Thursday, April 22, 2021

FALSAFA : SOMA VITABU , JUA FALSAFA ILA WEKEZA NGUVU NYINGI KUISHI KILE ULICHOSOMA.

Soma Vitabu, Jua Falsafa Ila Wekeza Nguvu Nyingi Kuishi Kile Ulichosoma

UNASUMBUKA NA UFANISI KAZINI ??

Leo nimeamua nikusogezee mada hii kwenye macho yako kwani imekuwa changamoto na kuathiri utendaji kazi wa watu wengi.

 Ukweli ni kwamba akili zetu sisi binadamu ni kitu cha ajabu sana, ni kitu ambacho kina nguvu ya kufanya makubwa kuliko tunavyoweza kutegemea.

Lakini cha kushangaza ni kwamba, mtu anaweza kuitawala akili yake akafanya makubwa, au akatawaliwa na akili yake na kuwa mtumwa maisha yake yote.

kuhusu ubongo wa binadamu ni kwamba una nguvu za ajabu lakini watu wengi hutumia sehemu ndogo sana ya nguvu hiyo.

Asilimia kubwa ya watu huishia kufanya mambo ya kawaida, hivyo hupata matokeo kawaida na kuishi maisha ya kawaida (routine life).

Lakini kundi lingine ni watu ambao ni asilimia ndogo ambao hufikia viwango vya juu vya ufanisi/ nguvu za ubongo wao.

Kundi hili hufanya mambo makubwa na huwa na maisha tofauti na kundi la kwanza.

Tofauti ipo kwenye namna tunavyotumia bongo zetu, uamuzi upo mikononi mwako.

Ujenge au ubomoe.

Uzuri mpaka hapa umeshajua upo kundi gani.

Kama tayari tuendelee…

Ubongo wetu unaweza kutunza taarifa  mbalimbali kwa muda,  ambazo baadae huenda kwenye subconscious mind.

Ili taarifa zivuke kwenye subconscious mind, hupita kwenye mfumo RAS ( Recuticular Activating System) ambapo taarifa huchujwa.

Ili kundi lingine huruhusu vitu vya kimazingira kuingia ambavyo huathiri maamuzi na kisha utendaji.

Kwa bahati mbaya huwezi kufikia viwango vya juu vya ufanisi ikiwa muda mwingi umezungukwa na usumbufu.

Hivyo unapaswa uwe na ufahamu juu ya vitu gani vinavyokuletea usumbufu na kuweza kuvidhibiti mara moja.

Kuna maelfu ya watu walipitia hali kama hii na wakafanikiwa kutoka mimi ni miongoni mwao, hata wewe leo hii unaweza kutoka kwenye hali hii.

Friday, April 16, 2021

USHAURI : KAMA HUWEZI KUFANYA KITU HIKI , FUNGA BIASHARA YAKO MARA MOJA.

Karibu rafiki yangu mpendwa kwenye makala yetu ya ushauri wa changamoto mbalimbali zinazokuwa kikwazo kwa mafanikio yetu.

Kwenye makala ya leo tunakwenda kushauriana kwenye msimamo muhimu mno unaouwezesha biashara kufanikiwa au kufa. Msimamo huo ni misingi ambayo biashara inafuata bila ya kuivunja.

Kila biashara inapaswa kuwa na misingi au miiko yake, ambayo walio ndani na nje ya biashara wanapaswa kuifuata bila ya kuivunja. Walio ndani ya biashara ni wamiliki na wafanyakazi na walio nje ni wateja na wadau mbalimbali wa biashara.




Pale mtu yeyote anapovunja misingi muhimu ambayo biashara hiyo imejengwa basi anapaswa kuondolewa kwenye biashara hiyo. Kwa sababu kama anayevunja misingi ataendelea kuachwa kwenye biashara, biashara hiyo itakuwa dhaifu na kufa.

Hapa ndipo changamoto za biashara nyingi zinapoanzia, watu wanavunja misingi na miiko ya biashara, lakini bado wanaachwa kwenye biashara. Wanaachwa kwa sababu mmiliki wa biashara anaona biashara yake haiwezi kwenda kama atawaondoa watu hao.

