Wednesday, May 1, 2019

JINSI YA KUOKOA MUDA UNAOPOTEZA KILA SIKU NA OKOA MASAA MAWILI YA ZIADA KILA SIKU.

Kila mtu ana masaa 24 kwa siku ila kuna wanaofanikiwa sana na kuna ambao wanaishia kulalamika kwamba hawana muda. Kama una jambo ambalo ni muhimu kwako lazima utapata muda wa kulifanya. Tumia njia hizi hapa chini kuokoa muda unaopoteza kila siku na uanze kuwekeza kwenye maisha yako.

  Hebu fikiria unaambiwa ujisomee kila siku, ufanye mazoezi, ufanye  meditation, utenge muda wa kuweka mipango yako kwa siku, upate muda wa kupitia mipango yako, upate muda wa kupumzika na pia upate muda kwa ajili ya wale unaowapenda na wanaokupenda. Kwa mambo hayo tu tayari siku imeisha na bado hujaweka muda wa kufanya kazi na muda wa kulala.
 
  Kwa muda mfupi tulio nao ni vigumu sana kufanya mambo yote hayo kila siku. Unaweza kujiaminisha hivyo ila ni uongo mkubwa sana ambao umekuwa unajidanganya kila siku.
  Ili uache visingizio visivyo na maana leo ninakupa njia ya kupata masaa mawili ya ziada kila siku ambapo unaweza kufanya mambo hayo ambayo yatabadili maisha yako na kuwa bora zaidi.

  Kwanza hebu tuangalie muda wetu kwa siku. Kila binadamu ana masaa 24 kwenye siku moja. Wapo wengi ambao wameyagawa masaa yao kwa masaa nane ya kulala, nane ya kazi na nane ya kupumzika. Kwa vyovyote ulivyoyagawa wewe haijalishi, ila unaweza kuokoa masaa mawili ili kufanya mambo yako.

  Ili kupata masaa mawili ya ziada kila siku fanya mambo yafuatayo;
1. Amka nusu saa kabla ya muda uliozoea kuamka kila siku. Utumie muda huo kufanya jambo lenye manufaa kwenye maisha yako kama kujisomea au kuweka MALENGO   NA  MIPANGO. Na ili uweze kuamka nusu saa kabla ni vyema ulale mapema na ulale usingizi mzuri.

2. Punguza nusu ya muda unaotumia kusikiliza redio, kuangalia tv na kuangalia filamu. Asilimia 80 ya vipindi unavyofuatilia kwenye tv au redio havina msaada wowote kwenye malengo yako ya maisha. Asilimia kubwa ya taarifa zinazokushtua kila siku sio za kweli au zimeongezwa chumvi mno. Hivyo punguza muda huu unaotumia kwenye vyombo vya habari na uutumie kubadili maisha yako.

3. Punguza muda unaotumia kwenye mitandao ya kijamii hasa facebook na twitter. Mitandao hii ina ulevi fulani, unaweza kusema unaingia kuchungulia ujue ni nini kinaendelea ila ukajikuta saa nzima unashusha tu kuangalia zaidi. Na asilimia 90 ya unayofuatilia kwenye mitandao hii hayana msaada kwenye maisha yako. Tenga muda maalumu kwa siku wa kutembelea mitandao hii ili kujua nini kinaendelea.

4. Zima simu yako au iweke kwenye hali ya kimya kabisa(wala isitetemeshe). Hapa najua utanipinga sana na unaweza kudhani nimechanganyikiwa. Tumehamishia fikra zetu kwenye mawasiliano hasa ya simu. Mtu unakaa na simu ikiita kidogo tu unakimbilia kujibu bila ya kujali ni kitu gani cha muhimu unafanya. Inaingia meseji ambayo haina hata maana ila inakuhamisha kutoka kwenye jambo la muhimu unalofanya. Najua una madili mengi yanayokuhitaji kupatikana kwenye simu ila kuiweka simu yako mahali ambapo huwezi kuiona kwa masaa mawili kwa siku haiwezi kukupotezea dili lolote. Muda ambao unafanya kazi inayokuhitaji ufikiri sana na uwe na utulivu hakikisha simu yako haiwezi kukuondoa kwenye kazi hiyo. Hivyo izime au iwe kimya kabisa na iwe mbali.

No comments:

Post a Comment