweza kuweka muda wa kutosha kwenye kusoma vitabu au kufanya mazungumzo na wengine.
Lakini sasa mtu hawezi kusoma hata kurasa kumi kabla hajagusa simu yake. Watu wanaweza kuwa hawajaonana miaka lakini wanapokutana baada ya salamu kila mtu anahangaika na simu yake.

Kukufanya utake raha ya muda mfupi na kuwa tegemezi kwa mitandao hiyo kupata raha hiyo ndiyo madhara makubwa sana ya mitandao ya kijamii kwenye akili yako.
Hili linavunja kabisa ustahimilivu wako, ambao unahitajika sana ili uweze kufanikiwa kwenye maisha yako.

Akili yako ikishaharibiwa na mitandao ya kijamii, uwezo wako wa kuweka vipaumbele sahihi kwenye maisha yako unaharibiwa kabisa.
Unakuwa huwezi tena kuweka umakini wako kwa muda mrefu kwa yale ambayo ni sahihi kwako.
Mitandao hiyo inakujengea hofu ya uongo, hofu ya kwamba kuna kitu unakosa kama hujaingia kwenye mitandao hiyo hata ndani ya muda mfupi tu.

Tatizo kubwa zaidi ni kwamba hakuna anayeliona na kulizungumzia tatizo hili wazi wazi. Wanasema kulijua tatizo ni nusu ya kulitatua. Wengi ambao akili zao zimeshaharibiwa na mitandao ya kijamii hawajui hata kama wana tatizo. Wao wanaona ni sehemu ya kawaida ya maisha yao, kumbe wameshageuzwa kuwa tegemezi kwenye mitandao hiyo.

Tatizo hilo halizungumziwi kwa sababu wengi hawana uelewa na wale wanaomiliki mitandao hiyo wanapima mafanikio kwa idadi ya walio tegemezi kwenye mitandao hiyo.
Hivyo hili linabaki kuwa wajibu wako mwenyewe kama hutaki liendelee kuwa na madhara kwako.

Mitandao ya kijamii imeajiri watu wenye elimu kubwa kwa lengo moja tu, kuteka umakini wako na kukufanya kuwa tegemezi.

Ni wakati wa kuwa huru sasa na kushika hatamu ya maisha yako ili uweze kufika kwenye mafanikio makubwa.

Chukua hatua sasa maana kadiri unavyochelewa, ndivyo mitandao hiyo inavyozidi kutawala na kuharibu akili yako. JIUNGE   SASA  NA  " DARASA  ONLINE "   uanze  kubadili maisha yako.

Rafiki yako mpendwa

KOCHA  MWL.  JAPHET  MASATU , DAR  ES  SALAAM, TANZANIA

 WASILIANA   NAMI  SASA

 

 ( WhatsApp + 255 716  924136  )  / + 255 755 400 128

 

AFYA NI MTAJI NAMBA MOJA UNAOPASWA KUUJENGA NA KUULINDA ILI KUFANIKIWA.

Rafiki yangu mpendwa, mdau wangu
Mtaji umekuwa sababu ambayo wengi wanaitumia kama kikwazo kwao kufanikiwa.
Na wengi wanapozungumzia mtaji, huwa wanaangalia mtaji wa aina moja tu, fedha.

Kuna mitaji mingine muhimu ambayo mtu anakuwa nayo na anaweza kuitumia kufanya makubwa kwenye maisha yake, lakini haitambui wala kuitumia.
Anang’ang’ana na mtaji mmoja tu, ambao hata akiupata bado changamoto kwake haziishi.

Leo nakwenda kukushirikisha aina nyingine ya mtaji ambao unapaswa kujijengea na kuulinda ili uweze kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yako.

Kabla sijakuambia mtaji huo ni upi, kwanza nikupe taarifa muhimu kuhusu mafanikio, ambazo wengi wamekuwa hawakupi.

MOJA; mafanikio yanataka uweze kufanya maamuzi bora na haraka kuliko wengine. Maamuzi yanawatofautisha sana wanaofanikiwa na wanaoshindwa.

MBILI; mafanikio yanataka uweze kufanya kazi kwa juhudi kubwa na kwa muda mrefu kuliko wengine. Haijalishi unafanya nini, juhudi zinahitajika sana.

