Saturday, May 4, 2019

WEKA MALENGO YA MUDA MREFU ( MIAKA MITANO , KUMI ........... !! ) YA BIASHARA YAKO.

Ni lengo lipi kubwa unataka kufikia ndani ya miaka MITANO ,  KUMI ?  YA  BIASHARA   YAKO ?

Kabla sijaendelea hapa, hebu tafakari hilo swali na jipe majibu sahihi. Ni lengo lipi kubwa unalofanyia kazi ambalo unataka kulifikia miaka MITANO , KUMI  ijayo? Watu wengi wanaweza kushangaa unapangaje miaka kumi ijayo, wengi kupanga mwaka mmoja tu ni shida.

Huwezi kufanikiwa kwenye biashara kama huna malengo ya muda mrefu. Na hata kinachofanya wafanyabiashara wengi kukimbizana na fursa mpya zinazojitokeza ni kwa sababu hawana malengo yoyote ya muda mrefu, hivyo chochote kinachojitokeza wanaona ni sahihi kwao kukimbizana nacho.

Unapaswa kuwa na lengo kuu la miaka MITANO , KUMI  ijayo ya biashara yako, wapi unataka kufika na kwa kiwango gani. Lengo hili ndiyo litakusukuma kila siku, ndiyo litakuwa mwongozo wako na ndiyo litaathiri kila maamuzi unayofanya.

Kama huna lengo la miaka MITANO , KUMI  ijayo ya biashara yako, hujajitoa kufanikiwa kweli kwenye biashara hiyo. UNATANIA  NDUGU !  BADILIKA !  NA  AMKA !

No comments:

Post a Comment