Thursday, September 2, 2021

MAGUMU , MATATIZO NI SEHEMU UKUAJI KATIKA SAFARI YA MAISHA , USIJILAUMU NA KULALAMIKA

Kujilaumu ni kitendo cha kujiona mwenye hatia dhidi ya jambo fulani unaloona kwa namna moja umelisababisha litokee na linakuumiza sana ukilitafakari. Hali hii ni mbaya tena iso na usaidizi wowote ule mbali na kuongeza ugumu na taabu ya jambo apitialo mtu. Mtu anaweza kuendelea kuumia juu ya jambo alofanya iwe ni siku za karibuni au miaka mingi imepita. Haisaidii kujilaumu au kulaumu mtu juu ya matukio mbalimbali yanayotokea maishani.

Jamii zetu nyingi tumejengewa hali za kulaumu watu pale mambo yanapoenda tofauti na vile ambavyo tumepanga. Hivyo watu wengi kulaumu wengine inakuwa inaonekana ni kisingizio cha kujiondoa dhidi ya jukumu hilo na kuona wengine walipaswa kuadabishwa kwa hilo. Wakati wote kulaumu au kujilaumu hakujawahi kusaidia kutatua majukumu ya maisha mtu anapoishi. Ni kujisahaulisha tu kuwa tatizo halipo ingali tatizo lipo.

Eneo mojawapo ambalo watu wengi huanza kujilaumu ni pale ambapo vipindi vya hali ngumu maishani vinapobisha hodi, watu hujilaumu huenda wao si watu wenye bahati maishani, wao ni watu wanaonewa, wao hawastahili kupitia hayo na wengine ni kuona ni mikosi tu wao kutokoma kupitia hayo magumu. Magumu ni tafsiri yetu tunayoiweka katika yale yanapotokea maishani. Inaweza kuwa ni matukio yenye kuumiza yamekuja kwa mkupuo kama misiba, hali zisizoleta dalili za afueni iwe ni mahusiano au uchumi, hali za kiugonjwa na kadhalika.

Magumu hutukuza misuli ya akili, hutukuza kuwaza kiutu uzima. Hili ndilo linalowasaidia watu wengi katika umri mdogo kuwa na uwezo mkubwa wa kukabiliana na maisha ambapo kumetokana na wao kupitia magumu na magumu hayo hayakuwadumaza bali yaliwasaidia kukua zaidi. Si rahisi mtu aliyepitia magumu na yakamsaidia kukomaa kushangazwa na hali ngumu za maisha zikitokea maana tayari anajua na uzoefu wa kupitia magumu ya awali. Watu imara hawatengenezeki kwa njia rahisi isipokuwa kwa darasa la kushinda changamoto na kukabiliana na kila gumu njiani.

Mtoto ambaye anaepushwa asipitie magumu au kujua uhalisia wa maisha mapema ni kumwandaa kutokuwa imara siku za baadaye. Atakapokuja kuishi na kukutana na magumu kwa mara ya kwanza lazima itampa wakati mgumu sana kukabiliana na hilo. Huenda wazazi wengi wanaogopa kuwaambia watoto wao juu ya ugumu katika kuyakabili maisha kwa kuona watakuwa wakiwaonea ila si kweli bali wanawapa wakati mgumu baadaye watakapopita katika magumu hayo. Magumu humfanya mtu akutane na ukweli wa maisha kuwa maisha ili ukue kiuzoefu lazima upite magumu mbalimbali yanayomjenga mtu kuwa imara na kuyaendesha maisha.

Uhalisia wa maisha ni kuwa mtu atapitia magumu katika siku za kuishi kwetu. Magumu yapo na yataendelea kuja kwa namna tofauti tofauti. Si kuyalaumu pale yanapokuwa zamu yake kujitokeza. Magumu hutuimarisha na kutukuza kuyaona mambo

NA  KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU , DAR  ES  SALAAAM , TANZANIA

WhatsApp + 255 716 924136 / + 255 755 400128  /   +  255 688  361 539


 

No comments:

Post a Comment