Saturday, January 26, 2019

VITABU VIZURI VYA KUSOMA.

---The Monk who sold his Ferrari – Robin Sharma. Katika kitabu hiki, Sharma ananifundisha kuwa mafanikio ya nje hayana maana ikiwa mafanikio ya ndani (i.e. mwili, roho, na nafsi) hayajakaa sawa. Pia siri ya furaha si ngumu. Ni kutafuta kile unachokipenda kukifanya, kisha elekeza nguvu na maisha yako yote katika kukifanya hicho tu. Ukijijua, umeyajua maisha.

-----How to live on 24 hours a day - Arnold Bennett. Jamaa huyu ananifundisha kuwa, muda wa ziada kufanikisha mipango ya mafanikio unaweza kupatikana: mwanzoni mwa siku, kwa kuamka mapema, njiani kuelekea kazini, njiani kurudi nyumbani baada ya kazi, masaa ya jioni, mwisho wa wiki.

----Who Moved My Cheese? - Spencer Johnson. Kitabu kinaeleza kwa njia ya simulizi njia ya ajabu ya kushughulika na mabadiliko katika kazi na katika maisha. Kwa hiyo, mkao sahihi kwenye maisha ni kukubali kwamba mabadiliko yapo, yatarajie, fuatilia mabadiliko, endana na mabadiliko, badilika na yafurahia mabadiliko.

-----The Law of Success – Napoleon Hill. Ni hizi sarafu ndogondogo tunazozidharau na kuzipuuza zingeweza kutuletea uhuru wa kifedha kama tungedumu katika tungeziweka akiba na kuwekeza. “The nickels, dimes and pennies which the average person allows to slip through his fingers would, if systematically saved and properly put to work, eventually bring financial independence.”

---- How to achieve total success in life – Dr. C.S. Chopra. Kwa habari ya mafanikio, Chopra naye anakazia umuhimu wa kuanza na picha ya mwisho unakotaka kufika kisha kujenga mfumo wa kufika huko.

No comments:

Post a Comment