Saturday, April 4, 2020

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : TOA ELIMU NA USHAURI SAHIHI KWA WATEJA WAKO,

Kwenye mlipuko unaoendelea sasa, kila mtu ni mwalimu, mshauri na mtaalamu wa magonjwa ya mlipuko. Hata mtu ambaye mwezi mmoja uliopita alikuwa hajui (na huenda mpaka sasa) hajui kwamba kirusi siyo kiumbe hai kamili, ni mshauri mzuri sana kwa wengine kuhusu mlipuko unaoendelea.

Wewe wape wateja wako elimu sahihi, ambayo umeitoa kwenye vyanzo sahihi. Usilete ujuaji wako au kukusanya taarifa za mtandaoni na kufikiri hiyo ni elimu. Nenda kwenye vyanzo vya uhakika, na kwa hili la Corona, sikiliza taarifa za serikali na tembelea tovuti ya Shirika la Afya Duniani (WHO), kwa anuani www.who.int kupata elimu sahihi kuhusu mlipuko huu wa Corona.
Mfano; kuna vitu vingi ambavyo watu wanashauriana kufanya, ambavyo siyo sahihi. Kwenye tovuti ya WHO, kuna kipengele wanakiita MYTH BUSTERS ambapo wanatoa ukweli kuhusu vitu visivyo sahihi wanavyoshauriana watu. Kama ulaji wa vitunguu hauzuii maambukizi ya Corona. Ingia kwenye tovuti hiyo, pata taarifa sahihi na kisha washauri wateja wako kwa usahihi.

No comments:

Post a Comment