TATU; mafanikio yanakutaka uwe na uvumilivu mkubwa licha ya kupitia magumu na kukatishwa tamaa. Wanaofanikiwa siyo kwamba njia yao inakuwa rahisi, ila wanakuwa wagumu kuliko magumu wanayokutana nayo.

Vitu hivyo vitatu ni muhimu kuliko kingine chochote kwako kufanikiwa. Kufanya maamuzi sahihi, kuweka juhudi kuwa na kuwa mvumilivu.
Vyote hivi vitatu ni zao la AFYA.
Na hiyo AFYA ndiyo mtaji muhimu mno kwako kuweza kufanikiwa.
Bila ya afya bora, hakuna makubwa unayoweza kufanya kwenye maisha yako.




Wengi hudhani afya ni kutokuwa na magonjwa, lakini hilo siyo kweli.
Shirika la afya duniani linaeleza afya kama kuwa vizuri kimwili, kiakili, kiroho, kijamii na kiuchumi.
Kwa maana hiyo ya afya, unaweza kuwa huna ugonjwa wowote, lakini bado afya yako ikawa siyo nzuri.

Unaweza kujionea hapa ni kwa nini afya ndiyo mtaji muhimu kwako kufikia mafanikio makubwa, kwa sababu imegusa kila eneo la maisha.

Ili uweze kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako, unapaswa kujenga afya yako kwenye maeneo haya matano.

( 1 ).  MWILI.
Mwili wako ndiyo hekalu la maisha yako, ndiyo gari la kukufikisha kwenye mafanikio yako makubwa.
Bila mwili imara, hutaweza kuweka juhudi za kutosha ili uweze kufanikiwa.
Maana mafanikio yanakutaka uweke juhudi kubwa na kwa muda mrefu.
Jenga afya yako ya mwili kwa kuwa na ulaji mzuri, kufanya mazoezi na kupata muda wa kupumzika.
Linda afya yako ya mwili kwa kuepuka magonjwa na tabia hatarishi.
Mwili unapokuwa imara, unaweza kuendesha mapambano ya mafanikio.

( 2 ). AKILI.
Akili yako ndiyo inayofanya maamuzi, mafanikio yanahitaji sana maamuzi sahihi kwenye maisha. Hivyo ni muhimu kuijenga afya ya akili ili uweze kufanya maamuzi bora kwenye maisha yako.
Jenga afya yako ya akili kwa kuilisha maarifa sahihi na kufanya mazoezi ya kufikiri kwa kina katika hali mbalimbali. Pia kuwa na muda wa kutafakari mambo yako.
Linda afya yako ya akili kwa kuepuka habari hasi, vilevi mbalimbali na mitandao ya kijamii. Vyote hivyo vinadhoofisha akili yako na kuifanya isiweze kufanya maamuzi bora.
Bila ya maamuzi bora, mafanikio yatakuwa magumu kwako.

( 3 ). ROHO.
Roho yako ndiyo kichocheo cha wewe kuendelea na safari ya mafanikio hata pale unapokutana na magumu yanayokatisha tamaa. Kama haupo imara kiroho, hutaiweza safari ya mafanikio kwa sababu ina magumu na inakatisha sana tamaa.
Jijengee afya ya kiroho kwa kusali, kufanya tahajudi na kuwa na imani imara.
Linda afya yako ya kiroho kwa kuepuka waliokata tamaa na wasiokuwa na imani, maana mambo hayo huambukizwa kwa urahisi.

( 4 ). UCHUMI.
Uchumi ni eneo muhimu kinalokupa utulivu wa kuyaendesha maisha yako. Kama hujui kesho utapata wapi fedha ya kula, akili yako haiwezi kutulia kwenye mafanikio makubwa unayotaka kufikia.
Hivyo unapaswa kujenga afya yako ya kiuchumi ili uwe na uhakika wa kuyaendesha maisha yako wakati unaendelea kupambana na mafanikio.
Kujenga afya yako ya kiuchumi hakikisha una akiba ya kuweza kuyaendesha maisha yako kwa angalau miezi sita hata kama utapoteza kipato unachoingiza sasa.
Kulinda afya yako ya kiuchumi epuka matumizi kuzidi mapato yako. Kwa kila kipato unachoingiza, tenga sehemu ya kipato hicho ambayo utaweka kama akiba.