Na hapa ndipo ninapokupa kauli hii moja muhimu unayopaswa kuitafakari kila wakati; kama umeanzisha biashara yako binafsi na unashindwa kumfukuza mtu aliyendani (mfanyakazi au mbia) au nje (mteja au mdau) ya biashara basi funga biashara hiyo mara moja. Ifunge kwa sababu unachofanya ni kupoteza muda tu, kama biashara hiyo haina cha kusimamia itaangushwa na chochote.

Kama biashara haiwezi kwenda bila kuwategemea wasioheshimu misingi na miiko ya biashara hiyo, hapo huna biashara, ni swala la muda tu kabla haijafa kabisa.

Kwenye riwaya ya Fountainhead iliyoandikwa na Ayn Rand ambapo Howard Roark anapambana na wajamaa wanaotaka kutumia kipaji chake na kumdhibiti watakavyo, kuna kisa kimoja kinaeleza vyema hili ninaloshauri hapa. Gail Wynand mmoja kati ya wachache waliokuwa wanamuunga mkono Howard alikuwa anamiliki magazeti yenye ushawishi mkubwa. Ellsworth Toohey aliyekuwa anampinga sana Howard alikuwa mmoja wa waandishi na wahariri wa magazeti hayo. Toohey alipanga kuyatumia magazeti ya Wynand kumchafua Howard, kitu ambacho Wynand alikikataa.

Hivyo Toohey alitumia ujanja, wakati ambapo Wynand hayupo, aliajiri wafanyakazi wengi wanaokubaliana na wewe, akashawishi bodi ya wakurugenzi iwe upande wake na hapo akawa amepata udhibiti mkubwa wa magazeti hayo.

Baada ya kujihakikishia udhibiti wa magazeti, alianza kumchafua Howard kupitia magazeti hayo. Wynand aliporudi hakupendezwa na hilo, alimuita Toohey ofisini kwake na hapo Toohey akamwambia wazi kwamba kwa sasa yeye ndiye mwenye udhibiti wa magazeti hayo na hawezi kumfukuza. Wynand alimjibu kwa ufupi; siku ambayo nitashindwa kumfukuza mfanyakazi niliyemuajiri kwenye biashara yangu, ndiyo siku nitakayoifunga hiyo biashara kabisa. Na kweli ilimbidi Wynand kufunga magazeti yake maana Toohey alikuwa ameshakita mizizi.

Kuna mengi sana ya kujifunza kwenye kisa hicho na ushauri huu kwa ujumla. Lazima biashara iwe na misimamo na miiko na yeyote anayeivunja hapaswi kuachwa. Na kama kuondolewa kwake hakuwezekani, basi bora biashara ifungwe.

Kingine muhimu cha kujifunza ni umuhimu wa biashara kuendeshwa kwa mfumo ambapo hakuna mtu mmoja ambaye asipokuwepo basi biashara inakuwa imekufa. Hata wewe mmiliki wa biashara, lazima biashara iweze kwenda bila uwepo wako, la sivyo huna biashara.

Hatua za kuchukua hapa ni kujenga mfumo imara wa biashara yako ambao una misingi, miiko na miongozo ya jinsi ya kuendesha biashara hiyo. Kila anayehusika kwenye biashara anapaswa kuuelewa vizuri mfumo huo na kuufuata. Na pale inapotokea mtu anakwenda kinyume na mfumo basi anapaswa kuondolewa mara moja. Na kama unaona huwezi kumwondoa kwa kuwa biashara haiwezi kwenda, basi bora ufunge biashara moja kwa moja.

JIUNGE   leo  DARASA  ONLINE " ili uweze  KUJIFUNZA   MISINGI  NA  MIIKO   YA  BIASHARA   kujenga biashara imara na isiyotikiswa na kitu chochote. Wasiliana  NAMI   KOCHA   MWL.  JAPHET  MASATU (  WhatsApp + 255 716924136  ) NIKUUNGE   LEO.

Makala hii imeandikwa na Kocha Mwl  Japhet   Masatu  ambaye ni MWALIMU   KITAALUMA, kocha wa mafanikio, mwandiashi na mjasiriamali. 

