Friday, November 16, 2018

HUDUMA MBOVU, HUPOTEZA SANA WATEJA.

Huwezi kukwepa kukosa wateja kama una huduma mbovu kwa wateja wako. Unaweza usiwe wewe, hapa wanaweza wakawa ni wasaidizi au wafanyakazi wako  ndio wanaokuharibia pasipo wewe kujua kitu chochote na ukaona uko sawa.
Wengi kwa kushindwa kujua kwamba wanahuduma mbovu ndio wanajikuta ni chanzo cha kuanza kupoteza wateja wengi tena bila kujua. Huduma yako mbovu inaweza ikawa kwenye bidhaa au mazingira au  hata jinsi ya kuwahudumia wateja na wakaridhika.

NINI  UFANYE ?
Hapa kuwa makini sana na mazingira yote yanayoweza kupelekea huduma mbovu ikatolewa, kama wafanyakzi wako, mazingira na bidhaa unazozitoa. Vitu hivyo unatakiwa kuvihakiki mara kwa mara ili visiwe chanzo cha huduma ya hovyo kwako na kupelekea kukosa wateja. 

Na  Mwl  Japhet  Masatu , Dar  es  salaam , Tanzania, Afrika  Ya  Mashariki

+255 716 924136 ( WhatsApp ) , +255 755 400128 
EMAIL: japhetmasatu@gmail.com

No comments:

Post a Comment