Saturday, November 23, 2019

VITUKO VYA TAREHE ZA MSHAHARA------- ??????

Tarehe za mshahara huwa zina vituko sana. Mtu anaondoka nyumbani hakuwa na mpango wa kununua chochote, lakini anarudi na furushi ka vitu kemkem alivyonunua, ambavyo anajishawishi ni muhimu. Ila umuhimu huo unakuwa umeonekana kwa sababu mtu anakuwa na fedha. 

Lakini pesa zinapoisha, mtu anarudi kwenye maisha ya unyonge, maisha ya uombaomba, maisha ya kukopa. Je umechoshwa na hali hiyo? 

Kama jibu ni ndiyo basi KARIBU    UJIUNGE  NASI  KATIKA   DARASA   LA   SEMINA---ONLINE ( Google  Classroom )    KILA   SIKU   KWA  ADA  YA   Tshs  10000  kwa  mwezi , ndani ya DARASA  LA  SEMINA  utajifunza jinsi unavyoweza kutengeneza kipato cha pembeni ya mshahara wako na ukawa na maisha mazuri wakati wote na siyo tu tarehe za mishahara. 

Kwa  maelekezo   Zaidi  Wasiliana  na  Mwl.  Japhet  Masatu kwa  namba  zifuatazo :  WhatsApp / Call /  Meseji +255 716 924136 /  + 255 755 400 128 . 
Tengeneza maisha yenye msimamo sasa na acha kuishi mwisho wa mwezi kwa mwisho wa mwezi.
                UJINGA   NI   MZIGO.

MADOGO MADOGO YA KILA SIKU HUBOMOA AU KUJENGA NDOA.

Hakuna kitu kimoja peke yake kinaweza kuifanya ndoa yako kuwa bora. Bali mkusanyiko wa mambo madogo madogo ya kila siku ndiyo yanaweza kujenga au kubomoa ndoa. 

Hakuna mtu ambaye ameamka akajikuta na tabia ambayo anayo sasa katika ndoa yake. Tabia zote tulizonazo katika mahusiano yetu tumezitengeneza sisi wenyewe iwe ni tabia nzuri au mbaya bali sisi ndiyo wazazi wa tabia ambazo tunazo sasa.
Katika shabaha ya makala yetu ya leo tunakwenda kujifunza utii wa mgongo wa ndoa.

Uti wa mgongo wa ndoa yako ni heshima. Unapoheshimika heshimika.

Mwenzako anapowahi kurudi nyumbani hapo amekuheshimu. Heshima ni kitu cha bure wala hakihitaji mtaji.

Unapomheshimu mwenzako kwa yale mambo madogo naye anakuheshimu pia.
Leo ni vigelele kesho isiwe kelele.

Thamini kile anachofanya mwenzako, kwa kufanya hivyo unakuwa unamweshimu mwenzako.
Unapompenda mwenzako unakuwa unamweshimu. Hivyo kumpatia mwenzako upendo ni kumpa dozi ya heshima.
Ukiheshimiwa jiheshimu. Hapa unatakiwa kujiheshimu hata uvaaji wako, tembea yako ioneshe kama vile vile wewe ni mke au mume wa mtu.

Huwa tunajidharirisha sisi wenyewe kwa namna nyingi, unapokuwa mlevi kwa mfano, ukalewa mpaka kujikojolea hapo unapokuwa umemdharirisha mwenzako na kumvunjia heshima.
Unapomshirikisha mwenzako wa ndoa katika mipango yako hapo unakuwa una mweshimu na yeye atakuheshimu pia na kwa kukushirikisha mipango yake.

Unapomuaga mwenzako au kumjulisha kuwa leo utachelewa kufika nyumbani kwa kitendo Kama hiko hapo utakuwa unamweshimu mwenzako wa ndoa.
Nyumba zinaungua usiku mchana zinakuwa vizuri ni methali ya kihaya, hapo ina maana kwamba hata kama mnatofauti zenu mzimalize ndani na mkiwa nje muwe vizuri.
Hatua ya kuchukua leo; mweshimu sana mwenzako wa ndoa. Mpe dozi ya upendo na msikilizane kwa upendo na kuheshimiana kila siku.

Kwahiyo, hakuna kitu kidogo katika ndoa. Thamani yoyote unayoitoa kwa mwenzako inakuwa ni heshima na heshima inakuwa ni uti wa mgongo wa ndoa yako.