 

KAMA UNATAKA KUVUNJA TABIA FULANI AU URAIBU , USIJIRUHUSU KUWA KWENYE HALI HII YA KUFANYA KWA MAZOEA.

Siku moja mwandishi wa vitabu Tom Corley alifanya utafiti wa tabia za kila siku za matajiri 233 na pia akachunguza tabia za kila siku za watu maskini wapatao 128.

Alichogundua ni kuwa kulikuwa kuna tofauti kubwa sana kati ya tabia za maskini na matajiri.  

Katika kipindi cha utafiti wake aligundua kuna karibu mambo 300 ambayo hutofautisha wanaofanikiwa na wale ambao hawafanikiwi maishani.

Mara nyingi ni rahisi sana kufikiri kuwa tofauti ya waliofanikiwa na wasiofanikiwa hutokana na mambo makubwa sana yanayotutofautisha.

Ukweli ni kwamba tabia ina nguvu kubwa ya kuamua hatima yako ufanikiwe au ufeli.

Tabia za kitajiri ni ngumu kuzijenga na ni rahisi kuzivunja, upande wa pili ni kinyume chake tabia za kimaskini  ni rahisi kuzijenga na ni ngumu kuziacha.  

Na hii ni kwa sababu Ujengaji wa tabia huwa unaanzia kwenye akili zetu, hivyo hata kuzivunja lazima kuanzie kwenye akili zetu pia.

Huwa tunaijenga tabia kwa kutumia nguvu ya kufikiri lakini tabia ikishajijenga huwa tunaitekeleza bila hata ya kufikiri(mindless).

Chukua mfano mdogo wakati unajifunza kuendesha baiskeli au gari.

Mwanzoni ulikuwa unafikiria kila unachofanya , hukuweza hata kuongea na mtu wakati unaendesha, maana kila wakati ulikuwa unafikiri kuchochea au kukanyaga mafuta, breki na kubadili gia.

Lakini baada ya kuwa dereva mzoefu, unajikuta unaendesha bila hata ya kufikiria , tena unaweza kuendesha huku ukiwa unaongea na wengine.

Mfano huo unatuonesha jinsi akili zetu zinavyojenga tabia , mwanzo tunatumia nguvu na umakini mkubwa kwenye kufikiri lakini baadaye tunaifanya bila hata ya kufikiri.

Ni hiyo hali ya kufanya bila ya kufikiri ndiyo inayojenga na kufanya uraibu uwe mgumu kuvunja.

Wengi wenye uraibu huwa wanajikuta wameshafanya kile walichozoea bila hata ya kufikiri.

Kwenye teknolojia na mitandao ya kijamii ndivyo pia uraibu unajengeka.

Awali wakati unaanza kujifunza kutumia simu janja au mitandao ya kijamii ulikuwa unatumia nguvu na kufikiri.

 Ila baadae inakuwa rahisi kwako , unajikuta umeshika simu na uko kwenye mitandao ya kijamii bila hata ya kufikiria.

Ili tuweze kuvunja uraibu huu na wa aina nyingine , tunapaswa kutumia akili zetu vizuri, kama zilivyotuwezesha kujenga tabia, hivyo pia zitatuwezesha kuvunja tabia na uraibu.

Kama unataka kuvunja tabia za kimaskini ambazo zinakupotezea muda na zina kurudisha nyuma na huzipendi, huna budi kutumia uwepo wa akili (mindful) , mbinu hii itakusaidia sana kuvunja tabia nyingi mbaya.

Hii ni mbinu ambayo imenisaidia mimi na maelfu ya watu

KARIBU  UJIUNGE   DARASA  ONLINE   UJIFUNZE ZAIDI

 WASILIANA  NAMI--KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU

WhatsApp + 255 716924136  /   + 255 755  400  128

Saturday, April 3, 2021

JIANDAE KILA SIKU KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ILI UKOMAE KIAKILI NA KIHISIA.

