Saturday, May 4, 2019

KILA BIASHARA INA CHANGAMOTO ZAKE . USIPUUZE AU KUKWEPA IKABILI KILA CHANGAMOTO INAPOJITOKEZA.

Ni changamoto zipi unazokutana nazo na unazoweza kukutana nazo mbeleni?
Kila biashara ina changamoto zake, hakuna biashara isiyokuwa na changamoto kabisa. Lakini watu wengi huwa hawapendi kukutana na changamoto, na hivyo huwa hawapo tayari kuzikabili.
Wanachofanya wafanyabiashara wengi pale wanapokutana na changamoto ni kuzipuuza au kuziacha wakiamini zitaondoka zenyewe. Changamoto hizo huwa haziondoki, badala yake zinakua na kuota mizizi, na hizo ndiyo huja kuua biashara.
Unapaswa kujua zipi changamoto kubwa zinazoikabili biashara yako sasa na hata siku za mbeleni. Kisha kuwa na mkakati sahihi wa kukabiliana na kila changamoto pale inapojitokeza. Usijaribu kupuuza au kukwepa changamoto, badala yake ikabili kila changamoto inapojitokeza, na siyo tu utaitatua, bali pia utapiga hatua zaidi kwenye biashara yako.

No comments:

Post a Comment