Tuesday, January 1, 2019

MAMBO 18 YA KUFANYA KILA SIKU ILI KUPATA MAFANIKO MAKUBWA SANA.

1. Amka asubuhi na mapema sana, angalau masaa mawili kabla ya muda wako wa kuanza kazi.


2. Unapoamka cha kwanza kufanya shukuru, kwa sala au tahajudi.


3. Andika malengo yako makubwa kila siku unapoamka, malengo ya mwaka, miaka 5, miaka 10 na hata miaka 50. Lazima uwe na malengo ya aina hii.


4. Ipangilie siku yako kabla hujaianza, weka vipaumbele vyako kwa siku husika, viwe kati ya 3 mpaka sita. Andika kabisa nini utafanya na kwa muda gani wa siku hiyo.


5. Soma kitabu au pata maarifa yoyote chanya na ya hamasa kabla hujaianza siku yako. soma angalau kurasa kumi za kitabu kila siku.


6. Fanya mazoezi ya viungo kabla ya kuianza siku yako, mazoezi bora kabisa ni kukimbia.


7. Epuka habari au kitu chochote hasi muda wa asubuhi. Usisikilize redio, wala kuangalia tv au kusoma magazeti.


8. Unapoingia kwenye kazi au biashara yako, fuata vipaumbele ulivyoweka vya kufanya kazi, na unapokamilisha jukumu weka alama ya vema kisha nenda kwenye jukumu jingine.


9. Fanya jambo moja kwa wakati, usifanye mambo mengi kwa wakati mmoja, unapoteza nguvu na umakini.


10. Unapofanya kazi, akili na mawazo yako yote yawe kwenye kile unachofanya, usiwe unafanya kazi huku unafikiria vitu vingine.


11. Kula kwa afya, punguza sana vyakula vya wanga na sukari, kula matunda na mbogamboga kwa wingi na kunywa maji mengi zaidi, angalau lita tatu kwa siku nzima.


12. Ondoka kwenye mitandao yote ya kijamii unayotumia kama haikuingizii fedha moja kwa moja. Sheria ya kutumia mitandao ya kijamii iwe hii, iwe inakuingizia fedha moja kwa moja. Kama hakuna fedha inayoingia kupitia mitandao hiyo, achana nayo mara moja.


13. Acha kabisa kutumia kilevi cha aina yoyote ile, kuanzia pombe, sigara, madawa ya kulevya na hata viburudisho kama kahawa.


14. Kwenye kila kipato unachoingiza, sehemu ya kumi ya kipato hicho usitumie kwa namna yoyote ile, hicho ni kipato ulichojilipa na utakitumia kwa kuwekeza kwa ajili ya baadaye.


15. Imarisha sana mahusiano yako na watu wote wa karibu kwako, kuanzia familia yako, ndugu, jamaa na marafiki na pia wale unaohusiana nao kwenye kazi au biashara.


16. Imalize siku yako kwa kutafakari yale uliyofanya, matokeo uliyopata, makosa au changamoto ulizokutana nazo na namna unavyoweza kufanya kwa ubora zaidi siku inayofuata.


17. Lala mapema ili uweze kuamka mapema, kama hufanyi kazi za usiku, saa nne inapaswa kukukuta kitandani ukiwa umeshalala.


18. Tumia neno HAPANA mara nyingi uwezavyo, neno hapana ndiyo litakupa uhuru wako. Kama kitu hakikuwezeshi kufika kule unakotaka kufika, sema hapana bila ya kuona aibu.
Ndimi  MWL  JAPHET   MASATU, DAR  ES  SALAAM , TANZANIA.
MOBILE  PHONE: WhatsApp +255 716924136 / +255 755400128 /   +255 688 361 539
EMAIL: japhetmasatu@gmail.com
 

No comments:

Post a Comment