Friday, May 29, 2020

JE , WEWE NI MWANDISHI NA MCHAMBUZI WA VITABU , SOMA KILA SIKU NA SHIRIKISHA WENGINE ULICHOJIFUNZA.

1. Andika kile ambacho kinatoka ndani ya moyo wako, kile ambacho unasukumwa kukiandika, na siyo kuandika kuwafurahisha watu.
2. Tengeneza sauti yako ya uandishi, unaweza kuwa na waandishi au mwandishi unayemkubali au kujifunza kwake, ukajikuta unaandika kama yeye, huwezi kufika mbali kiuandishi, tafuta mtindo wako mwenyewe wa uandishi, ambao utakutofautisha.
3. Kazi ya uandishi kuna wakati ina upweke mkubwa, inakuhitaji uwe na muda mwingi peke yako kuliko kazi wanazofanya wengine, lazima uwe tayari kwenye hilo.
4. Unastahili na unapaswa kulipwa kupitia uandishi wako, usiache kuwataka watu walipie pale wanapotaka zaidi kutoka kwako.
5. Chagua hadhira utakayoiandikia na cha kutaka kila mtu awe msomaji wako, kama unalenga kila mtu huna unayemlenga. Jua kabisa unamwandikia mtu wa aina gani, na hapo uandishi wako utagusa maisha ya mtu.
6. Unaweza kuandika makala 100 nzuri kabisa, na watu wachache mno wakakushukuru au kukupa moyo kwa unachofanya. Lakini ukaandika makala au kutuma ujumbe mmoja ambapo umekosea na utashangaa kila mtu anakukosoa na kukupinga. Hata watu ambao hawajawahi kukupa moyo kwa makala nzuri 100 ulizoandika, watakuwa wa kwanza kukuhukumu kwa makala moja mbaya uliyoandika. Elewa hilo na usikubali likuumize.
7. Sehemu kubwa ya wale wanaokukosoa kwenye uandishi ni wivu tu. Wanatamani wangeandika, ila hawawezi kukaa chini na kuandika, wakiona wewe unaandika wanatafuta makosa ya kuonesha kwamba wewe siyo bora kuliko wao.
8. Epuka sana kujisifia kila wakati kupitia uandishi wako, watu wana wivu, kadiri unavyojisifia ndivyo wanavyotafuta makosa ya kukurudisha nyuma.
9. Usisubiri ukamilifu, andika na toa, iwe ni makala au kitabu au chochote, una nafasi ya kuboresha zaidi baadaye, kwa kutoa toleo la pili na mengine mengi.
10. Fanya uandishi kuwa kitu cha kwanza kwenye siku yako, andika kabla hujaendelea na ratiba nyingine za siku yako. Ukishindwa kutenga muda wa asubuhi na kuandika, ni vigumu sana kupata muda siku yako ikishaanza, na pia siku inavyoenda unachoka, na akili ikishachoka, utajipa kila sababu kwa nini usiandike.
Makala  hii  imeandikwa   na  KOCHA   MWL    JAPHET   MASATU  ambaye  ni  mwalimu  kitaaluma ( B.Ed ( AE ) , Kocha  wa  MAISHA   NA  MAFANIKIO , MWANDISHI  na  MJASIRIAMALI  , BLOGGER
WhatsApp + 255 716  924 136 /  + 255 755 400128  /   + 255 688 361 539

Wednesday, May 20, 2020

HAMISHA TABIA ZA AJIRA KWENDA KWENYE KUJIAJIRI UTAFANIKIWA SANA.

Tabia hizo kumi ni kama ifuatavyo;
(1).UNAENDA  KILA SIKU.

Kila siku ambayo ni ya kazi, unaenda kazini. Haijalishi kama unajisikia au hujisikii, umechoka au hujachoka, ni siku ya kazi na unaenda kazini. Na ili kuhakikisha unaenda, sehemu za kazi kuna daftari au mashine ya kuweka sahihi, ili kuthibitisha kwamba kweli umefika kazini.

