Sunday, May 5, 2019

CHANGAMOTO TANO ZINAZOKABILI KILA AINA YA BIASHARA.

Zipo changamoto kubwa tano ambazo zinakabili kila aina ya biashara, changamoto hizi tano ndiyo zinapelekea biashara nyingi kufa na hata zinazopona kushindwa kukua zaidi.
 
(1). KUKOSA  UDHIBITI .  Huna udhibiti wa kutosha kwenye muda wako, soko na hata biashara yako. Badala ya kuiendesha biashara, biashara inakuendesha wewe.
 
(2). WATU. Unavurugwa na wafanyakazi, wateja, wabia na hata wanaokusambazia huduma mbalimbali. Watu hao hawaonekani kukuelewa na wala hawazingatii yale unayowataka wazingatie.
 
(3). FAIDA. Faida unayopata haitoshi kuendesha biashara.
 
(4). UKOMO. Ukuaji wa biashara yako umefika ukomo, kila ukikazana kuweka juhudi zaidi hakuna ukuaji unaopatikana, unajikuta unachoka zaidi lakini hakuna cha tofauti unachopata.
 
( 5 ). HAKUNA  KINACHOFANYA  KAZI. Umeshajaribu mbinu mbalimbali za kuiwezesha biashara yako kukua na watu kukuelewa, lakini hakuna hata moja ambayo imeleta matokeo mazuri. Unaelekea kukata tamaa na kuona labda biashara siyo bahati yako.
 
Changamoto hizi tano zinaikabili kila aina ya biashara, lakini habari njema ni kwamba, changamoto hizi siyo mwisho wa biashara, unaweza kuzivuka na kuiwezesha biashara yako kukua zaidi kama utazingatia nguzo sita muhimu za ukuaji wa biashara yako.

No comments:

Post a Comment