Friday, May 24, 2019

UNAHITAJI KUWA NA KOCHA , MENTA AU MSHAURI ILI UWEZE KUPATA CHOCHOTE UNACHOHITAJI KATIKA MAISHA YAKO

Ili kupata unachotaka, unahitaji kupata mwongozo kutoka kwa mtu mwingine. Mtu huyo anaweza kuwa kocha, menta au mshauri ambaye anakusimamia ufike kule unakotaka kufika.
 
Iko hivi rafiki, sisi binadamu ni wavivu na hatupendi kujitesa. Tunaweza kuweka mipango mikubwa na mizuri sana, lakini tunapokutana na ugumu ni rahisi kuacha na kujiambia haiwezekani au hatuwezi.
 
Lakini unapokuwa na mtu wa pembeni ambaye anakuangalia na kukusimamia, kwanza hutataka kumwangusha, hivyo utajisukuma zaidi na pili yeye mwenyewe hatakubaliana na wewe kirahisi, hivyo itakubidi ujaribu tena na tena na tena kabla hujasema haiwezekani.
 
Watu wengi wamekuwa wanajiwekea malengo peke yao, na asilimia 99 wamekuwa hawayafikii. Ila wale wanaoweka malengo na kuwa na mtu wa kuwasimamia kwenye malengo yao, zaidi ya asilimia 90 wanayafikia.
 
Hii ndiyo nguvu kubwa iliyopo kwa kuwa na mwongozo. Kwa sababu pia mtu anayekuongoza anaweza kukushauri vizuri pale ambapo unakuwa umekwama. Ni rahisi kuona makosa ya mchezaji aliyepo uwanjani ukiwa nje ya uwanja, lakini yule aliyepo uwanjani anaweza asione kwa urahisi. Kuna makosa unaweza kuwa unafanya kwenye maisha yako lakini huyaoni, ila unapokuwa na mtu anayekusimamia, atakuonesha makosa hayo kwa urahisi na utaweza kupiga hatua sana.
 
Unahitaji kuwa na mtu wa kukusimamia kwenye malengo na mipango uliyonayo ambaye atakusukuma kuyafikia.

No comments:

Post a Comment