Unapojiajiri, hakikisha kila siku ya kazi ambayo umejipangia kulingana na kile unachofanya basi unaenda kwenye eneo lako la kazi. Japokuwa una uhuru wa kwenda au kutokwenda, usiutumie kabisa uhuru huo, wewe nenda, iwe unajisikia au hujisikii, iwe umechoka au la. Chukulia kuna bosi anakusubiria pale, na hawezi kukuelewa kama hujaenda.
(2). CHANGAMOTO  ZA  MAISHA  HAZIINGILII  KAZI.
Usiku umegombana na mke wako au mume wako, asubuhi unaamka na kujiandaa kwenda kazini. Hukai nyumbani na kumwambia bosi leo huendi kwa sababu kuna ugomvi nyumbani. Umeamka una mafua makali unajiandaa na kwenda kazini, husemi mafua haya wacha nipone kwanza. Mwajiri wako hawezi kukuelewa.

Peleka tabia hiyo kwenye kujiajiri pia, usikubali sababu ndogo ndogo zinazoendelea kwenye maisha yako kuingilia kazi zako. Endelea na kazi kila siku, kama ambavyo ungeenda kwenye kazi ukiwa umeajiriwa. 
(3). UNAKAA  KAZINI  MUDA  WA  KAZI.
Unaenda kazini kila siku, na ukifika, unakaa mpaka muda wa kazi uishe ndiyo unaondoka. Hata kama siku hiyo huna kazi za kufanya, utakaa hapo kazini mpaka muda wa kutoka ufike. Hata kama siku hiyo hujisikii kufanya kazi, utazurura zurura hapo ofisini mpaka muda wa kutoka ufike. Hutakatisha siku yako ya kazi kwa sababu tu hujisikii, siku ya kazi inaisha muda wa kazi unapoisha.

Hamishia hili kwenye kujiajiri, kwenye muda uliopanga kufanya kazi yako, fanya kazi na usiruhusu kuingiliwa na kitu kingine. Kama umepanga utaandika kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa sita mchana, basi fanya hivyo. Usiahirishe kwa sababu siku hiyo hujisikii kuandika. Kama umepanga utafungua biashara yako saa moja asubuhi na kufunga saa moja jioni fanya hivyo, isitokee siku unafunga saa 10 kwa sababu siku hiyo umechoka zaidi. Jiulize kama ingekuwa kazi ya kuajiriwa je ungeacha, kama hapana, fanya.
( 4 ).UNAFANYA  KAZI  KWA MIAKA  MINGI.
Kazi yoyote unayoifanya, utaifanya kwa miaka mingi. Kama ni mwalimu utafundisha kwa miaka mingi, unaweza kuhama shule mbalimbali, lakini utafundisha. Kama wewe ni daktari utatibu kwa miaka mingi, unaweza kubadili vituo vya kazi, lakini utatibu. Utafanya kazi yako mpaka pale utakapostaafu au kufikia uhuru wa kifedha. Na hufikirii kuifanya kwa muda mchache na isipolipa unaacha, unaifanya kwa miaka mingi.

Peleka tabia hiyo kwenye kujiajiri pia, kile unachochagua kufanya, jiandae kukifanya kwa miaka mingi. Kama ni uandishi, jua utaandika kwa miaka mingi, kama ni biashara pia, jipe muda mrefu wa kufanya. Acha kabisa kujidanganya kwamba utafanya kwa siku chache na kama hailipi utaacha. Jiandae kufanya kwa muda mrefu.
( 5 ). UNA  MAHITAJI  MAKUBWA.
Kinachokufanya uendelee kuifanya kazi yako, hata kama ni ngumu au huipendi ni mahitaji makubwa uliyonayo. Unahitaji fedha ya kuendesha maisha yako, kula, kulala, kuvaa, kuendesha familia, kusomesha watoto na mengine. Una ndugu wanaokutegemea ambapo kazi yako ndiyo inakuwezesha kuwasaidia. Mwajiri akikuambia fanya tu kwa upendo hakuna haja ya malipo huwezi kumwelewa, una mahitaji, unataka fedha, unafanya kazi ili ulipwe.

