Tuesday, July 23, 2019

JUA UNAKOKWENDA.

Kama hujui unakokwenda, huwezi kufika na hata ukifika hutajua kama umefika. Hatua ya kwanza kuchukua ili kupata unachotaka ni kujua wapi unapokwenda.
Unapaswa kujua kwamba kila mtu kwenye maisha kuna kitu anauza, iwe upo kwenye biashara au ajira, hivyo jua ni nini unachouza na uweze kukiuza vizuri zaidi.
Zipo njia tatu za kukuwezesha kuuza zaidi, kupata wateja wapya, kuuza zaidi kwa wateja ulionao na kuwafanya wateja ulionao waje kununua mara nyingi zaidi.
Kama umeajiriwa, unauza muda wako, utaalamu wako na uzoefu wako kwa mwajiri wako. Na kitu kimoja ambacho kila mwajiri anapenda sana ni mtu ambaye anaweza kutatua matatizo na siyo anayesababisha matatizo.
Chochote unachochagua kufanya, hakikisha unakifanya kwa utofauti mkubwa na wengine wanavyokifanya. Usikubali kufanya kwa mazoea au kuiga kile ambacho wengine wanafanya.
Wape wateja wako urahisi wa kusema ndiyo kwa kile unachouza, kwa kutoa thamani kubwa sana ambayo hawawezi kuipata sehemu nyingine yoyote ile. Yaani unapaswa kutoa thamani kubwa kiasi kwamba mteja atajiona ni mjinga kujaribu kutafuta sehemu nyingine ya kununua.

No comments:

Post a Comment