Friday, November 2, 2018

KUWA STADI UTAPATA FURAHA YA KWELI KATIKA MAISHA YAKO.

Umahiri katika jambo fulani unalofanya kwenye maisha yako. Mtu unakuwa na furaha pale unapojua kwamba kuna kitu unaweza kukifanya vizuri na kikawa na msaada kwenye maisha ya wengine.

Mtu unakuwa na furaha pale unapofanya kitu chenye maana kwako na kuweza kukifanya kwa ustadi na umahiri wa hali ya juu. Hata kama kitu ni kigumu kiasi gani, unapoweza kukifanya vizuri, unajijengea kuridhika ndani yako na hiyo ndiyo inakufanya uwe na furaha ya kudumu.

Ukitaka kudhibitisha hili angalia watu ambao wanapata fedha nyingi bila ya kufanya kazi. Labda wameshinda bahati nasibu au wamepata urithi, maisha yao huwa mabovu sana licha ya kuwa na fedha nyingi. Ni kwa sababu wanakuwa hawajafanya kitu kikubwa kupata fedha hizo, na wengi huishia kuzipoteza.

UFUNGUO  WA   FURAHA: Chagua kitu au eneo utakalokuwa na ustadi nalo kwenye maisha yako, eneo ambalo utafanya vizuri na utaongeza thamani kwenye maisha ya wengine. Kama ni mwalimu fundisha vizuri sana, kama daktari tibu vizuri, kama mwandishi andika vizuri vitu vinavyowasaidia watu. Kadhalika kwenye kilimo, ufundi, uwakili na ujuzi mwingine wowote.

No comments:

Post a Comment