Saturday, April 4, 2020

MFANAYABIASHARA / MJASIRIAMALI : JIKINGE WEWE NA TIMU YAKO.

Wewe mfanyabiashara ukiumwa au wasaidizi wako wakiumwa, biashara itaathirika zaidi. Hivyo wewe na timu yako mnapaswa kuwa mstari wa mbele katika kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huu.
Hakikisha njia zote za kujikinga zinajulikana na kutumika na kila anayehusika kwenye biashara yako. Njia kuu zinafahamika, kunawa mikono kwa maji safi na sabuni, kuepuka kushikana, kuepuka kushika uso. Hivi vyote vinapaswa kufanyiwa kazi.
Pia eneo la biashara liboreshwe kwa namna ambayo linapunguza maambukizi. Ukaribu baina yako au watoa huduma na wateja unapaswa kupunguzwa. Maeneo ya kunawa mikono yanapaswa kuwepo au dawa za kusafisha mikono kupatikana kwa urahisi.
Usiache kujilinda wewe na timu yako kwa kuepuka gharama, ukiugua wewe au timu yako, ni tiketi ya kifo kwa biashara yako.

Mfano; kwenye kila eneo la biashara kunapaswa kuwa na sehemu ya watu kunawa mikono kwa maji na sabuni au kwa dawa maalumu. Pia kama biashara inahusisha watu wengi, kuwekwe utaratibu wa kupunguza msongamano wakati huu. Kwenye huduma za afya, watoa huduma wanapaswa kuwa na vifaa vya ziada vya kujilinda wao wenyewe.

No comments:

Post a Comment