Friday, November 30, 2018

TUNA MIPANGO MINGI SANA NA MIZURI, TATIZO NI UTEKELEZAJI WAKE ???

Mipango ni rahisi sana, kila mtu anapanga na msimamishe mtu yeyote njiani na muulize mipango yake ni ipi, atakupa mipango mizuri sana.

Pamoja na kila mtu kuwa na mipango mizuri, ni wachache sana ambao wanaweza kufanyia kazi mipango hiyo na ikawa uhalisia kwenye maisha yao. Wengi wamekuwa wanabaki na mipango tu, lakini haiwi uhalisia.

Kinachowazuia wengi kutekeleza mipango waliyonayo ni tabia ya kuahirisha mambo. Hii ni tabia ambayo ni asili yetu sisi binadamu, huwa hatupendi kufanya chochote ambacho kinatuumiza au kinataka tuweke kazi.

Huwa tunapenda kutumia muda wetu kwa vitu visivyo na maana. Kwa muda ule ule na kwa nguvu zile zile, huwa tunaona ni bora kutumia kufanya vitu ambavyo vitatupa raha ya muda mfupi, kuliko kufanya vitu ambavyo havina raha ya muda mfupi lakini kwa muda mrefu vina maana.

Kinachowatofautisha wale wanaopata mafanikio makubwa kwenye maisha yao na wale wanaoshindwa siyo bahati wala akili wala fursa. Kinachowatofautisha ni namba wanavyoweza kuishinda tabia ya kuahirisha mambo. 

Wanaofanikiwa na wanaoshindwa wote wanakuwa kwenye mazingira sana, wanakutana na fursa sawa, lakini wale wanaoshindwa huwa wanasubiri wakati wanaofanikiwa wanachukua hatua.

No comments:

Post a Comment