( 5 ). JAMII.
Jamii ni wale wanaokuzunguka, ambao unawahitaji sana kwenye safari yako ya mafanikio. Huwezi kufanikiwa peke yako, chochote unachotaka kinatoka kwa watu wengine.
Jenga afya yako ya kijamii kwa kuboresha mahusiano yako na wengine, kuwajali na kuweka maslahi yao mbele. Jua utapata unachotaka kwa kuwapa wengine kile wanachotaka.
Linda afya yako ya kijamii kwa kuepuka kuwasema wengine vibaya, majungu na kuwadhulumu wengine. Hata kama unaona unaweza kufanya kwa siri, jua kuna siku mambo yote yatakuwa hadharani.

Jenga afya yako kwenye maeneo hayo matano na utakuwa moto wa kuotea mbali kwenye safari yako ya mafanikio. Kwani utakuwa na mwili wenye nguvu ya kupambana, akili yenye uwezo wa kufanya maamuzi bora, roho yenye hamasa ya mafanikio, uchumi unaokuweka huru na jamii inayokupa kile unachotaka.




KARIBU  UJIUNGE   " DARASA  ONLINE " na ujifunze jinsi ulivyo na nguvu kubwa ndani yako za kukuwezesha kufanya makubwa mno.


Unaweza kuwa unajichukulia poa na kuona huwezi kufika kwenye mafanikio makubwa, lakini kwa kujifunza   zaidi   kwa  undani  utaona wazi nguvu zako zilipo na jinsi ya kuzitumia kufanya makubwa  na  kufanikiwa. HAKUNA  UCHAWI.


Rafiki, umejifunza hapa jinsi AFYA ilivyo mtaji muhimu kwako kufanikiwa, chukua hatua sahihi sasa ili kujenga afya imara itakayokuwezesha kufika kwenye mafanikio makubwa.

Rafiki yako anayekupenda sana,
KOCHA   MWL.  JAPHET   MASATU, DAR ES  SALAAM , TANZANIA

Tuwasiliane  nami  sasa ili  nikuunge  katika   "DARASA   ONLINE "  kwa   kutumia  EMAIL   YAKO   YA  GMAIL "


( WhatsApp  + 255 716 92 4136  ) /   + 255 755 400128

Tuesday, June 29, 2021

JINSI UNAVYOWEZA KUWA BILIONEA , HATUA KWA HATUA.

Whatever the mind of man can conceive and believe, it can achieve.” - Napoleon Hill

Rafiki yangu mpendwa,

Napoleon Hill, baada ya kufanya utafiti kwa watu zaidi ya 500 waliofikia utajiri mkubwa kwenye maisha yao na kuwalinganisha na wengine ambao hawakuweza kufikia utajiri, alikuja na kanuni rahisi ya mafanikio na utajiri aliyoishirikisha kwenye kitabu chake alichokiita THINK AND GROW RICH.

Sentensi moja ambayo unaweza kuitoa kwenye kitabu chake na ikabadili kabisa maisha yako ni ile inayosema; chochote ambacho akili ya mwanadamu inaweza kuelewa na kuamini, inaweza kukifikia.

Soma tena taratibu na uielewe kauli hiyo, kwani ina nguvu ya kuifungua akili yako na ikakuwezesha kupata kila unachotaka, ikiwepo kufika kwenye ubilionea.

Najua unavyosoma hapa kuna kisauti ndani yako kinakuambia hilo haliwezekani, kinakupa ushahidi kwamba katika mazingira yako hakuna aliyefikia ubilionea, wewe utawezaje. Sauti hiyo inakukumbusha kipato kidogo ulichonacho au madeni makubwa uliyonayo na kukuhakikishia huwezi kufika kwenye ubilionea.

Leo nina habari njema kabisa kwako, kwamba sauti hiyo haina nguvu kwako kama akili yako itaelewa na kuamini kile kweli unachotaka.

Na kwa ushahidi tu, hapo ulipo sasa hujafika kama ajali, bali ni matokeo ya kile ambacho akili yako imeelewa na kuamini kwa muda mrefu. Kama ulikuwa unaamini wewe ni wa chini na huwezi kupiga hatua, hayo ndiyo umezalisha mpaka sasa. Na kama utaamini unaweza kufanya makubwa, hilo pia ndiyo litatokea.