Kitu kimoja ambacho watu wengi hatuandaliwi mapema kufahamu basi ni kuambiwa ukweli wa maisha. Ukweli wa maisha ni kuwa maisha yatakuwa na changamoto siku zote. Changamoto hizi hazitaondoka hata tukifanikiwa kwa baadhi ya mambo tutakayo. Tutakapofanikiwa basi tutakutana na muundo mwingine wa changamoto.

Unaweza kutamani maisha yasingekuwa na changamoto ili yawe mazuri, imara au maana. Ila ukiangalia kwa kina uwepo wa changamoto ndio uletao ladha nzuri ya maisha, ndio unaofanya uzalishe wabunifu, wagunduzi na wanafalsafa. Changamoto zimefanya turejee ndani yetu na tugundue tuna uwezo mkubwa ambao tunapotumia tunavuka na kutatua hali mbalimbali ambazo zinajitokeza tunapoendelea kuishi.

Usipokuwa imara kihisia katika zama tunazoishi basi matukio yanayoendelea kutokea maishani yatakudhoofisha, yatakunyima furaha na yakufanya uishi na wasiwasi wakati wote. Ukomavu wa kihisia ni uwezo wa namna usivyoweza kutetereka na chochote kinachotokea maana unakuwa umejiandaa kuwa hata mabaya ni sehemu ya maisha, magumu ni njia ya maisha na changamoto ni fursa ya kukua na kukomaa. Watu wengi wasojiandaa kwa lolote kutokea ni rahisi hisia zao kuumizwa.

Kadri unavyoweza kukabiliana na changamoto na kuzivuka ndani yako unajenga utulivu, nguvu, uimara na ukomavu. Mtu ambaye anapitia changamoto nyingi ni mtu aliye imara kuliko mtu ambaye hapitii magumu au changamoto zozote. Uzuri wa changamoto ni kuwa unamsaidia mtu kutumia akili, kustahimili na kujituma ili avuke hapo. Kupitia mchakato wote wa kukabiliana na changamoto basi mtu anajenga uzoefu, hekima, ujuzi na uimara wa kukabiliana na changamoto nyingine mpya.

Simama imara katika wakati ambao maisha yatakutana na changamoto. Huu ni wakati ambao unapaswa kuwa tayari kukabiliana na changamoto ili zikusaidie ukomae, ukue na uwe imara zaidi kwa ajili ya changamoto nyingine mpya zitakazojitokeza maishani.

NA  KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU , DAR  ES  SALAAM

WhatsApp + 255  716 924136 /    + 255  755  400128


 

Friday, April 2, 2021

WEWE NI WA PEKEE SANA , ISHI UHALISIA WAKO.

Falsafa ya Ustoa inatualika sote kuishi kulingana na asili yetu. Kuogopa, kutokujiamini, kutojikubali ni mambo ambayo falsafa haiyaruhusu yawe ndani ya mtu anayetaka kuishi uhalisia wake alivyo. Kutojiamini ni zao la kutokujikubali. Maisha ya kijasiri huzaliwa pale ambapo mtu anatambua namna ana nguvu, kujikubali kupitia vipawa vyake, vipaji vyake na kuwa tayari kuishi bila kupepesa macho yoyote yale akiiga maisha ya watu wengine. Ukiiga maisha ya watu wengine ni kujivua uhalisia wako na huwezi kukutana na utoshelevu wa kile unachokifanya.

Wengi wanaogopa kuruhusu kuishi vipawa, vipaji vyao, ujuzi wao na msukumo wowote ule wenye tija kuonesha dunia. Hofu imekuwa kikwazo kwa wengi wakiona wakiishi au kuonesha uwezo walionao kwa watu wanaowazunguka watavunjwa moyo. Watakatazwa, watasemwa au kuchekwa.

Katika maisha yangu ya kujifunza, kuandika, kusoma vitabu na kutunga mashairi sijawahi kupata ukinzani wowote toka kwa wazazi wangu. Wao walikuwa watu wa kwanza kunikubali kuwa nimeamua kuishi maisha hayo. Hili limeacha alama kubwa sana maishani kuishi au kutoogopa kujifunza, kuandika na kutunga mashairi sehemu yoyote ile maana naona kufanya hili napata utoshelevu mkubwa ndani yangu.

