Thursday, September 18, 2014

MAARIFA YA KUPATA PESA NA UTAJIRI ----BIASHARA YA KUKODISHA VITI

KUKODISHA  VITI      kwa     ajili   ya    SHEREHE  , HARUSI , MIKUTANO , KIPAIMARA  n.k .   ni  biashara   ambayo   haikugharimu   kitu    zaidi    ya    KUNUNUA     VITI    na     KUAZIMISHA.


TAFUTA   CHUMBA ,  hata   kimoja  tu    KINATOSHA.   NUNUA   VITI   VYA  PLASTIKI     KAMA   MIA   TATU   HIVI    VYA   KUANZIA.  Kila  kiti  kinauzwa   ELFU   KUMI.    kodisha  kila   kiti     kimoja    kwa     shs.  300 /=   kwa    siku   moja { saa  24 }.

 Kwa  mfano , Ukiazimisha    viti   200   kwa   siku   moja tu   utakuwa    una   shs.  60,000/ =.  Hii   ni    mojawapo     ya     shughuli    ya    KUKUINGIZIA   MAPATO   AINA   YA  TULI (  PASSIVE   INCOME ).  Baadaye   waweza  kupanua biashara   kwa   kununua  na   MEZA , STULI , MATURUBAI ,  VYOMBO  n.k.


MAPATO  TULI  ni  mapato   anayoyapta    mtu  pasipo   kuwa   na   ulazima  wa   kushughulika  au  kufanya  kazi  kwa   wakati  huo. Yanatokana  na  kazi  au  shughuli  uliyokwisha  kufanya  kitambo   na  kuendelea    kupata  mapato  haya  kimya  kimya.  Unayapata  kutokana  na  vitega  uchumi   ulivyo  weka.

No comments:

Post a Comment