Chochote unachofanya pale unapojiajiri, hakikisha unalipwa ili uweze kuendesha maisha yako. Na hili ni muhimu sana kwenye kazi za sanaa, ni rahisi kujiambia naandika kwa sababu napenda, siyo kwa sababu nataka kulipwa. Andika ili ulipwe, una mahitaji ya maisha yako, unafikiri utayamudu vipi kama unachofanya hakikulipi?
(6 ). UNAKUBALI MALIPO  YA  KAZI.
Unapoomba kazi, cha kwanza unachouliza ni mshahara. Unapofanya kazi hiyo kwa muda unamtaka mwajiri wako akuongeze mshahara. Unaenda kusoma au kuongeza ujuzi ili upate mshahara zaidi. Unafanya kazi muda wa ziada ili upate malipo zaidi.

Peleka tabia hii kwenye kujiajiri pia, hakikisha unapata malipo na kila wakati kazana kutoa thamani zaidi ili ulipwe zaidi. Weka juhudi kubwa ili kupata malipo makubwa. Na asikusumbue mtu kwamba unataka sana kulipwa, kama hayupo tayari kulipia achana naye. Hufanyi unachofanya kuuza sura, ndiyo kinawasaidia watu, lakini asante haitaleta chakula mezani, hakikisha unalipwa.

( 7 ). KAZI   YAKO  SIYO  WEWE.
Kama wewe ni mwalimu, unajua kabisa ualimu wako unaishia shuleni, hukutani na watoto barabarani na ukaanza kuwafundisha hapo hapo. Kama ni daktari udaktari wako unaishia hospitali, hupandi kwenye daladala na kuanza kuwatibu watu. Kwa kifupi ni kwamba unapokuwa umeajiriwa, unajua kuyatenganisha maisha yako binafsi na maisha ya kazi, huchanganyi hivyo pamoja.

Hapa ndipo wengi waliojiajiri huwa wanafeli, hawajitofautishi wao binafsi na kazi zao. Kila wakati wanachanganya kazi na maisha, na ndiyo maana hawapati muda wa kupumzika. Hivyo kwa kile ambacho umejiajiri kufanya, tenga muda wa kukifanya na tenga muda wa maisha pia. Kushindwa kufanya hivyo, utachoka haraka na kushindwa kuendelea. 
(8). UNAJUA  MBINU  ZA  KUFANYA  KAZI.
Kama wewe ni mwalimu, unajua mbinu za ualimu, njia za kufundisha watu mpaka waelewe na pia unaendelea kujifunza. Kama wewe ni daktari, unajua jinsi ya kudadisi dalili za mgonjwa, vipimo gani ufanye mpaka ujue mgonjwa anaumwa nini na kisha umpe matibabu sahihi. Huamki siku moja na kujiita daktari kisha ukaanza kutibu, unajifunza.

Peleka tabia hii kwenye kile unachojiajiri kufanya, mwanzoni jua kabisa ni muda wa kujifunza, kuzijua njia bora za kufanya kitu hicho na kila wakati kazana kujua mbinu bora zaidi. Unafanya vizuri pale unapokuwa na ujuzi wa kufanya. Hivyo jifunze ujuzi wa kile ulichojiajiri kufanya.
(9 ). UNA UCHESHI  AU  UTANI  KWENYE  KAZI.
Kwa kila kazi, kuna utani fulani upo, ambao huwa haukuumizi. Utani huo unaweza kuonekana kama ni kejeli, lakini haukusumbui. Mfano baina ya madaktari, huwa wanataniana sana, mfano daktari wa upasuaji atamuita daktari wa magonjwa ya ndani ni mtu wa kubahatisha, maana anatibu kitu ambacho hakioni. Daktari wa magonjwa ya ndani atamuita daktari wa upasuaji kama mtu wa buchani, kazi yake ni kukata vitu. Huu ni utani ambao upo na madaktari hao hawapigani kwa sababu ya utani huo.

