Saturday, April 4, 2020

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : MIKAKATI YA UKUZAJI BIASHARA IENDELEE.

Wakati wa majanga kama haya, wengi huacha kufanyia kazi mikakati yao ya ukuzaji wa biashara. Kwa kuwa hali ya uchumi inakuwa siyo nzuri, wateja siyo wengi na waliopo hawanunui sana, wafanyabiashara huona hakuna haja ya kujisumbua, badala yake wanasubiri mpaka mambo yawe vizuri.
Kama tulivyoona mpaka sasa, hakuna mwenye uhakika mambo yatarudi sawa lini, inaweza kuwa kesho, wiki ijayo, mwezi ujao au mwaka ujao, hakuna ajuaye.
Hivyo wewe endelea na mikakati yako ya ukuzaji wa biashara kama vile hakuna mlipuko unaoendelea.
Endelea na mkakati wako wa masoko kwenye matangazo na hata kuwatembelea wateja kule walipo, mtaa kwa mtaa, ofisi kwa ofisi na nyumba kwa nyumba. Ila hakikisha unajikinga na kuikinga timu yako.
Endelea na mkakati wa mauzo kwa kuwashawishi wateja kununua na kununua zaidi ya walivyopanga kununua.
Endelea na mkakati wa utoaji wa huduma bora sana kwa wateja wako ili wanunue tena kwako na wawaambie watu wao wa karibu kununua
Mikakati hii inapaswa kufanyiwa kazi kila siku, iwe kuna majanga au hakuna. Hata kama huoni matokeo yake kwa haraka, usiache kufanya.

Mfano; mikakati ya masoko, mauzo na huduma kwa wateja kwenye kila biashara inapaswa kuendelea kama vile hakuna kilichobadilika, ila iendane na hali halisi ilivyo sasa.

No comments:

Post a Comment