Monday, September 8, 2014

MCHEZO TUUCHEZAO UITWAO MAISHA. MAISHA NI NINI ?

MAISHA   ni  mchezo  wa   kuigiza  ambao  kila  mmoja  wetu   ana   nafasi   mahususi   ya   kushiriki   kama    MWIGIZAJI. Hata   hivyo  tunachofanya   katika   MAISHA  yetu    wenyewe, ni  zaidi  ya  KUSHIRIKI  tu  kama    WAIGIZAJI----hakika   tunaandika   Mchezo   wenyewe. TOFAUTI  na   Mchezo  ambao   tayari  tunafahamu   kwamba  HATIMA   yake   ni    nini ,  HATIMA   YA  MAISHA   YETU    TUMEISHIKILIA    MIKONONI  MWETU     WENYEWE  .

     BAADHI   YA  WATU huamini  kwamba   HATIMA  ya    MAISHA  YETU  huwa   tayari  imeamuliwa  hata   KABLA  YA   KUZALIWA  KWETU.  MIMI   SI   KAMA  hao  wanaoamini    hivyo.   NINACHOAMINI    MIMI    NI   KWAMBA  UPO    UWEZEKANO  WA  KUBADILI   HATIMA  YA    MAISHA   YETU   WENYEWE  KWA    KUBORESHA   NAMNA  TUNAVYOZITUMIA  FIKRA  ZETU.
      
         BADALA   YA   KUISHI  KWA    KUTEGEMEA  KUDURA  TULIVYOPANGIWA ,  Tupanue   FIKRA  ZETU  ili  zituwezeshe    KUANDIKA  MCHEZO   WA  MAISHA    YETU    TUKIWA  TUMEJIPANGIA   NAFASI   TUNAZOPENDELEA   KUSHIRIKI   KATIKA   MCHEZO  HUO.  Kadiri  tutakavyoweza  kufanya    jambo  hili  mapema   ndivyo   tutakavyoharakisha     mwanzo   wetu   sisi   wenyewe    wa   kutawala   kikamilifu  kila    kipengele   cha    MAISHA   yetu  ya  kila   siku. 

        KATIKA  MCHEZO  UITWAO   MAISHA   KUNA    TOFAUTI   KUBWA   SANA  BAINA   YA  WALE    WALIOJIPANGIA   WENYEWE   NAFASI   ZA   UHUSIKA   KWENYE  MCHEZO  HUO , NA   WALE  WANAOISHI   MAISHA   YA    MAJALIWA    YASIYO    NA  LENGO.


     FURSA   mbalimbali   zinatusubiri   katika    mambo    mengi   yanayohusu   MAISHA   YETU.  Tuna  UWEZO    WA  KUZIPATA  FURSA   HIZO   KAMA  TUKIPANIA.   HATA   HIVYO   tusipokuwa   na   DHAMIRI   pamoja    na   MALENGO    BAYANA   KATIKA  FIKRA  ZETU ,  haitakuwa  rahisi   kufaulu  hata   katika   FURSA   zile   za     kawaida   na    bayana   kabisa.





KANUNI    YA    MAFANIKIO----JIPATIE   NAMBA   KATIKA   MCHEZO  UITWAO   MAISHA.

No comments:

Post a Comment