Tuhusu utani au ucheshi kwenye kile ambacho umejiajiri kufanya. Kuna watu watachukulia hiyo kama sehemu ya kukudhihaki au kukukejeli, lakini wewe utachukulia ni kama utani tu na utaendelea kufanya. Mfano unaweza kuwa mwandishi na watu wakakuambia unachoandika ni nadharia tu, hakiwezekani kwa vitendo. Usichukulie kwa umakini sana hilo, ona kama ni utani na endelea kuandika.
(10 ). UNAPOKEA  SIFA  NA  LAWAMA  KWA  KAZI  UNAYOFANYA.
Ukiwa kwenye ajira, unaweza kufanya kazi yako vizuri na ukasifiwa sana, wakati mwingine unakosolewa na kulaumiwa kupitia kazi yako. Unajua hiyo ni sehemu ya kazi, hivyo huendi nyumbani na kukosa usingizi kwa sababu bosi wako amekuambia ripoti uliyoadika siyo sahihi. Unajua kesho utaenda kufanya marekebisho kama alivyokuambia, ni sehemu ya kazi.

Peleka tabia hii kwenye kujiajiri pia. Kwa kila unachofanya, jua kuna wakati itasifiwa na kuna wakati utapingwa, kukosolewa au kulaumiwa. Kuwa tayari kupokea hayo na kuchukua hatua sahihi. Usiache kuandika kwa sababu mtu amekuambia makala yako au kitabu chako ni cha hovyo, jua kipi hakipo sahihi na boresha zaidi kwenye uandishi ujao.

MIRADI 10 INAYOWEZA KUENDESHWA NA WANAWAKE

Mwanamke kuwa na kazi au biashara ya kufanya na ikamwingizia kipato ni kitu cha muhimu sana, maana dunia ya sasa hivi tunaishi Kwa kutegemeana. Na wanawake tuna fursa nyingi sana za kujiongeza kiuchumi kama mtu ukiwa na bidii, uvumilivu na kutogopa vikwazo.
Nitakwenda kuorodhesha biashara au miradi ambayo mwanamke unaweza kuifanya , kitu cha muhimu ni anza mradi kutokana na mtaji na ujuzi ulionao na uwe unakipenda hicho kitu kutoka moyoni;

1. Bakery: hii ni bishara ya kutengeneza na kuuza vitafunwa inapata kasi sababu watu wengi hawapendi kununua vitafunio mitaani, hata kama huna mtaji wa kufungua bakery unaweza kupika vitafunwa mbalimbali nyumbani Kwa order au ku supply kwa wenye maduka au migahawa.

2. Shule za chekechea, ni biashara nzuri Kama ukipata eneo zuri na ukatoa huduma nzuri, na walimu wakiwa wana ujuzi wa kutosha. Pia kama wewe ni mwalimu unaweza kuanzisha shule yako mwenyewe kutokana na mtaji wako.

3. Event management and catering , siku hizi sherehe ni nyingi sana na watu wawataki kuangaika na mambo ya chakula, mc, mapambo, usafiri nk, wana kodi kampuni ya watu Kwa ajili hiyo.

4.Ufundishaji wa ujuzi mbalimbali, wanawake wengi wana penda kujifunza mambo mbalimbali ili watumie huo ujuzi kwenye ujasiriamali, iwe ni kupika vyakula, utengenezaji wa sabuni, mapambo, kilimo nk. Ukiwa na ujuzi wowote utumie kufundisha wengine na ujipatie kipato.

5.Maduka ya urembo na kuuza nguo za wanawake, hii ni biashara nzuri sababu supply ni kubwa mfano Dar kariakoo kuna maduka mengi tu ya jumla unaweza kupata bidhaa, na wanaume wengi wanafanya Biashara hii Ila ikifanywa na mwanamke ni bora zaidi unajua kabisa vitu gani wanawake wanapenda.

6.Insurance, consultancy companies: Kama una elimu, uzoefu na mtaji wa kutosha unaweza kuanzisha kampuni yako ya bima au kotoa ushauri mbalimbali au watu kukupa kazi zao uwafanyie na unaweza kufungua kampuni mbalimbali.

7.Biashara ya chakula, unaweza kuanzisha hotel au kimgahawa na ukapika vyakula, muhimu uweze kuandaa chakula vizuri, na kuandaa mazingira masafi na huduma ziwe nzuri.

