Wednesday, May 20, 2015

UNAYO BAHATI , LAKINI HUJUI KUITUMIA ! KILA MTU ANA BAHATI .



Bila  shaka  umekuwa  ukijiuliza  kwanini    watu    wengine   wana   bahati ? Ni  matajiri  wanafanikiwa  kimapato wana  pesa?  wana  mahusiano  mazuri  na  watu ?  Wana   kazi  nzuri ?    Yaani  ni  kama   miguuni  mwao   wanatembea  na  bahati ! Kwanini   isiwe   mimi pamoja   na juhudi  na  uwezo  nilionao ?  Nini  tatizo  kwangu  mimi   ninayesoma   makala  hii  ? Je, ni   mipango   ya  mungu  au …… ?  SOMA   SIRI  YA  MAFANIKIO  HAPA  CHINI !
KWANINI   WAO  WANA  BAHATI  ? NA   SI  MIMI  ?
Katika  utafiti unaonyesha  ya  kwamba , MTU  ANAJITENGENEZEA   BAHATI   MWENYEWE  KULINGANA   NA  JINSI  ANAVYOFIKIRI ,  NA  JINSI   ANAVYOTAZAMA  MAMBO , NA  JINSI  ANAVYOTENDA.
Pindi  utakapoanza   kubadili    jinsi   unavyofikiri   na   jinsi   unavyotazama   mambo   utaanza  kutengeneza   bahati   yako.
Ukitazama  kukosa , mikosi , balaa , shida  ndivyo    hivyo  itakavyokuwa.Ukitazama   kinyume  chake  yaani   kupata  au   kufanikiwa, bahati  nzuri , maisha   mazuri , kupata  pesa   ni   hivyo   hivyo    itakavyokuwa.
Watu  wanaodai   kuwa  hawana  bahati   ya  kufanikiwa , hujikosesha   wenyewe  bahati. Hukutana   na  fursa  au    nafasi  adimu  na   kuzipitiliza   bila  kutambua. Watu  wenye  bahati    husimama  mara    moja  pindi    wanapokutana  na  kitu   kipya  mbele    yao.
Kwa  mfano ,  siku   moja   unakutana   na  watu   usiowajua  kabisa.Watu  hao  wanazungumzia  biashara   fulani   yenye   kuzalisha  faida    kubwa. USIWAPUUZE !  Kaa  kitako   karibu  nao. Wasikilize   kwa    makini .Wadadisi   mengi   kadiri  uwezavyo.Hivi  ndivyo   bahati   huanza.  Hii  ndiyo    fursa  au   nafasi   usiichezee   kabisa   ndugu   yangu.
Watafiti   waligundua  kwamba   watu   wanaopata  bahati  ni  kwa  sababu   HAWACHEZEI   NAFASI  AU  FURSA  pindi   inpojitokeza   hata kama  ni  ndogo   mithili   ya  punje  ya  haradali. Na   siku  zote  hutarajia   kufanikiwa.  Husema ………….ipo  siku. Huamini  kuwa    hawajaumbwa  ili    wakose. Kwao  kukosa  ni  chanzo  cha  kupata.
Watu   wenye    bahati ,yaani  wale  wanaowaza  kufanikiwa , maisha  mazuri ,kupata   pesa  badala  ya  kulaumu kwa   mambo   yanayotokea  katika  maisha   ni    wenye   kushukuru  kwa   yale   yanayotokea    au  kile   kilichotokea .Kwao   glasi  tupu   ni  kama  glasi  iliyojaa.
Jinsi  unavyofikiri   na   jinsi  unavyotazama   mambo  ndivyo   unavyotengeneza  bahati. KILA   SIKU    FUKIRIA  KWAMBA  UNA   BAHATI, UTAONA  MAMBO  YATAKAVYOBADILIKA ! UTAONA  JINSI  UTAKAVYOVUTA  MATUKIO  YA  YENYE  BAHATI .ITAZAME  GLASI   TUPU  KAMA  ILIYOJAA.
