Friday, September 12, 2014

EWE MWANAFUNZI / KIJANA ISHINDE NAFSI YAKO.

UWEZO  WETU   wa    KUFANIKIWA   katika   Safari   yetu   ndefu   ya   MAISHA   hautegemei  uwezo  wa    AKILI  peke  yake.
     
Tunapofikiria   kuhusu  UWEZO   WA   MTU  hatuna    budi    kujumuisha   pia    UTASHI   WAKE. Kama   mtu ameshindwa  kuishinda    NAFSI  yake  na    kuamua   kuchukua  NJIA  RAHISI  bila  shaka  UWEZO  wake   kamili  utakuwa   pia    UMEPUNGUZWA  SANA.

UNAPOKUWA   SHULENI    utagundua  ya   kwamba  kuna  aina  mbili {2} za    WANAFUNZI :-
      AINA  YA   KWANZA  ni  wale   ambao  hawana  UWEZO    SANA  KIAKILI  lakini  hujitahidi   sana   SHULENI  ili   wahitimu   wakiwa  wamefanya   vizuri  katika   MASOMO   YOTE.
       AINA   YA   PILI   ni    wale    wenye    AKILI    NYINGI     lakini     hupenda    STAREHE  na  katika   MUDA  wao  wote   chuoni   huwa   hawana  nafasi    hata   ya   kufungua   kitabu.
        HUYU wa   pili   angesema   " yule   MBUKUZI  maefaulu    Vizuri ,  lakini    kama   ningekuwa  nimesoma   kama   yeye ,   ASINGEWEZA   KUNISHINDA  AU   ASINGEWEZA   KUFUA   DAFU   KWANGU ".
     BAADA  ya   kuhitimu , yule   mpenda   starehe  anakutana  na   rafiki   yake    mwingine    mwenye   MAFANIKIO    katika   biashara , na    kusema   "  HAKUWA   NA   AKILI   SHULENI. ALAMA  ZANGU   ZILIKUWA   NZURI   KULIKO  ZAKE "  akimaanisha  kwamba  kama    YEYE   angekuwa   ndiye   mwenye   BIASHARA ile   bila    shaka  angekuwa    AMEFANYA   VIZURI  ZAIDI.
  JE, LAKINI   HUO   NDIO  UKWELI   WENYEWE  ?Kujisomea   sana   ni   kuishinda  ILE  SEHEMU  MOJA  YA   NAFSI  YAKO   INAYOTAMANI   STAREHE   ZILIZOPO-----KUJINYIMA  SHEREHE  NA  HATA  KUTAZAMA  RUNINGA.  BILA   SHAKA  PIA  RAFIKI  ALIYEFANIKIWA  AMEJINYIMA   MAMBO  HAYO. 

        ILIMBIDI  AJIZUIE   NA  TAMAA  ZA  STAREHE  NA   KUUTUMIA  MUDA  WAKE   WOTE KWENYE    SHUGHULI  ZAKE.  INAHITAJI   UAMUZI   MKUBWA  ILI   KUISHINDA  NAFSI .

No comments:

Post a Comment