Friday, November 2, 2018

JENGA MAHUSIANO CHANYA UTAPATA FURAHA YA KWELI KATIKA MAISHA YAKO

Mahusiano yetu na wengine yana mchango mkubwa sana wa namna maisha yetu yanavyokuwa. Kama utakuwa na mahusiano chanya, mahusiano ya kuelewana na wale watu unaojihusisha nao, mahusiano ya kujaliana, mahusiano ya kuwa tayari kutoa zaidi, kwa kuhusiana na wanaotoa zaidi, basi maisha yako yatakuwa ya furaha.

Kitendo cha kujua kuna watu wapo kwa ajili yako, na wewe upo kwa ajili ya wengine kinakufanya uridhike na maisha na kuwa na furaha.
Kwa upande mwingine mahusiano hasi, yasiyo na maelewano, yenye msuguano mara zote, ni chanzo cha kukosa furaha kwa wengi.

UFUNGUO WA FURAHA:Tengeneza mahusiano chanya kwenye maisha yako, chagua wale watu ambao ni wa muhimu kwako na unapenda kuwa na mahusiano bora na wao, kisha wape muda na wajali zaidi. Kuwa tayari kujitoa zaidi kwa ajili yao, na wao watakuwa tayari kujitoa kwa ajili yako.

No comments:

Post a Comment