Saturday, September 28, 2019

KOSA KUBWA UNALOFANYA KWENYE MSHAHARA WAKO UNAOPOKEA KILA MWEZI

Kwa mshahara au kipato chochote unachopokea, iwe ni malipo ya kazi zako binafsi au faida unayotengeneza kwenye biashara, kuna kosa moja kubwa umekuwa unalifanya. Kosa hilo ni KUMLIPA KILA MTU NA KUJISAHAU WEWE MWENYEWE.

Hebu fikiria unapopata fedha unaanza na nini? Kulipa madeni, kulipa bili, kununua vyakula, kununua nguo, kulipia starehe na mapumziko mbalimbali. Baada ya siku chache za kupata fedha unakuwa umeimaliza yote, huku wewe ukibaki mtupu kabisa.
Sasa rafiki, jua kwamba huwezi kuwa huru kifedha kama utaendekeza utaratibu huo wa kuwalipa wengine na kujisahau wewe mwenyewe. Kwenye kila kipato unachoingiza, mtu wa kwanza kumlipa unapaswa kuwa wewe.

Monday, September 23, 2019

UWEZO WA KUJUA KAMA TUTAKUFA MASKINI TUNAO ----------NA MUNGA TEHENAN

TUNA UWEZO MKUBWA TUNAOSHINDWA KUUTUMIA-----------NA MUNGA TEHENAN

PIGA HATUA MOJA KWA WAKATI---ISHI KWA MUJIBU WA KANUNI YA MAFANIKIO----------NA DR. KAZUO INAMORI

MAZUNGUMZO NA DR . KAZUO INAMORI KUHUSU KANUNI YA USHINDI

A Simple System To Transform Any Business From A Cash-Eating Monster To A Money-Making Machine

MSHAHARA NI MADAWA YA KULEVYA , JIFUNZE JINSI YA KUEPUKANA NA MADHARA YAKE


Nassim Taleb anatuambia kuna vitu vitatu vyenye uraibu mbaya, madawa ya kulevya(unga), vyakula vya wanga (sukari) na mshahara wa kila mwezi. 

Ukishauzoea mshahara, ni vigumu sana kuweza kufanya kitu kikubwa kwenye maisha yako. Kwa sababu maisha yako yanakuwa ya mipango ya mwisho wa mwezi tu. Kwamba mwisho wa mwezi huu nitafanya hiki au kile.
Mshahara ukitoka unakuwa na mipangilio mingi kuliko kiwango chake, hivyo ndani ya siku mbili unakuwa umeisha. Na hapo unafanya nini? Unajua vyema, unaanza kukopa kwa sababu unajua mshahara ujao utalipa. Na hapo ndipo uraibu unapojenga mizizi.
Kuondokana na uraibu huu wa mshahara, lazima uanze kujijengea msingi wa kipato nje ya mshahara. 

 TEMBELEA BLOGS   ZA   MWL.   JAPHET   MASATU , JIFUNZE   ,  JIUNGE   NA   DARASA  LA   MAFUNZO  KILA   SIKU   NA  UCHUKUE HATUA , MAISHA   NA  WEWE !



Tuwasiliane  kwa  Call / Message /  ( WhatsApp + 255716924136 )/   + 255 755 400128  /   +255 688 361 539

Saturday, September 14, 2019

KWA NINI BAADHI YA BINADAMU NI WABUNIFU NA WENGINE SI WABUNIFU ? -------------------" Fursa Afrika Mashariki Blog "

TUWE WABUNIFU KWA KIWANGO GANI ? -------------------------- " Fursa Afrika Mashariki Blog "

VIRUTUBISHO 04 VINAVYOHITAJIKA KWENYE UBUNIFU -------------------" Fursa Afrika Mashariki Blog "

KWA NINI WASTAAFU WENGI HUFELI KWENYE BIASHARA ? JINSI YA KUFANYA BIASHARA BAADA YA KUSTAAFU.---------------------" Fursa Afrika Mashariki Blog "

KUACHA WOSIA NA MIPANGO YA MALI ZAKO BAADA YA KIFO CHAKO -----------------" Fursa Afrika Mashariki Blog "

Friday, September 13, 2019

MIPANGO YA MAISHA INAPASWA KUJA KABLA YA MIPANGO YA BIASHARA.

Ni rahisi sana kuweka malengo na mipango mikubwa ya kibiashara, lakini unapokaa na kujiuliza kwa nini unataka kufikia malengo hayo makubwa unakosa jibu la uhakika.

Watu wengi wamekuwa wanapotea kwenye biashara kwa sababu wanaweka malengo ya biashara kabla hawajaweka malengo ya maisha. Wanataka kuwa mabilionea kupitia biashara zao, na hilo linawataka kuweka maisha yao yote kwenye biashara na kusahau vitu vingine vyote. Wanaweza kufikia lengo hilo, lakini maeneo mengine ya maisha yao kama afya na mahusiano yanakuwa yameathirika sana.

Kabla hujaweka lengo kubwa la biashara, anza kwanza na lengo kuu la maisha yako. Jua unataka kuwa na maisha ya aina gani, jua maisha ya mafanikio kwa upande wako yana maana gani.

Ukishajua kwamba unataka nini kwenye maisha yako, hapo sasa unaweza kuitumia biashara yako kuwa na maisha unayoyataka wewe. Lakini ukianza kufikiria unachotaka kwenye biashara pekee, utaishia kuwa na maisha mabovu sana.

SHERIA 10 ZA BIASHARA ZA KUFUATA ILI UFANIKIWE SANA , UKIZIVUNJA SHERIA HIZI HUTAFANIKIWA ---------------------------- " Fursa Afrika Mashariki Blog "

FURSA YA BIASHARA YA KUFUNGUA MAKAMBI --------------------- "Fursa Afrika Mashariki Blog "

Monday, September 2, 2019

HATUA 05 ZA KUCHUKUA ILI KUTOKA KWENYE AJIRA MPAKA KUJIAJIRI ----------------- " Fursa Afrika Mashariki Blog "

MAMBO 20 YA KUFANYIA KAZI ILI KUTOKA KWENYE AJIRA NA MADENI NA KWENDA KUJIAJRI NA KUWA NA UHURU WA KIFEDHA--------------------- " Fursa Afrika Mashariki Blog "

UNAPOJIAJRI , UNAPASWA KUFIKIRI TOFAUTI NA WALE WALIOAJIRIWA.

Unapojiajiri, unapaswa kufikiri tofauti kabisa na wale walioajiriwa. Kwa sababu kuna vitu ambavyo watu walioajiriwa hawajisumbui navyo sana, kwa sababu wameahidiwa vinafanyiwa kazi, mfano bima ya afya, mafao ya uzeeni na mengineyo. Unapoachana na ajira na kuamua kujiajiri moja kwa moja, mambo hayo utapaswa kuyahangaikia mwenyewe, lazima utafute bima yako na familia yako na pia lazima uwekeze ili kujiandaa kwa siku zijazo. Kwa sababu hakuna anayekuandalia mafao, unapaswa kutengeneza uwekezaji wako mwenyewe, ambao miaka mingi ijayo utaweza kukuingizia wewe kipato hata kama hufanyi kazi moja kwa moja.