Friday, September 26, 2014

ELIMU YA KUJITAMBUA

                              KUJITAMBUA    NI     NINI   ?
 
Neno    KUJITAMBUA    linatokana   na   neno    TAMBUA   lenye    maana   ya    KUJUA    UKWELI   WA   KITU   FULANI   KWA    KINA ,  kwahiyo    KUJITAMBUA   ni  hali   ya    KUJIJUA   VILIVYO  KWA    KINA .  Ingawa    watu   wengi   sana   WANAISHI   lakini  HAWAJITAMBUI   KWA   KINA.


HUWEZI  kuwa    MJASIRIAMALI    mwenye     MAFANIKIO  bila   ya   KUJITAMBUA.  Wakati  huo  huo   HUWEZI   KUJITAMBUA   BILA   KUMJUA   MUNGU.

                         JIULIZE    MASWALI   HAYA :--
{1}.  Kwanini  Ulizaliwa  ?
{2}.Umekuja   hapa   duniani   kufanya   nini  ?
{3}.Umetokea   wapi   na   unaenda   wapi  ?

AMINI   USIAMINI   MATAJIRI   (  Watu   wenye   MAFANIKIO ) duniani  kote   wanajua  kwanini   walizaliwa   ?  Kwa   nini    Wanaishi  lakini    pia    wanajua   wanakokwenda.

Kwahiyo   ili   UFANIKIWE   ni    lazima     UJUE    UMETOKA   WAPI ?   NA   UNAKWENDA   WAPI ?  NA   KWANINI   UPO   HAPA   DUNIANI ?

Katika   MAISHA    YA    MAFANIKIO   ni    lazima    SIO   OMBI   kuwa   ili     Uweze   KUFANIKIWA   katika   kiwango   kikubwa   ni     lazima   uwe    umeyapata   majibu   ya    maswali   ya  hapo  juu.  

No comments:

Post a Comment