8.Biashara ya kuuza maua na miche, hii ni biashara unaweza kuanza bila mtaji au mtaji kidogo sana, kama una maua yakate na uoteshe mengi zaidi katika vifuko, pia miche ya miti au matunda unaweza kuetengeneza kitalu, unaweza kupata maua Kwa watu hata kununua bei sio ghali. Tafuta eneo zuri la kuuzia hata kwako muhimu ni kujitangaza.

9.Biashara ya vinywaji; soma zaidi hapa

10.Biashara ya mapambo ya nyumba

Miradi iko mengi sana na bidii yako ya kufanya utafiti na kujifunza wengine wanafanya nini. Pia kumbuka biashara yoyote mwanamke unaweza kufanya na suala la mtaji sio tatizo sana mikopo ipo mradi utafute yenye masharti nafuu.


Kwa ushauri wa  BIASHARA / UJASIRIAMALI na MAISHA  wasiliana nami WhatsApp 0716924136  /   + 255 755 400 128 /  + 255 688 361 539  /  + 255 629 748 937
KOCHA MWL JAPHET MASATU

Thursday, May 14, 2020

MTAJI NI MDOGO ? --JINSI YA KUKABILIANA NA USHINDANI WA BEI .

Zifuatazo ni hatua za kuchukua ili kukabiliana na ushindani wa bei pale unapofanya biashara kwa mtaji mdogo.
 (01 ). CHEZA  MCHEZO  WAKO  MWENYEWE.
Kama unataka kupata ushindi kwenye eneo lolote la maisha yako, basi unapaswa kucheza mchezo wako mwenyewe. Hii ina maana kwamba unapaswa kutengeneza mchezo wako, kujiwekea sheria zako mwenyewe, kisha kucheza mchezo huo. Ukiingia kucheza mchezo wa wengine, ambao wameutengeneza wao na kuweka sheria zao, huwezi kushinda, maana wao ndiyo wanaoujua mchezo huo kuliko wewe.
Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye biashara, haijalishi unafanya biashara gani, unapaswa kucheza mchezo wako mwenyewe. Hapa unapaswa kupanga ni aina gani ya biashara unaifanya na utaifanya kwa njia zipi. Tengeneza njia zako mwenyewe, ambazo zinatumia uwezo ulio ndani yako na aina ya wateja unaowalenga, kwa kile unachouza. Jiwekee sheria zako mwenyewe na kisha endesha biashara yako kwa sheria hizo.
Chagua kufanya biashara ya tofauti, ambapo sheria yako kuu kwenye ushindani siyo bei, bali utofauti. Usishindane kwa kupunguza bei, bali shindana kwa kutoa kitu ambacho biashara nyingine hazitoi. Kwa maneno mengine, usikazane kuwa bora zaidi ya wengine, bali kazana kuwa tofauti na wengine.
Hakikisha kuna kitu ambacho wateja wanakipata kwenye biashara yako, ambacho hawawezi kukipata kwenye biashara nyingine yoyote. Inaweza kuwa aina ya bidhaa unazouza, inaweza kuwa aina ya huduma wanayoipata. Ni lazima uwe na kitu ambacho wateja wanakipata kwako tu na hawawezi kukipata kwa wafanyabiashara wengine.
Kama kwenye biashara unayoifanya huwezi kutengeneza kitu cha aina hiyo, ushindani wa bei hauwezi kukuacha salama. Usitegemee utoe kile ambacho kinaweza kupatikana kwa wengine, halafu wateja waje kununua kwako kwa bei juu wakati wanaweza kupata kwingine kwa bei ya chini.
Kumbuka ubinafsi ni asili yetu binadamu, huwa tunaangalia maslahi yetu kwanza kabla ya kitu kingine. Hivyo hakikisha kwenye biashara yako kuna kitu unachowapa wateja wako, kinachowanufaisha na hawawezi kukipata sehemu nyingine. Kwa kuwa na kitu hicho, watakuwa tayari kuja kununua kwako kwa bei ya juu kuliko kwenda kwa wengine wanaouza kwa bei ya chini.
