Saturday, April 4, 2020

MFANYABIASHARA / MJASIRIAMALI : JIANDAE KWA MABADILIKO MAKUBWA YANAYOKUJA.

Kuna watu wanasema kwamba ugonjwa huu wa Corona ni mwisho wa dunia. Hilo ni kweli, lakini siyo kwa wanavyomaanisha wao. Corona siyo mwisho wa dunia kwamba watu wote watakufa. Ila Corona ni mwisho wa dunia kwamba baada ya janga hili kupita, dunia mpya itazaliwa, kila kitu kitabadilika.

Hakuna chochote kitakachobaki kama kilivyokua kabla ya Corona. Kuanzia mfumo wa afya, mfumo wa uchumi, ushirikiano wa kimataifa, ufanyaji kazi wa watu na hata tabia za wateja.
Watu kufanyia kazi majumbani kutaongezeka, matumizi ya fedha za noti na sarafu yatapungua, tabia ya watu kunawa mikono itaendelea na mengine mengi ambayo yanasisitizwa sana kipindi hiki.
Hivyo angalia ni jinsi gani biashara yako inaathirika na yale yanayoendelea sasa, kisha usijipe moyo kwamba hali hii itapita na biashara zitarudi kawaida. Jua kwamba hii ndiyo kawaida mpya.
Iandae biashara yako kuendana na mabadiliko yaliyopo sasa na mengine makubwa zaidi yanayokuja. Kufanya biashara kwa ukawaida na mazoea kumefika ukomo. Huu ni wakati wa mabadiliko, hivyo badilika la sivyo utakufa.

Mfano; biashara ambazo zilikuwa zinasubiri wateja kwenda kununua, zinapaswa kubadilika na kuweka mfumo wa wateja kuagiza na kisha kupelekewa au kutumiwa.

No comments:

Post a Comment