Tuesday, June 16, 2020

JINSI UNAVYOWAZA KILA SIKU HUPELEKEA KUWA MASKINI AU TAJIRI.

Watu sio maskini eti kwa sababu hawana pesa, watu ni maskini ni kwa sababu ya mawazo yao. Unaweza ukawa unapato zuri sana lakini ukabaki kuwa maskini katika maisha. Kitakachokufanya uwe maskini ni matumizi ya mawazo yako katika kukufanikisha.

Wapo watu wengi sana ambao wana kipato kikubwa lakini wanashindwa kufikia utajiri. Hapo hakuna uchawi wowote ni matokeo ya matumizi ya mawazo. Wataalamu wa mambo ya mafanikio wanatuambia hivi, asilimia 90 ya matatizo yote ya pesa yana sababishwa na matumizi ya mawazo au akili zako.

Hivyo, ni muhimu sana kila wakati kuangalia, je mawazo yako yana uwezo wa kukufikisha kule unakotaka kufika kimafanikio? Ukiona una mashaka hata kidogo, ongeza juhudi ya kujifunza na kutamani kujua kila kitu kinachohusiana na pesa na mafanikio maishani mwako.

Wewe ni tajiri mkubwa sana, ikiwa utajiamini na kukubali kutumia nguvu kubwa ya mawazo uliyo ndani mwako kukufanikisha. Miaka kadhaa mbele naamini utakuja kunitafuta na kuniambia aisee ni kweli ulichosema  Mwl   Masatu. Yote hayo yanawezekana kwako, hakuna uchawi zaidi kuchukua hatua na kujituma.

Ndimi Rafiki  Kocha  Mwl  Japhet   Masatu ,  see  you  at   the   top .  Tuwasiliane  kwa   WhatsApp / Meseji / Call + 255  716  92 41  36