Saturday, November 23, 2019

MADOGO MADOGO YA KILA SIKU HUBOMOA AU KUJENGA NDOA.

Hakuna kitu kimoja peke yake kinaweza kuifanya ndoa yako kuwa bora. Bali mkusanyiko wa mambo madogo madogo ya kila siku ndiyo yanaweza kujenga au kubomoa ndoa. 

Hakuna mtu ambaye ameamka akajikuta na tabia ambayo anayo sasa katika ndoa yake. Tabia zote tulizonazo katika mahusiano yetu tumezitengeneza sisi wenyewe iwe ni tabia nzuri au mbaya bali sisi ndiyo wazazi wa tabia ambazo tunazo sasa.
Katika shabaha ya makala yetu ya leo tunakwenda kujifunza utii wa mgongo wa ndoa.

Uti wa mgongo wa ndoa yako ni heshima. Unapoheshimika heshimika.

Mwenzako anapowahi kurudi nyumbani hapo amekuheshimu. Heshima ni kitu cha bure wala hakihitaji mtaji.

Unapomheshimu mwenzako kwa yale mambo madogo naye anakuheshimu pia.
Leo ni vigelele kesho isiwe kelele.

Thamini kile anachofanya mwenzako, kwa kufanya hivyo unakuwa unamweshimu mwenzako.
Unapompenda mwenzako unakuwa unamweshimu. Hivyo kumpatia mwenzako upendo ni kumpa dozi ya heshima.
Ukiheshimiwa jiheshimu. Hapa unatakiwa kujiheshimu hata uvaaji wako, tembea yako ioneshe kama vile vile wewe ni mke au mume wa mtu.

Huwa tunajidharirisha sisi wenyewe kwa namna nyingi, unapokuwa mlevi kwa mfano, ukalewa mpaka kujikojolea hapo unapokuwa umemdharirisha mwenzako na kumvunjia heshima.
Unapomshirikisha mwenzako wa ndoa katika mipango yako hapo unakuwa una mweshimu na yeye atakuheshimu pia na kwa kukushirikisha mipango yake.

Unapomuaga mwenzako au kumjulisha kuwa leo utachelewa kufika nyumbani kwa kitendo Kama hiko hapo utakuwa unamweshimu mwenzako wa ndoa.
Nyumba zinaungua usiku mchana zinakuwa vizuri ni methali ya kihaya, hapo ina maana kwamba hata kama mnatofauti zenu mzimalize ndani na mkiwa nje muwe vizuri.
Hatua ya kuchukua leo; mweshimu sana mwenzako wa ndoa. Mpe dozi ya upendo na msikilizane kwa upendo na kuheshimiana kila siku.

Kwahiyo, hakuna kitu kidogo katika ndoa. Thamani yoyote unayoitoa kwa mwenzako inakuwa ni heshima na heshima inakuwa ni uti wa mgongo wa ndoa yako.

No comments:

Post a Comment