Sunday, May 5, 2019

WEWE NA BIASHARA YAKO NI VITU VIWILI TOFAUTI

Hiki ni kitu ambacho kila mfanyabiashara anapaswa kuambiwa, tena kupigiwa kelele kila mara mpaka aelewe. Kwa sababu kama wafanyabiashara wakielewa hili, nusu ya matatizo ya biashara yatatoweka yenyewe.
 
Sehemu kubwa ya matatizo ya biashara yanasababishwa na mfanyabiashara kufikiri yeye ni biashara yake, kitu ambacho siyo kabisa.
 
Biashara nyingi hazikui kwa sababu hakuna mpaka baina ya biashara na mmiliki wa biashara. Mtu anaweza kutoa fedha kiholela kwenye biashara kwa sababu anaona biashara ni yake. Kitu ambacho kinakuwa na athari kubwa sana kwenye ukuaji wa biashara hiyo.
 
Ndugu , naomba nikusisitizie hili, na liandike mahali ambapo utaweza kulisoma kila siku; WEWE SIYO BIASHARA YAKO, wewe na biashara yako ni vitu viwili tofauti kabisa.
 
Wewe una maisha yako, ndoto zako na mahusiano yako, biashara ina maisha yake, ndoto zake na mahusiano yake. Kinachowaunganisha wewe na biashara yako ni mtaji ambao umeuweka kwenye biashara hiyo, mtaji huo umeikopesha biashara, na njia pekee ya kunufaika kupitia biashara hiyo ni pale inaopata faida baada ya kufanyika kwa biashara.
 
Ukiweza kuelewa hili, kwamba wewe siyo biashara yako, ukaiheshimu biashara yako na kuiacha ikue bila ya kuiingilia, ukaiendesha kwa misingi ya ukuaji wa biashara, utaiwezesha biashara hiyo kukua zaidi.

No comments:

Post a Comment