Wednesday, May 20, 2020

MIRADI 10 INAYOWEZA KUENDESHWA NA WANAWAKE

Mwanamke kuwa na kazi au biashara ya kufanya na ikamwingizia kipato ni kitu cha muhimu sana, maana dunia ya sasa hivi tunaishi Kwa kutegemeana. Na wanawake tuna fursa nyingi sana za kujiongeza kiuchumi kama mtu ukiwa na bidii, uvumilivu na kutogopa vikwazo.
Nitakwenda kuorodhesha biashara au miradi ambayo mwanamke unaweza kuifanya , kitu cha muhimu ni anza mradi kutokana na mtaji na ujuzi ulionao na uwe unakipenda hicho kitu kutoka moyoni;

1. Bakery: hii ni bishara ya kutengeneza na kuuza vitafunwa inapata kasi sababu watu wengi hawapendi kununua vitafunio mitaani, hata kama huna mtaji wa kufungua bakery unaweza kupika vitafunwa mbalimbali nyumbani Kwa order au ku supply kwa wenye maduka au migahawa.

2. Shule za chekechea, ni biashara nzuri Kama ukipata eneo zuri na ukatoa huduma nzuri, na walimu wakiwa wana ujuzi wa kutosha. Pia kama wewe ni mwalimu unaweza kuanzisha shule yako mwenyewe kutokana na mtaji wako.

3. Event management and catering , siku hizi sherehe ni nyingi sana na watu wawataki kuangaika na mambo ya chakula, mc, mapambo, usafiri nk, wana kodi kampuni ya watu Kwa ajili hiyo.

4.Ufundishaji wa ujuzi mbalimbali, wanawake wengi wana penda kujifunza mambo mbalimbali ili watumie huo ujuzi kwenye ujasiriamali, iwe ni kupika vyakula, utengenezaji wa sabuni, mapambo, kilimo nk. Ukiwa na ujuzi wowote utumie kufundisha wengine na ujipatie kipato.

5.Maduka ya urembo na kuuza nguo za wanawake, hii ni biashara nzuri sababu supply ni kubwa mfano Dar kariakoo kuna maduka mengi tu ya jumla unaweza kupata bidhaa, na wanaume wengi wanafanya Biashara hii Ila ikifanywa na mwanamke ni bora zaidi unajua kabisa vitu gani wanawake wanapenda.

6.Insurance, consultancy companies: Kama una elimu, uzoefu na mtaji wa kutosha unaweza kuanzisha kampuni yako ya bima au kotoa ushauri mbalimbali au watu kukupa kazi zao uwafanyie na unaweza kufungua kampuni mbalimbali.

7.Biashara ya chakula, unaweza kuanzisha hotel au kimgahawa na ukapika vyakula, muhimu uweze kuandaa chakula vizuri, na kuandaa mazingira masafi na huduma ziwe nzuri.

8.Biashara ya kuuza maua na miche, hii ni biashara unaweza kuanza bila mtaji au mtaji kidogo sana, kama una maua yakate na uoteshe mengi zaidi katika vifuko, pia miche ya miti au matunda unaweza kuetengeneza kitalu, unaweza kupata maua Kwa watu hata kununua bei sio ghali. Tafuta eneo zuri la kuuzia hata kwako muhimu ni kujitangaza.

9.Biashara ya vinywaji; soma zaidi hapa

10.Biashara ya mapambo ya nyumba

Miradi iko mengi sana na bidii yako ya kufanya utafiti na kujifunza wengine wanafanya nini. Pia kumbuka biashara yoyote mwanamke unaweza kufanya na suala la mtaji sio tatizo sana mikopo ipo mradi utafute yenye masharti nafuu.


Kwa ushauri wa  BIASHARA / UJASIRIAMALI na MAISHA  wasiliana nami WhatsApp 0716924136  /   + 255 755 400 128 /  + 255 688 361 539  /  + 255 629 748 937
KOCHA MWL JAPHET MASATU

No comments:

Post a Comment