 ( 02 ). ANZA  NA  WATEJA  SAHIHI.
Kuna wateja ambao wanachoangalia ni bei tu, na wapo wateja ambao wanachoangalia ni thamani wanayoipata. Ni vigumu sana kumshawishi mteja anayeangalia bei rahisi kuona thamani.
Hivyo kabla hujaweka nguvu zako kwenye ushawishi au mengine yoyote, anza na wateja sahihi. Jua kwanza kinachomsukuma mteja kununua ni bei au thamani.
Kama kinachomsukuma mteja kununua ni bei peke yake, usipoteze hata muda wako, kwa sababu atakwenda kule ambapo anapata kwa bei ya chini. Lakini unapokutana na mteja ambaye anaangalia thamani anayoipata, hapo una nafasi ya kumshawishi kulipa zaidi ili apate thamani zaidi.
Wateja wa thamani siyo wengi, lakini wale wachache unaowapata watakufanya ufurahie kuifanya biashara yako, maana huwa ni waelewa na hawakusumbui sana.
Wateja wa bei rahisi huwa ni wengi, lakini pia ni wasumbufu. Unaweza kuwapunguzia bei na bado wakaona umenufaika zaidi na hivyo kutaka zaidi kutoka kwako.
Kwa biashara unayofanya, chagua aina ya wateja unaotaka kwenda nao, kisha tafuta aina hiyo ya wateja. Wanapokuja wateja wanaoangalia bei tu, waeleze thamani unayotoa na kama bado wanasisitiza kwenye bei, unaweza kuwaelekeza wapi pa kupata kwa bei wanayotaka wao, lakini pia waoneshe nini watakosa kwa kuangalia bei pekee.
 ( 03 ). KUWA  KARIBU   ZAIDI  NA  WATEJA WAKO.
Biashara ndogo huwa zinazishinda biashara kubwa kwenye eneo hili, uwezo wa kuwa karibu na wateja. Biashara kubwa zinahudumia watu wengi, hivyo huwa hazihangaiki na mteja mmoja mmoja, hivyo mteja hawezi kupata upekee kwenye biashara kubwa.
Ila kwenye biashara ndogo, kwa sababu wateja ni wachache, ni rahisi kumpa kila mteja upekee anaostahili. Ni rahisi kumjua kila mteja na matakwa yake, hivyo wajibu ni kumtimizia mteja yale anayotaka kwa namna yake mwenyewe.
Kosa kubwa ambali wafanyabiashara wengi wadogo huwa wanafanya ni kufanya biashara zao ndogo kama vile ni biashara kubwa, kitu ambacho kinawagharimu sana.
Kuwa karibu zaidi na wateja wako, wasiliana nao mara kwa mara, jua matukio mbalimbali kwenye maisha yao, mfano siku zao za kuzaliwa, watu wao wa karibu na kadhalika. Kisha watumie salamu au jumbe mbalimbali katika siku zao hizo muhimu.
Tumia kila fursa kuwapa wateja wako upekee, uwafanye wajisikie vizuri wanapokuja kwenye biashara yako ambapo wanalipa zaidi kuliko wanavyojisikia wanapokwenda kwenye biashara kubwa ambapo wanalipa kidogo.
 ( 04 ).  WAFUATE  WATEJA  KULE  WALIPO.
Njia nyingine ya kuongeza thamani kwa wateja wako ili wawe tayari kulipa zaidi kwako ni kuwafuata kule walipo. Sasa hivi watu hawana muda, hivyo wanapenda sana pale biashara inapowafuata wao kule walipo. Lakini pia uaminifu umekuwa mdogo, hivyo watu wengi huhofia kuagiza vitu ambavyo hawajaviona.
Wewe kwa kuwa na biashara ndogo, una nafasi ya kujenga uaminifu na wateja wako na kisha kuwafanya waweze kuagiza kile unachouza popote walipo na wakapelekewa. Hii inawafanya wateja wawe tayari kulipa zaidi, kwa sababu imewapunguzia usumbufu na upotevu wa muda kutoka walipo na kwenda kutafuta wanachotaka.
