Friday, May 29, 2015

SIRI ZA MAFANIKIO KATIKA BIASHARA



   MAFANIKIO  KATIKA   BIASHARA
Wafanyabiahara   walioanza      biashara   ndogo   na  kupata   mafanikio   makubwa   wamekuwa    watu  wasiokatishwa  tamaa  wala   kurudishwa   nyuma  na  vikwazo. Badala   yake  wamekuwa   wakitumia  MBINU  zifuatazo  kupambana  navyo :
KIKWAZO  I :  MITAJI  YA  KUFANYIA  BIASHARA. 
MBINU  ZITUMIWAZO  NA  WALE   WALIOPATA  MAFANIKIO
{1}. Kuanza  biashara  ambazo   hazihitaji   mitaji    mikubwa.
{2}. Kutegemea   mali    kauli   na   kujenga   uaminifu  wa  hali   ya  juu  katika  kuilipia.
{3}.Kukopa    kutoka  taasisi   zinazotoa   mikopo  midogomidogo { MFIs }
{4}.Kukopa  na    kurudisha  fedha   haraka  ili   kuweza   kupata   mikopo   mikubwa  zaidi  mapema
{5}. Kukopa   kwa  jamaa , marafiki  ambao  wanawaamini
{6}. Kuwa   na  mahusiano  ya  karibu  na benki  kila   wakati  na  kuhakikisha  wanafahamu  maendeleo    ya  biashara  zao  ili  wakienda   kukopa  wasiwe  wageni.
{7}. Kukopa  benki  wakati  ambao  hali   ya  fedha  ni nzuri  na  kurejesha   mara  kadhaa  ii  kujijengea  rekodi   nzuri.

KIKWAZO  II:  KUPATA    MASOKO
MBINU  ZITUMIWAZO NA  WALE   WALIOPATA   MAFANIKIO
{8}.Kuhakikisha  kuwa  wanaridhisha  wateja   kwa   gharama  yoyote ,  mfano  mnunuzi  asiporidhika  na  nguo   aliyoshonewa anashonewa   nyingine.
  




{9}.Kuajiri  wafanyakazi hodari  sana  katika  utoaji   huduma  na   kuwapa  mishahara na   mazingira    mazuri   ya  kazi
{10}. Kutangaza  biashara  kwa  njia ambazo  hazigharimu  sana , mfano  kutuma  salamu kutoka   kwenye  biashara  kwa  njia  ya  redio / postcard.

KIKWAZO  III :  KUPATA  USHIRIKANO  WA  MUME  /  MKE
MBINU  ZITUMIWAZO  NA  WALE  WALIOPATA    MAFANIKIO
{11}.Kuwa   muwazi  na   mkweli, na   kuhakikisha   kuwa   mume / mke  anafahamu  kila  anachofanya.
{12}.Kukwepa  kuonyesha  dalili  zozote  za  dharau  kwa  mume / mke.
{13}.Wengine  wameamua  makusudi  kabisa  wenzi   wao   wa  ndoa   wasijihusishe  katika  biashara  zao  ,  kwa  kuwa   dira  na  tabia  zao  katika  uendeshaji  biashara  ni  tofauti    mno.

KIKWAZO  IV :  KUCHANGANYA    MAJUKUMU  YA  ULEZI  NA  BIASHARA
MBINU  ZITUMIWAZO  NA  WALE   WALIOPATA    MAFANIKIO
{14}.Kuwaonyesha  watoto  kazi  wanazofanya ,  ili  awapo  kazini  wawe    wanaelewa  kinachoendelea
{15}. Kucgagua   shughuli   moja  au  chache  ili   kuweza  kumudu    na   majukumu  ya  nyumbani.

KIKWAZO  V :  RUSHWA  NA  USUMBUFU  WA   MAOFISA  WA  SERIKALI
MBINU  ZITUMIWAZO  NA  WALE   WALIOPATA   MAFANIKIO
[16}.Kutokubali   kuwa  legelege  wanapoona   wanaonewa.
{17}.Kuweka  kumbukumbu  vizuri ,  na   kuzitumia  kubishana  na  maofisa  wa  kodi.
{18}.Kutumia    wataalam  kuandaa  mahesabu  ya  biashara ,  na  kuyatumia   kuonyesha   kodi  wanayopaswa     kulipa.


Makala  hii  imeandikwa    na  MWL  JAPHET    MASATU   + 255  716  924136   /   + 255  755   400 128