Tuesday, September 2, 2014

TAFUTA SHABAHA / LENGO LA MAISHA.

Watu   wengi   zaidi   hasa  VIJANA, wanaonekana    kupoteza   SHABAHA  yao  au   LENGO   lao  katika   MAISHA.  HUISHI   maisha  ya  hapa    na  pale    WAKIFUKUZIA  MANUFAA  YA  MUDA    MFUPI.    SABABU   yao  pekee    ya  kufanya  KAZI   ni    ili   kupata   HUNDI   YA  MALIPO  kwa    madhumuni   ya  kukidhi    MATAMANIO    YA  KUFANYA  ANASA   NA   STAREHE.Utafutaji  wa    FURAHA  wa  namna    hii   hauwezi    kumfkisha   mtu    popote.
      Bila  kujali   zama  tunazoishi , dhati  ya  UBINADAMU  inabaki   kuwa  ile  ile. NI   KUTAFUTA   MAISHA    yenye    KUPENDEZA  na    KUFANIKIWA  kufikia  hali    ya     KUTOKUFA  KWA  KUKIACHIA  KIZAZI     KIJACHO   jambo  ambalo     LITAENDELEA   KUKINUFAISHA.Tunapaswa  kutafuta  MAISHA   yaliyotimia  ili  siku    moja     tuweze    kusema 
  "NILIFANYA  KAZI    KWA  BIDII , NILITENDA   MAMBO  YENYE  MANUFAA , NA    NINAJISIKIA   FURAHA."
   Baadhi    ya  watu    wanaweza  wasikubaliane   na  mimi  kuhusu  WAZO  HILI , LAKINI    naamini  kwa   dhati  kabisa  kwamba    njia   hii    ya   KUJIBIDIISHA KATIKA   MAISHA  NI  BORA  ZAIDI  KULIKO  ILE  NJIA  RAHISI.  Watu    wenye   uzoefu  mkubwa zaidi  wanaweza  kuelewa  kile  ninachokisema. KWA  BAHATI  MBAYA , WATU   WA  AINA  HIYO  HAWAKO  TAYARI  KUTOA  MAONI  YAO  KUHUSU   MAISHA.  SABABU  ambayo   kwa   kawaida  wamekuwa    wakiitoa  ni kwamba,   WAKATI  umebadilika    na    HADITHI  zao  za  kale  hazina  mchango  wowote  KWA   VIJANA   WA  LEO. LAKINI   kama  tukizungumza   kwa dhati   ya   moyoni  ,  WATU   WENGI  WATAJITOKEZA   kuzungumzia    kile  TUNACHOAMINI.
        KWA  KUHITIMISHA  NASEMA      " MFUMO    wa    MAISHA   RAHISI  MWANZONI    UNAWEZA  KUONEKANA  KAMA  WA  KUCHANGAMSHA  NA   KUVUTIA  HATA  HIVYO   HUFIKA  WAKATI  SISI  SOTE  TUKATAMANI  KUWA  NA   SHABAHA YA/ LENGO LA  JUU  ZAIDI  KIMAISHA.

No comments:

Post a Comment