Biashara ndogo inaweza kuwafikia wateja kule walipo kwa ufanisi zaidi kuliko biashara kubwa, hivyo tumia vizuri nafasi hiyo.
 ( 05 ) WEKEZA  ZAIDI  KWENYE  BIASHARA  YAKO.
Unapomtaka mteja alipie zaidi kile anachonunua kwako, ambacho anaweza kukipata kwa bei ya chini sehemu nyingine, lazima utengeneze mazingira ambayo yatamfanya mteja aone anastahili kulipa zaidi. Mfano ukinunua soda ya cocacola kwenye duka la mtaani utalipa shilingi mia tano, lakini soda hiyo hiyo ukiinunua hotelini utalipa shilingi elfu mbili. Ukiwa hotelini hutalalamika kwa nini uuziwe soda ya mia tano kwa shilingi elfu mbili, kwa sababu kuna mazingira yanayokufanya uone kulipa elfu mbili ni halali. Unakuwa umekaa eneo zuri na tulivu, unahudumiwa na watu wanaokujali na kadhalika.
Hivyo pia ndivyo unavyopaswa kufanya kwenye biashara yako, fanya uwekezaji unaoipa biashara yako thamani zaidi kuliko washindani wako. Kuna kitu kidogo sana unaweza kukifanya kwenye eneo lako la biashara na likawafanya watu waipe thamani kubwa. Kitu hicho ni mwonekano wa eneo la biashara, linapaswa kuwa safi na lililopangiliwa vizuri. Mtu akifika kwenye eneo hilo anaona utofauti mkubwa, na ndani yake anakuwa tayari kulipa zaidi.
Wewe mwenyewe ni shahidi, huenda umewahi kufika kwenye eneo la biashara, na kwa jinsi lilivyo na mwonekano mzuri, ukajua utatozwa gharama kubwa, lakini ulipotozwa gharama za kawaida ukashangaa. Hiyo ndiyo hali unayopaswa kuileta kwenye biashara yako pia, kufanya uwekezaji unaowaandaa wateja kuwa tayari kulipa zaidi.
Mwonekano na mpangilio wa eneo la biashara, vifaa unavyotumia na huduma unayowapa wateja wako vinapaswa kuwa vya viwango vya juu sana kiasi cha mteja kuona kama anakuibia pale unapomtajia bei. Na kumbuka hapa utakuwa unawalenga wateja sahihi na siyo wale wanaoangalia bei ya chini pekee.
Rafiki, hizo ndizo hatua tano za kuchukua ili kuweza kukabiliana na ushindani wa bei pale unapofanya biashara kwa mtaji kidogo. Kama ulivyoona, kuna mengi ya kufanya kuliko kuingia kwenye ushindani wa moja kwa moja kwenye bei, ambao utakuumiza sana.
Nimalizie kwa kukuambia hili rafiki yangu, kama upo kwenye biashara ambayo kitu pekee unachoweza kujitofautisha nacho ni kupunguza bei, basi upo kwenye biashara ambayo siyo sahihi. Kwa sababu kuna wengine wapo tayari kupunguza bei zaidi yako, na wakiwa na mtaji mkubwa kuliko wewe, watapata faida kwa kuuza kwa wengi zaidi kuliko wewe unayeuza kwa wachache.
Hivyo fanyia kazi haya matano uliyojifunza, na mengine yanayoendana na hayo, lakini siyo kupunguza bei. Na kama biashara haina namna nyingine bali bei basi achana nayo na nenda kwenye biashara sahihi, ambapo unaweza kutengeneza mchezo wako mwenyewe na kuucheza vizuri.

JIUNGE  NA  DARASA  ONLINE  KWA  KULIPIA   ADA  YA  MWEZI , MWAKA---UJIFUNZE KWA  UNDANI  NA  MAPANA--ELIMU  YA  BIASHARA &  UJASIRIAMALI--- NA  UCHUKUE  HATUA --UTAFANIKIWA

SEE  YOU  AT  THE    TOP
Ndimi  rafiki   yako KOCHA /   MWL.  JAPHET   MASATU , BLOGGER
Kwa   maelekezo   zaidi  tuwasiliane  kwa ;--
SIMU / MESEJI / ( WhatsApp  + 255 716 924136 )    /    +255 755 400128  /  + 255 688  361  539 /  + 255 629 748  937