Saturday, May 4, 2019

KUWA NA MKAKATI WA MASOKO YA BIASHARA YAKO.

Upi mkakati wa masoko unaofanyia kazi wa  biashara     yako ?
Biashara ni wateja, bila ya wateja, haijalishi una bidhaa au huduma bora kiasi gani, huna biashara. Na njia pekee ya kuwaleta wateja kwenye biashara hiyo ni mkakati wa masoko.
Wafanyabiashara wengi wadogo huwa hawajisumbui kabisa na masoko. Huwa wanaendesha biashara zao kwa mtazamo wa kizamani kwamba ukijenga biashara wateja watakuja wenyewe. Lakini zama hizi ambazo wafanyabiashara ni wengi, hakuna mteja atakayekuja kwako, bali unapaswa kuwatafuta wateja.
Unawatafuta wateja kupitia mpango mkakati wa masoko unaokuwa nao kwenye biashara yako.
Hii ni kusema kwamba ili biashara yako ifanikiwe, lazima iwe na mkakati wa masoko, ambao unawatambua wateja wa biashara hiyo, kuwafikia kule waliko na kuwashawishi kununua.
Mkakati wako wa masoko unapaswa kuzingatia vitu vinne muhimu sana;
  1. Kuwatabua wateja sahihi wa biashara yako, wale ambao wanaweza kunufaika na bidhaa au huduma unazotoa.
  2. Kutambua vitu vitatu vinavyokutofautisha wewe na wafanyabiashara wengine wanaofanya biashara kama yako. Kama huna utofauti wowote na wafanyabiashara wengine, hakuna sababu ya mteja kuja kwako.
  3. Mchakato sahihi wa ufanyaji wako wa biashara, jinsi mteja anavyohudumiwa na hatua zote zinazochukuliwa kwenye biashara yako.
  4. Uhakika unaowapa wateja wako. Wateja wamepata fedha zao kwa shida, hawataki kuzipoteza, hivyo wanahofia sana kufanya manunuzi mapya. Unapaswa kuwapa uhakika kwamba wakinunua kwako hawapotezi fedha bali wanapata thamani.
Tengeneza mkakati wako wa masoko ambao unajumuisha vitu hivyo vinne na utaweza kuwafikia wateja wengi na kuwashawishi kununua kwako.

No comments:

Post a Comment