Wednesday, May 1, 2019

FURAHA HAIPATIKANI KWENYE MATOKEO , BALI IPO KWENYE MCHAKATO.

Kama unaitafuta furaha kwenye maisha, tayari umeshapotea, kwa sababu unatafuta kitu ambacho hakipatikani. Furaha haipo mwisho wa safari, bali ipo kwenye safari yenyewe. Furaha haipatikani mwishoni, bali katika ufanyaji wenyewe.
 
Ndiyo maana nakuambia furaha ndiyo njia yenyewe, hakuna njia ya kukupeleka kwenye furaha.
 
Mtu anajiambia nikipata kazi nitakuwa na furaha, anaipata na haioni furaha, anajiambia nikipanda cheo nitapata furaha, anapanda cheo hapati furaha, anajiambia tena nikiwa bosi nitakuwa na furaha, anakuwa bosi na haioni furaha. Mtu huyu haoni furaha kwa sababu anaangalia sehemu ambayo siyo sahihi. Furaha haipo kwenye matokeo bali ipo kwenye mchakato. Hivyo kama mtu huyo anataka furaha, basi inapaswa kutoka kwenye kazi zake za kila siku, na siyo matokeo ya mwisho ya kazi zake.

No comments:

Post a Comment