Monday, April 13, 2020

VIPAUMBELE VYAKO NI VIPI ? KAMA UNATAKA KITU KIFANYIKE , MPE MTU ALIYE BIZE

Huwa tunajidanganya kwamba hatuna muda wa kufanya vitu kwa sababu tupo bize.

Ila ukweli ni kwamba, kama kuna kitu unataka kufanya, basi utakifanya vizuri ukiwa bize kuliko ukiwa hauko bize.
Angalia, kipindi kama hiki ambapo watu wengi hawana kazi nyingi za kufanya, ungetegemea uwe ndiyo watu wangeutumia muda huu vizuri kusoma na kujifunza.


Lakini waangalie watu wanafanya nini, kufuatilia habari na mitandao siku nzima.


Hali hii inasababishwa na kukosa vipaumbele.
Unapokuwa bize unajiwekea vipaumbele na kukazana kuvifikia.
Lakini unapokuwa haupo bize, unakosa vipaumbele, hivyo hata kitu kidogo kinakushinda kufanya.

No comments:

Post a Comment