Tuesday, June 29, 2021

JINSI UNAVYOWEZA KUWA BILIONEA , HATUA KWA HATUA.

Whatever the mind of man can conceive and believe, it can achieve.” - Napoleon Hill

Rafiki yangu mpendwa,

Napoleon Hill, baada ya kufanya utafiti kwa watu zaidi ya 500 waliofikia utajiri mkubwa kwenye maisha yao na kuwalinganisha na wengine ambao hawakuweza kufikia utajiri, alikuja na kanuni rahisi ya mafanikio na utajiri aliyoishirikisha kwenye kitabu chake alichokiita THINK AND GROW RICH.

Sentensi moja ambayo unaweza kuitoa kwenye kitabu chake na ikabadili kabisa maisha yako ni ile inayosema; chochote ambacho akili ya mwanadamu inaweza kuelewa na kuamini, inaweza kukifikia.

Soma tena taratibu na uielewe kauli hiyo, kwani ina nguvu ya kuifungua akili yako na ikakuwezesha kupata kila unachotaka, ikiwepo kufika kwenye ubilionea.

Najua unavyosoma hapa kuna kisauti ndani yako kinakuambia hilo haliwezekani, kinakupa ushahidi kwamba katika mazingira yako hakuna aliyefikia ubilionea, wewe utawezaje. Sauti hiyo inakukumbusha kipato kidogo ulichonacho au madeni makubwa uliyonayo na kukuhakikishia huwezi kufika kwenye ubilionea.

Leo nina habari njema kabisa kwako, kwamba sauti hiyo haina nguvu kwako kama akili yako itaelewa na kuamini kile kweli unachotaka.

Na kwa ushahidi tu, hapo ulipo sasa hujafika kama ajali, bali ni matokeo ya kile ambacho akili yako imeelewa na kuamini kwa muda mrefu. Kama ulikuwa unaamini wewe ni wa chini na huwezi kupiga hatua, hayo ndiyo umezalisha mpaka sasa. Na kama utaamini unaweza kufanya makubwa, hilo pia ndiyo litatokea.

Ujumbe wangu kwako leo rafiki yangu ni huu, unaweza kuwa bilionea. Na ushahidi ni mabilionea ambao tayari wapo duniani. Kama wengine wameweza kufikia ubilionea, kwa nini wewe ushindwe?

Na kama alivyowahi kusema Benjamin Franklin, wachache kuwa matajiri ni ushahidi kwa wengine kwamba inawezekana.



Je upo tayari kujifunza kutoka kwa wale ambao wameweza kufikia utajiri na mafanikio makubwa kwenye maisha yako?

Kama jibu ni NDIYO  basi KARIBU    UJIUNGE   DARASA   ONLINE  LA  " MAISHA  NA  MAFANIKIO "  UJIFUNZE  SIRI   ZA  MAFANIKIO   YAO.

 WASILIANA  NAMI  SASA  ILI  NIKUUNGE.

KOCHA  MWL;  JAPHET   MASATU , DARA ES  SALAAM--TANZANIA

( WhatsApp + 255 716 924136 ) ,  + 255 755 400128

 

No comments:

Post a Comment