Ujumbe wangu kwako leo rafiki yangu ni huu, unaweza kuwa bilionea. Na ushahidi ni mabilionea ambao tayari wapo duniani. Kama wengine wameweza kufikia ubilionea, kwa nini wewe ushindwe?

Na kama alivyowahi kusema Benjamin Franklin, wachache kuwa matajiri ni ushahidi kwa wengine kwamba inawezekana.



Je upo tayari kujifunza kutoka kwa wale ambao wameweza kufikia utajiri na mafanikio makubwa kwenye maisha yako?

Kama jibu ni NDIYO  basi KARIBU    UJIUNGE   DARASA   ONLINE  LA  " MAISHA  NA  MAFANIKIO "  UJIFUNZE  SIRI   ZA  MAFANIKIO   YAO.

 WASILIANA  NAMI  SASA  ILI  NIKUUNGE.

KOCHA  MWL;  JAPHET   MASATU , DARA ES  SALAAM--TANZANIA

( WhatsApp + 255 716 924136 ) ,  + 255 755 400128

 

IJUE SIRI KUELEKEA SAFARI YAKO YA MAISHA NA MAFANIKIO

Siri Ambayo Itaharakisha Safari Yako Ya Mafanikio.

Picha linaanzia hapa,

 Mstari unachorwa kati ya wale wanaofika mbali na wale ambao hawafiki mbali.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa.

Na kuna mambo mengi sana watu wanajaribu kuyatofautisha katika makundi haya mawili.

Lakini moja ya eneo muhimu sana ambalo linafanya watu wafanikiwe sana na wengine wasifanikiwe ni namna wanavyotumia akili zao kufikiria kufanya mambo na kupata mawazo, lakini kuna aina mbili kisayansi ambazo zinaweza kutofautisha makundi haya ya watu wawili.

Aina ya kwanza tunaita GROWTH MINDSET na aina ya pili tunaita FIXED MINDSET, hizi ni aina mbili za watu wanavyofikiri labda kitu cha kujiuliza MINDSET ni nini?.

 MINDSET ni mfumo wa kufikiri ambao umeshajengeka ndani yako na hauitaji kujadiliana nao ili kupata matokeo.

Kwa maneno mengine unapokuwa na FIXED MINDSET, kwenye jambo Fulani ni kwamba jambo lolote linapotokea ubongo wako unakuwa  umeshaamua utafanya nini au utachukua hatua gani.

Lakini kwenye GROWTH MINDSET, tunasema ni ile hali ambayo ubongo wako unakuwa umeshajiandaa kupokea taarifa tofauti na zile ambazo hazikuwepo hapo kabla.

Ukweli ni kwamba watu wanaofanikiwa ni wale wenye GROWTH MINDSET.

Watu wenye GROWTH MINDSET, ni kwamba wako tayari kuanza kujifunza , ulishawahi kukutana na mtu ambaye hataki kabisa kujifunza anaamini yeye anajua kila kitu huyo hawezi kufanikiwa.

Mtu ambaye  anayefanikiwa kwenye GROWTH MINDSET ni mtu ambaye anasema ni kweli ninajua lakini ninahitaji kujua zaidi, ni mtu ambaye pia yupo tayari kuona watu wengine wanaweza kuliko yeye, mtu anayefanikiwa ni Yule anayesema ni kweli mimi ni mtaalamu kwenye uhandisi lakini ninaamini yupo mtu mtaalamu kwenye jambo la biashara kwa maneno mengine anaamini watu wengine wanaujuzi ambao yeye hana, na anauhitaji kukamilisha kile kitu ambacho anataka kukifanya lakini unapokuwa mtu wa FIXED MINDSET hutofanikiwa.

Watu wa FIXED MINDSET, moja ya sifa yao kubwa ni kwamba kila wakati wanajiona wao ni watu wanaojua sana, wanajiona wao ni watu wenye utaalamu kuliko watu wengine lakini kama kweli unataka kufanikiwa kwenye eneo lako  wanasema hivii siku zote unapotaka kufanikiwa tambua kwamba chochote unachokijua sasa hivi ni kidogo sana kuliko kile ambacho unatakiwa kukijua kwa maana nyingine unakuwa tayari kujifunza na kusonga mbele katika kufahamu kile kitu ambacho unakitaka, lakini kuna jambo ambalo unaweza kulifanya kwa haraka sana, ili kutoka kwenye FIXED MINDSET na kuelekea kwenye GROWTH MINDSET.

