HUDUMA ZETU / OUR SERVICES

DARASA LA JUMA LA 24; NJIA TATU ZA KUJENGA AU KUBADILI TABIA.
 
Habari wanamafanikio?
 
Napenda kuchukua nafasi hii kuwapa taarifa ya darasa la juma la 24 2019.
 
Katika darasa hili tunakwenda kujifunza njia tatu za kubadili tabia na kuweza kujijengea tabia bora kabisa za mafanikio.
 
Wote tunajua umuhimu wa tabia kwenye mafanikio, hivyo darasa hili ni muhimu sana kwa mafanikio ya kila mmoja wetu.
 
Kwenye darasa hili tunakwenda kujifunza yafuatayo;
 
1. UMUHIMU WA TABIA KWENYE MAFANIKIO.
 
2. JINSI TABIA ZINAVYOJENGEKA KWENYE MAISHA YETU.
 
3. MAENEO MATATU MUHIMU KWENYE KUJENGA TABIA.
 
4. NJIA TATU ZA KUJENGA AU KUBADILI TABIA.
 
5. JINSI YA KUCHAGUA NJIA BORA KWAKO KUTUMIA.
 
6. MASWALI, MAONI NA SHUHUDA KWENYE UJENGAJI WA TABIA.
 
Darasa hili litafanyika kupitia kundi la wasap la KISIMA CHA MAARIFA.
 
Darasa litafanyika jumapili ya tarehe 16/06/2019 kuanzia saa 12 jioni mpaka saa 2 usiku.
 
Kila mmoja wetu asikose darasa hili, ni muhimu sana kwenye safari yetu ya mafanikio.
 
Karibuni sana wote.
 
JIUNGE NA KISIMA CHA MAARIFA KUSHIRIKI DARASA HILI NA MENGINE MENGI.

Rafiki, kama bado hujawa mwanachama wa KISIMA CHA MAARIFA basi unakosa maarifa mengi na mzuri kwa mafanikio yako.
Jiunge na KISIMA CHA MAARIFA leo na unufaike na maarifa haya mazuri yanayopatikana kila siku.

Maelezo zaidi kuhusu kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA;

Hongera sana kwa kupenda kujiunga na kundi la wasap la KISIMA CHA MAARIFA.
Kundi la KISIMA CHA MAARIFA ni kundi tofauti na makundi mengine ambayo upo au umewahi kuwepo.
Kwa kuwa ndani ya kundi hili utapata nafasi ya kusoma makala za biashara, mafanikio, uchambuzi wa vitabu na makala nyingine nzuri kila siku.
Pia unapata nafasi ya kushirikishana mawazo na watu wengine wenye mtazamo chanya wa mafanikio.
Kila siku unapata makala ya KURASA ZA MAISHA YA MAFANIKIO ambapo utajifunza mambo muhimu ya kukuwezesha kuwa na maisha bora yenye furaha na mafanikio makubwa.
Kila siku unapata nafasi ya kuianza siku kwa TAFAKARI ya siku ambayo inakupa kitu chanya cha kufanyia kazi kwenye siku husika ili kuboresha maisha yako na kazi zako pia.
Na kila jumapili kunakuwa na mjadala wa DARASA LA JUMAPILI ambapo unapata kujifunza mambo mbalimbali kitoka kwa waliofanikiwa na wanaofanya. Unajifunza kuhusu uwekezaji, biashara, kilimo, mafanikio kwenye kazi na mengine mengi.

Karibu sana kwenye KISIMA CHA MAARIFA.
Kujiunga unatakiwa kulipia ada ya mwaka ambayo ni tsh laki moja (100,000/=). Ada hii ni kuanzia unapolipa mpaka utakapomaliza mwaka ndiyo unalipa tena.
Tuma ada kwa namba zifuatazo, tigo pesa 0717396253 au mpesa 0755953887, majina ya namba hizo ni AMANI MAKIRITA.
Ukishatuma ada tuma ujumbe kwenye wasap kwenye namba 0717396253 na utapewa maelekezo ya kujiunga.
Karibu sana kwenye KISIMA CHA MAARIFA tujifunze kwa pamoja na kushirikiana ili tuweze kufikia mafanikio makubwa.

No comments:

Post a Comment