Watu wote wenye ushawishi mkubwa duniani wametokana na wao kuishi kwa uhalisia, wamejikubali kuwa wao kama wao na kwa njia hiyo imewatengeneza wawe watu wenye nguvu katika maeneo ya taaluma zao, vipaji, biashara, mahusiano na uongozi. Unapoishi ishi kulingana na kitu kilivyopaswa kuishi moja kwa moja nishati au nguvu huzalishwa.

Jitoe na idhihirishie Dunia kuwa una kitu ndani yako cha tofauti ambacho upo tayari kukionesha, kutoa, kuchangia dunia iwe bora kuliko vile ulivyoikuta. Wale wanaojitoa, wanaotoa mchango wao mkubwa ndio wenye kufikia njia ya kuona ni watoshelevu ndani yao. Kubali kuwa halisi, kubali kuvipa vitu ulivyonavyo thamani na kuwa tayari kuishi bila kujibakiza. Maisha haya yana maana kubwa kuliko maisha ya kujikimbia uhalisia wako, au kuviacha vipaji vyako bila kutumiwa. Tumia vyote ulivyojaliwa kuifanya dunia sehemu salama ya kuishi.

NA  KOCHA  MWL.  JAPHET  MASATU , DAR  ES  SALAAM.

WhatsApp + 255 716 924136 / + 255 755 400128 /   + 255 688 361 539

 

WATENGENEZA NJIA NI WACHACHE , KUNAMTAKA MTU AMBAYE AMEVUKA UBINAFSI , WATAZAMAJI NI WENGI.

Kutengeneza njia kwataka moyo kweli pale ambapo unapotengeneza njia inayosaidia wengine nao kupita kupitia wewe. Ugeni wa mambo, vikwazo na changamoto za kujitoa sadaka ili uwe wa kwanza kuonesha njia kwa wengine kumefanya pawe na watu wachache ambao wapo tayari kuingia gharama, mateso na magumu huku wakijua huenda wasije kushuhudia au kutambuliwa hata baada ya wao kutengeneza njia kwa ajili ya wengine.

Jamii zetu zina wingi wa watu ambao wameyaona mambo yakienda isivyotakiwa na wanajua hatua ambazo zinaweza kufanyika ila nani aanzishe, nani athubutu ? hapo ndipo wengi huyaacha tu yaendelee kuwepo na kuishi nayo wakiyazoea. Mabadiliko ili yatokee eneo kama hilo ni mpaka pale mmoja ambaye ni jasiri, imara, mwenye nia anapokubali jukumu zito la kutengeneza njia ili wengine waone namna ya kuvuka hapo. Watu hawa si kuwa hawana hofu bali wanaweza kuwa na hofu ila wamechagua kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine wapite na kufaidika.

Kutengeneza njia kwa eneo lolote la maisha ili wengine waanze kuona njia kunataka moyo thabiti, ukakamavu na kuwa tayari hata kufa kwa ajili ya wengine. Kutengeneza njia kunaogopesha maana ni sawa na mtu anayesafiri kwenda safari asiyokuwa nayo wenyeji. Mashaka makubwa hutokea pale ambapo mtu hajui nini matokeo yanayoweza kujitokeza kutokana kwa utengenezaji wa njia kwa ajili ya wengine. Kujitoa ili njia itengenezeke kumegharimu wengine hata maisha yao kukosa kuwa na watu wa karibu ili tu wengine wapate nafasi ya kuvuka.

Kutengeneza njia kunamtaka mtu ambaye amevuka ubinafsi bali kajitoa kubeba magumu, kuwa tayari kujeruhika, kuwa tayari kuvumilia ili njia ipatikane. Hii kazi si rahisi ndo maana huwezi kushangaa kwanini hatuna watu watengeneza njia katika jamii zetu wengi kwa kuwa kazi hii ni ya hatari na ngumu.

Mbali na kufahamu kuwa kutengeneza njia kugumu ila kuna manufaa makubwa sana ya watengenezaji njia ambayo hudumu vizazi hadi vizazi. Mateso ya watu ambao walikubali kuyapoteza maisha yao kwa kupambana, kuvumilia, kustahimili kuanzisha mambo, kubuni vitu, kufikiri na kutengeneza mifumo ni alama kubwa ambayo huwa haifutiki katika maisha kuwa mchango wao ulikuwa mkubwa na mhimili wa maisha tulonayo sasa.

