Tuesday, September 29, 2015

FURAHA KATIKA MAISHA.



MWANADAMU   mara  nyingi  amekuwa   akifanya  makosa  kwa   kudhani   FURAHA  ndiyo  hitaji    muhimu    sana   katika   MAISHA , badala  ya   KUFAHAMU    jinsi  ya   KUTAWALA  MAISHA.
      Ni   vigumu   kueleza   maana   ya   FURAHA   kwani   ni  zawadi    muhimu  kwa   kila  mtu. Huepuka    uchambuzi   wa   mwanasayansi , sawa  na    inavyoepuka     maelezo    ya   MWANAFALSAFA.
       Kila   siku    FURAHA   huwa   ni   jambo   la  ziada   ambalo    huongezwa   kwenye   MAISHA , ni   kama   sukari   inavyoongezwa   kwenye      maisha  mazuri , ni  tuzo    inayotolewa  kutokana   na   juhudi   kubwa.
       Si   maumbile. Mtu   mwenye  afya  nzuri  ambaye  pia  ana   maumbile  mazuri  , anaweza  asiwe   ameridhika   na   kasha   kukosa   FURAHA   ambako    kunaweza   kutokana    na   mashambulizi   ya    matatizo.
       Kuwa   na  afya   nzuri   haimaanishi   uhakika   wa   kuwa    na   FURAHA. Kinyume  na   hivyo , hata   wakati  mtu   ni  mgonjwa  au   wakati    mazingira   kwa   nguvu   zote   hujikusanya   na    kumwangamiza  mtu , bado  anaweza   akaifahamu   FURAHA.
      FURAHA   si   kumiliki , tunaweza  kumiliki   ulimwengu  wote , lakini   tukakosa   FURAHA  kabisa. Haipatikani    katika  MAFANIKIO , kwani  unaweza   kufikia  MALENGO  yako  yote , lakini  ukakosa  FURAHA. Unaweza   kupata  UMAARUFU , BAHATI , na   MAFANIKIO , bado  unaweza  ukapungukiwa  zawadi  ya   FURAHA.
       Si  matatizo   yanayowafanya  watu   wasiwe  na  FURAHA , mtu   anaweza   kuangalia   jinsi    matumaini  na   matakwa   yake  yalivyokosa   MAFANIKIO , bado   moyoni  akawa  na  FURAHA.
       FURAHA  NI NINI ?  FURAHA  ni  hali   ya  mtu.Si  jambo ambalo linatokea , ila  ni   majibu   ya  kile  kinachotokea   yanayoonesha  kiasi  cha  FURAHA au  HUZUNI. MAZINGIRA  hayana   uwezo  wa   kuharibu  utulivu  wa  mawazo  yetu , ila  kama   tunayaruhusu.
 MATUKIO  ni   mambo   ya nje. FURAHA   ni  jambo  la   kiundani.Si   kitu   kinachotokea  pekee ,  bali   ni   majibu  ya  tukio   fulani  la  kiundani.
 FURAHA  ni  likizo  ya  mawazo ,  burudiko  la  moyo  au  roho.Ni  UHURU  WA  MAISHA   usio  na  bei. Haina  kitu  kinachoweza  kufidiwa  badala  yake. Malipo   yote  ambayo   mwanadamu    huyatafuta   ni  njia   tu   ya  mwisho  huo.

Makala  hii  imeandikwa  na  MWL   JAPHET   MASATU ,  anapatikana  kwa   EMAIL , japhetmasatu@yahoo.com.   Mobile : + 255 716 92 4136   WhatsApp  + 255 755 400 128.