Jambo la kwanza, Kila siku tenga muda angalau wa nusu saa wa kujifunza kitu kipya katika eneo lako la utaalamu ambalo unaliishi kwa maneno mengine tafuta vitabu vitakavyokusaidia kupiga hatua, au tafuta mtu ambaye utaweza kuzungumza naye lakini hakikisha kila siku kuna jambo jipya ambalo unajifunza katika kukuza ufahamu wako.

Jambo la pili, Jaribu kila siku kujiuliza hivi ninasonga mbele au ninarudi nyuma kwa maneno mengine jaribu kujikagua na kujifanyia review yakuona kama unapiga hatua au haupigi hatua kwenye maisha yako, ukifanya mambo haya mawili kila siku yatakusaidia kutoka kwenye FIXED MINDSET kwenda kwenye GROWTH MINDSET.

Lakini siku zote hasara ya kuwa na FIXED MINDSET, ni kwamba utafanya mambo yale yale kwa namna ile ile bila kupata matokeo tofauti, wataalamu walisema kwamba kama utafanya jambo lile lile kwa namna ile ile utapata matokeo yale yale.

Kwa hiyo GROWTH MINDSET, inasema sijui kama ninavyotakiwa kujua kwa maneno mengine nipo tayari kujifunza, unapomzungumzia WARREN BUFFET, mtaalamu mkubwa kwenye mambo ya uwekezaji, unapomzungumzia  BILLGATE hao wote wana operate kwenye GROWTH MINDSET.

Wanajifunza jambo jipya kila siku wanasoma kitu kipya cha kuwakuza .

Je, LEO uko tayari kusoma kitu kipya ili kukuza ubongo wako?

KARIBU   UJIUNGE  SASA  " DARASA  LA   MAISHA  NA  MAFANIKIO "  ONLINE     ILI  UJIFUNZE  SIRI   ZA  MAISHA   NA   MAFANIKIO  KWA   MAPANA  NA  MAREFU

WASILIANA  NAMI    SASA    KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU

 ( WhatsApp  + 255 716924136 ) /  + 255 755 400128 /  + 255 688 361 539 

EMAIL : japhetmasatu@gmail.com

 

Saturday, June 26, 2021

JINSI YA KUPATA UTULIVU WA AKILI , TEKNOLOJIA IMEVURUGA AKILI ZA WATU WENGI.

Je, Ungependa Kupata Utulivu Wa Akili?

Wahenga waliwahi kusema“ Usipoziba Ufa Utajenga Ukuta”.

Hakuna anayeweza kubisha kwamba kumekuwa na ukuaji mkubwa sana wa teknolojia kwenye zama tunazoishi sasa.

Kuna maendeleo makubwa ambayo yametokea tangu kuanza kwa karne ya 21 ambayo hakuna aliyetegemea yangetokea kwa kasi kubwa hivyo.

Nani alidhani angeweza kuwasiliana na mtu aliye bara la mbali kwa kuonana uso kwa uso bila hata ya kutumia gharama kubwa?

Nani alifikiri vitabu vyote duniani vingeweza kuweka mtandaoni na ikawa rahisi mtu kuvipata na kuvisoma?

Nani alifikiri kungekuja simu za mkononi (simu janja) ambazo unaweza kuzitumia kufanya kila kitu kama unavyotumia kompyuta, kuanzia kuwasiliana, kutunza kumbukumbu, kupiga picha, kurekodi sauti na video, kuuza na kununua na hata kujifunza?

Haya ni maendeleo makubwa, ambayo mtu aliyefariki kwenye karne ya 20, akifufuliwa leo atashangaa mno kwa maendeleo haya na angetegemea kuona maisha ya watu yakiwa bora kutokana na maendeleo haya makubwa.

Lakini hapo ndipo atakaposhangazwa zaidi, kwani licha ya maendeleo makubwa ya teknolojia atakayokuwa ameyaona, atagundua maisha ya watu yako hovyo kuliko kipindi ambacho teknolojia hizo hazikuwepo.