Kumbuka  wengi   wetu  tunaamini  bahati   hutengenezwa   na  waganga  wa  kienyeji  au  jadi. Mtazamo  huo  si   sahihi. Bahati haipatikani  kwa   uchawi , wala  mwujiza. Bahati  ni  wewe  ni   jinsi   UNAVYOFIKIRI, UNAVYOTAZAMA  MAMBO  NA  JINSI  UNVYOTENDA.
Tambua  unapokuwa  na   AFYA  una   neema , hivyo   una   bahati. Unapokuwa   na  AKILI  timamu  una   neema, hivyo  una  fursa  pana  sana  ya  kupata   bahati.UHAI  ni  neema, unapokuwa  unapumua  pumzi, una  bahati , una  bahati kubwa  sana.
Unaitazama  neema   kinyume.Unaitazama  miguu  kama  si  bahati, unaitazama  mikono  kama   si  bahati , unayatazama   macho   kama   si  bahati. Unazitazama  neema  zote   zilizo  katika   mwili  wako  kama   si   bahati.Badala  yake ,  unatazama   mtu    mwenye  pesa   nyingi   kuwa  ana  bahati.  PESA   bila   AKILI , bila  AFYA  zitakuja ?  Na  hiki  ndicho   kinachofanya   baadhi  ya  watu   wanaiba , wanaua  ili   wapate   PESA.Hii  ni   kwa   sababu  wanatazama  mambo   kinyume.
Kitendo  cha   kutambua   kuwa , AKILI   na   AFYA   ni  fursa  za   bahati , jione   ni  mwenye   bahati   kubwa.Na  ukisikia  mtu  yeyote  anakwambia  ana   mkosi , basi   tambua  ana  ukosefu  wa   kutambua  elimu  hii ,  maana   mkosi  ni  ukosefu.
Bahati   ina   nafasi   katika  mafanikio  yetu,  lakini   kwa   wale   wapaniaji , wachapa  kazi  na  wenye  malengo. Binadamu  hupanga  na  kuamua  mwenyewe ,  awe   mtu  wa  namna  gani.Huwa  tunageuka  vipofu   kabisa   tunapoingia   kwenye  kudhani  mganga  fulani  anaweza  kuongeza  bahati   zetu, kutufanya    kupendwa  na  wateja  hata  kama  tunawatukana  wateja  hao  au  kutuwezesha  kupata  dhahabu  kwenye  shimo  la  udongo  wa   kufinyangia  vyungu.
Imani  kwamba   kuna   nguvu  ya  nje  ambayo   inaweza   kumsaidia   mtu   kupata  bahati  au  kufikia  mafanikio  bila   malengo   na  juhudi   yake   ni yenye  kupotosha   sana. Imani   kwamba , kuna   wenye  nota   zenye   kung”ara  kuliko  wengine , hivyo   hao  wanaweza  kupata  bahati  au   mafanikio  kirahisi  haina  ukweli.
Tulilishwa  imani  gani   kuhusu  sisi, kufikiri  kwetu   kukawa  kwa   namna  gani  na tukaweza   kuwa   na  malengo   au  hapana  maishani , huchangia  sana kutufanya  tuwe  na  mafanikio  au   tusiwe  nayo. Lakini  kuchagua   maisha   tunayotaka   kuishi , ndiyo  muhimu zaidi.Tukijiuliza   na  kutafuta  maarifa , tataujua  ukweli  na  hata  kama   tuliathiriwa   na  malezi ,  tutatoka  tu   kwenye   kiza.
                     Asante  sana  mdau    wangu   kwa   kusoma   makala  hii    muhimu  sana ili  kubadili  maisha   yako .Binadamu   ni    jinsi    anavyofikiri . Imeandaliwa  na   MWL  JAPHET    MASATU , anapatikana  kwa  namba   0716 924136 / 0755 400128.  Kama  una  swali au  maswali    kuhusu   mada  hii  uliza .

No comments:

Post a Comment