Wakati mwingine wa safari ya kutengeneza njia kwa ajili ya wengine kunaweza kuambatana na upweke na ukiwa. Wengi huona kutengeneza kwao njia kunakuwa kugumu, hali ya kukata tamaa hutokea na wengine hata kurudi nyuma kabisa. Manufaa wanayoyafikiria yatatokea kwa kutengeneza njia ni makubwa ambayo huwasaidia waendelee hilo huwafanya wao wajikaze na kuhakikisha wanafika hadi mwisho wa kuandaa njia kwa ajili ya wengine.

Ukiwa umejitoa kutengeneza njia kwa ajili ya wajao basi jiandae kuwa utakutana na magumu, upweke, mateso na kujikuta peke yako ila alama utakayoacha itakuwa na manufaa makubwa tofauti na ukiacha mambo yaendelee kuwa hivyo hivyo wakati unayo nafasi ya kuonesha njia.

NA  KOCHA  KOCHA  MWL.  JAPHET  MASATU , DAR  ES  SALAAM

WhatsApp  + 255 716 924136 /    + 255 755 400128 /  + 255 688 361 539 

EMAIL :  japhetmasatu@gmail.com

 

MAISHA BORA HUJENGWA KATIKA SUBIRA , HEKIMA , NA ULIMI MWEMA.

Maisha yanahitaji nini kama si uwezo mkubwa wa mambo matatu. Maisha ni mapambano ambayo yanahitaji moyo wa subira, ubongo wa hekima na ulimi mwema. Haya mambo matatu unapokuwepo nayo maishani basi ni njia ya kuyaishi maisha bora katika dunia hii. Maisha yatatupa magumu, mateso na matatizo hivyo ili uwe imara lazima uwe na moyo wa subira, uwe na hekima na udhibiti wa ulimi au uneni wako.

Magumu mengi yanayojitokeza katika maisha yanazidi kuwa makubwa pale ambapo tunakosa kuwa ni watu wenye subira, kukosa hekima na udhibiti mdogo wa kauli zetu. Unapokuwa na moyo wa subira unaweza kuvumilia na kukabiliana na hali zozote katika maisha. Unapokuwa na ubongo wa hekima unajiepusha na maangamivu yaletwayo na ujinga na tatu unapokuwa na udhibiti wa kinywa chako unajiepusha migogoro na watu wanaokuzunguka.

Jifunze kuwa na subira katika maisha haya. Ili umeanzisha kitu basi jua hakiweza kukupatia matokeo leo leo bali unapaswa kuvuta subira ukiwa unaendelea kuweka juhudi hadi ufike kuyapata matokeo yake. Moyo wa subira utakusaidia ukomae katika kuyakabili mambo maishani. Ukikosa subira utakuwa ukipata changamoto nyingi za kuumizwa hisia maana hakuna kitu kilicho bora maishani kisichohitaji moyo wa subira.

Itafute hekima ili uweze kuyaongoza maisha. Hekima ni lulu katika maisha ya mtu. Walio na hekima hutafutwa kila sehemu maana kupitia hekima maisha huenda, maisha huwa salama na kuwa imara. Hekima huzaliwa katika kujifunza kutokana na maisha ya watu wengine, kukaa na watu wenye hekima, kusoma vitabu na kadhalika.

Mwisho zuia ulimi wako usiseme hila, usisambaze habari zisizo za kweli na ruhusu ulimi wako usambaze upendo na nuru kwa wengine. Hili litakuepusha na mambo mengi maishani.

Maisha yanaweza kuwa imara uwapo katika jitihada ya mambo haya matatu. Kuwa na moyo wa subira, ubongo wa hekima na udhibiti wa ulimi. Yaishipo ndani ya mtu humpa mtu kuwa na maisha bora.

NA  KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU

WhatsApp + 255 716 924136 /   + 255 755 400128

EMAIL : japhetmasatu@gmail.com