Atashangaa kuona watu wakiwa wamechoka, wana msongo na hawana muda kabisa.

Atashangaa kuona watu wakitumia muda wao mwingi kwenye simu zao, kwa mambo ambayo hayana manufaa kwao.

Atashangaa jinsi watu wanaonena wivu kwa mambo ambayo wanayaweka kwenye mitandao ya kijamii.

Ujumbe atakaokuwa ameupata ni mmoja, kwamba teknolojia hizi mpya ambazo zina nguvu ya kufanya maisha ya wengi kuwa bora, zimegeuka kuwa gereza lililowafungia wengi na hawana tena uhuru wa kuyaishi maisha yao.

Ni dhahiri kwamba teknolojia mpya, hasa simu janja na mitandao ya kijamii, vimekuwa tatizo kubwa kwa wengi. Kila mtu analalamika jinsi vitu hivyo vinavyochukua muda mwingi, kuleta uchovu na hata msongo.

Wanaotengeneza na kuendesha teknolojia hizo hawajali kuhusu hilo, kwani kadiri unavyozitumia kwa muda mrefu, ndivyo wao wanavyopata faida. Hivyo wamejipanga kuhakikisha watumiaji wanaendelea kuwa wafungwa kwenye teknolojia hizo.

Na kwa kuwa teknolojia hizi ni mpya, hakuna mwenye uzoefu wa jinsi ya kukabiliana nazo, hivyo watu wanaingia kwenye teknolojia hizo mpya kwa kuhadaiwa watanufaika sana, lakini kinachotokea ni wanageuzwa kuwa wafungwa.


Leo nina habari njema mdau  wangu  , habari hizo ni kupatikana kwa mwongozo wa kuzitumia teknolojia hizi mpya vizuri na ukombozi wa ufungwa ambao teknolojia hizo zimetengeneza kwako.

Kupitia   " DARASA   ONLINE "   MAISHA  NA  MAFANIKIO utajifunza  jinsi  teknolojia mpya zinavyokufanya mtumwa na njia za kuondoka kwenye utumwa huo.

Mungu  akubariki  sana.

WASILIANA  NAMI  HARAKA  NIKUUNGE

 ( WhatsApp  + 255 716924136 ) /  + 255 755400 128  /  + 255 688 361539 / + 255

 

KWANINI WATU WENGI HAWANA FURAHA ??

Unajua Kwa Nini Wanakosa Furaha?

Ili uweze kufanikiwa kwenye malengo ambayo unayo ni lazima uwe mtu mwenye furaha.

Na wapo watu wengi sana ambao wamekosa furaha kwenye maisha yao na inawezekana hii imesababishwa na changamoto mtu anazozipitia mambo anayopitia, inawezekana ni changamoto za kifedha, changamoto za kimahusiano au ni changamoto za kiuongozi.

Lakini kuna jambo ambalo limenyang " anya furaha ya watu wengi sana.

Lakini kitu kimoja ambacho watu wengi sana ambacho hawakifahamu furaha huwa haianzii nje furaha huwa inaanzia ndani yako.

 Na kuna vitu ambavyo watu waliofanikiwa siku zote kuwa na furaha kwenye maisha yao, wamezingatia na wamevifanya siku zote.

Kuna mambo ukiyafahamu utakuwa na furaha kila siku bila kujali nini kinaendelea, bila kujali hauna nini na ndio mambo leo ninataka uyazingatie na kujifunza, ili uweze kuyatumia kama sehemu ya kujenga furaha yako inawezekana kabisa kuwa na furaha kila siku kwenye maisha yako.

Jambo a ambalo mwanasaikolojia leonard ambalo alilisema 1954, ili uwe na furaha usijilinganishe na watu wengine , yeye alitumia concept nzuri sana, upward comparison na downward comparison, kwamba kuna kujilinganisha kwa juu yako au kujilinganisha chini yako, kwa watu wengine wenye mitazamo chanya inawasaidia kama kutamani lakini wengi sana inakuwa kama inawakatisha tamaa, wanajiona kama wamechelewa wanasema kwa kweli najiona kama nimechelewa.

Maana kama Yule kafanikiwa kiwango kile kwa nini mimi sijafanikiwa kwenye hichi.

