Monday, September 22, 2014

JE, NI LINI TUANZE MIPANGO YA KUSTAAFU ?

                    MIPANGO     YA    KUSTAAFU
Maandalizi   kwa    ajili  ya   MAISHA    YA   UZEENI    ni    lazima     yaanze   tangu   ukiwa    KIJANA   na   sio   mpaka  uanze  KUZEEKA.   MAISHA   YASIYO  NA  MIPANGO    ENDELEVU    mpaka    unapofikisha   UMRI   WA    MIAKA   65   hayawezi   KUFANIKIWA   GHAFLA    pindi   unapostaafu.


ANZA   SASA   kujiwekea   AKIBA   na    kuwekeza   kwa    ajili    MAISHA    YAKO   YA    BAADAYE   KUANZIA    SASA.

HAUTAKIWI    KUSUBIRI  mpaka  upate  PESA     ndio    uanze    MIPANGO   YA  KUSTAAFU ,   bali    unatakiwa    UWE    na   mipango  KABLA    ili    utakapopata   KAZI   AU   PESA     uwe   na    kazi    ya  KUITEKELEZA  TU    MIPANGO  ambayo  tayari   ilishapangwa.


  SIRI   YA   MAFANIKIO:  Watu   wenye    MIPANGO    kabla   ya   kupata  PESA    HUFANYA    MAMBO   MAKUBWA  sana   na    mazuri   pindi   wanapopata   PESA  kuliko    wale      WANAOSUBIRI  na    KUANZA    MIPANGO  baada    ya    kupata    PESA  AU   PINDI   PESA   ZINAPOKUWA  TAYARI  MEZANI.

Hata  kama   unakaribia   KUSTAAFU   au   tayari   umeshastaafu  bado    unayo  nafasi. Kamwe   huwa   hakuna   kuchelewa   katika   kufanya    MABADILIKO  chanya   katika   maisha   yako.  NI   BORA  KUCHELEWA  KULIKO   KUTOFANYA  KAMWE { Better   late   than   never }.
 Inakadiriwa    kwamba  ukiachana   na kiwango   cha   kipato ,  zaidi  ya   70%  ya   waajiriwa   wanakuwa  wameishiwa   kabisa  kabla   ya   mwisho    wa   mwezi.  Mara  nyingi  wanaanza  maisha   ya MADENI   mpaka   MSHAHARA   mwingine   unapokuwa  tayari. Hata  kama   wewe    ni  miongoni  mwa  hawa  bado  una  uwezo  wa   KUJIWEKEA   AKIBA  kwa  ajili  ya  maisha  yako  baada ya  kustaafu.

MAISHA  UNAYOISHI   SASA   YANAASHIRIA  AINA  YA   MAISHA   UTAKAYOISHI  BAADAYE.

     Mungu  Akubariki   kwa   Kusoma   Makala   hii. 

No comments:

Post a Comment