Saturday, April 4, 2020

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : USITUMIE NAFASI HII KUNUFAIKA ZAIDI.

Katika hali ya mlipuko kama huu, ambapo watu hawana uhakika wa lini hali itarudi kama kawaida, wanakimbilia kufanya manunuzi makubwa. Hapa mfanyabiashara unapata tamaa ya kuongeza bei kwa sababu uhitaji ni mkubwa. Watu wanaweza kununua kwa bei juu kwa sababu hawana namna.
Lakini tambua kwamba huu mlipuko utapita, na kama unataka biashara yako iendelee kuwepo na iwe na wateja waaminifu hata baada ya mlipuko huu, usiutumie kujinufaisha zaidi.
Usiongeze bei kwa sababu tu kila mtu anaongeza bei na uhitaji ni mkubwa. Kama ulikuwa na mzigo wa kutosha kabla ya janga hili kuanza, endelea kuuza kwa bei zile zile. Na kama uhitaji ni mkubwa, wape kipaumbele wale wateja ambao umekuwa nao kwa muda mrefu.
Kama mlipuko umepelekea gharama za wewe kupata unachouza kuwa juu, waeleze wazi wateja wako kuhusu mabadiliko hayo. Usikimbilie tu kupandisha bei, jua wateja hawatasahau hilo na watavunja uaminifu kwenye biashara yako baada ya janga hili kupita.

Mfano; wauzaji wa vitu muhimu kama dawa, vifaa vya kujikinga, vyakula na vitu vingine wamekuwa wanapandisha bei katika nyakati kama hizi, wewe usifanye hivyo.

No comments:

Post a Comment