 Lakini wale wanaojilinganisha na wachini yao tunasema wao wanajiona kama wamefanikiwa sana, wakijilinganisha na wale watu ambao wapo chini yao.

Mwanasaikolojia leonard, anasema ukifanya ulinganifu wako na watu wengine itakupa shida sana kufanikiwa kwako, kwa sababu ukweli ni kwamba (“somebody ten chapter it can be your one chapter”).

Kwamba sura ya kumi ya mtu mwingine unayemwangalia kwako inawezekana ikawa ni sura ya kwanza kwenye kitabu chako, kwa maneno mengine unapojilinganisha unakuwa hujui kinachoendelea kwenye maisha ya mtu mwingine watu wengi kwa ajili ya kujilinganisha wamejikuta wamejikuta wameingia kwenye maisha yenye gharama kubwa sana, wamejikuta wanatumia vitu katika viwango vikubwa kuliko walivyokuwa wanatakiwa.  

Mtu anajilazimisha kufanya mambo yaliyo juu sana ya uwezo wao, kutokana tu na kujilinganisha.

Unachotakiwa kujua ni kwamba watu wengi hawakuonyeshi kitu kilichopo wanakuonyesha kitu wanachotaka wewe ukione.

Rudia ili uelewe vizuri, watu hawaonyeshi kitu kilichopo kwao wanakuonyesha kitu wanachotaka wewe ukione.

Kitakacho tokea ni nini? Wewe utakuwa unajilinganisha na kitu ambacho wanataka wewe ukione lakini hujui uhalisia wa mambo yaliyojificha, lakini ushawahi kukutana na hali au ukasikia kitu cha mtu ukasema aisee nilikuwa sijui kama jamaa ndivyo alivyo kumbe alikuwa anaigiza kumbe maisha yake hayakuwa hivyo, kwa hiyo usijilinganishe na watu wengine, watu wengi ambao wanajilinganisha nao, unawakuta wana struggle kwenye maisha yao, kuna mambo wanaendelea kustruggle kuyapata.

kwa hiyo focus kwenye kitu unachokifanya, focus kwenye maono yako, angali kitu unachopaswa kukifanya , angalia jinsi maisha yako wanavyopaswa kwenda, acha kujilinganisha utajikuta kwenye matatizo makubwa  sana kwenye maisha yako.

Nilishawahi kukutana na mtu mmoja, akawa ananiambia alikuwa na anajilinganisha sana, alikuwa anawatamani sana watu Fulani, lakini siyo kitu kibaya wapo watu ambao wanaishi vizuri lakini mwisho wa siku tunasema lazima urudi kwako wewe mwenyewe kwa sababu yeye mwenyewe anakuja kusema alichokuja kugundua baadae akawa anasema kwa kweli ningekuwa nawajua nisinge watamani wapo ki hivyo.

Kuna watu umekuwa unawatamani wanaendesha magari mazur, unatamani kujifunza vitu vizuri kutoka kwao lakini isifike sehemu ukawa unajiona wewe siyo kitu, hauna maana kwa sababu ya kujilinganisha sana na wengine kwa hiyo cha kwanza acha kujilinganisha badilisha kutoka kwenye kujilinganisha kwenda katika kujifunza, kujifunza alifanya nini akapata alichokipata, alifanya nini au alijifunza nini, au alipita njia gani ili na mimi niweze kupita.

Lakini mtu ambaye anajilinganisha ni Yule anayesema na mimi nataka kuwa kama Fulani bila kujifunza yaliyo nyuma yake.

Unaweza kuwa na FURAHA  kila siku kwa  kujiunga  na  " DARASA   ONLINE "  LA  MAISHA   NA  MAFANIKIO " ,kwawa sababu UTAJIFUNZA   hatua kwa hatua jinsi ya kujijengea tabia zinazoleta   FURAHA   NA   MAFANIKIO  katika  Maisha  yako.

 WASILIANA   NAMI   HARAKA   HUJACHELEWA.  ILI  NIKUUNGE ,  " MAARIFA  NI   NGUVU "

NA  KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU , DAR  E  SALAAM , TANZANIA

 ( WhatsApp  + 255  716 924 136 ) /    + 255 755 400 128 / + 0688  361  539 /  + 255 629 748  937

EMAIL :  japhetmasatu@gmail.com